The Genius
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 820
- 2,070
Kitabu cha kwanza kutafsiriwa kwenda kwenye lugha nyingi ni Biblia, Ambayo ilitafsiriwa kwenda kwenye lugha takribani 3589.
Kitabu cha pili kutafsiriwa kwa lugha nyingi ni Don Quixote, riwaya iliyoandikwa na Miguel de Cervantes (Pichani), Riwaya hii huhesabiwa kuwa ni riwaya bora ulaya nzima, Na ilitafsiriwa kwa lugha zaidi ya 140.
Mwandishi wa Riwaya hii bwana Miguel alikua mtoto wa Daktari huko Uhispania, Alijiunga na jeshi akiwa na miaka 23 tu.
Alipokua akipigania nchi ya yake dhidi ya Milki ya Osman, Alijeruhiwa vibaya na kupoteza mkono wake wa Kulia.
Aliwahi kukamatwa na maharamia wa Algeria mwaka 1575 na kufungwa, Kisha akanunuliwa na Wamonaki Wakatoliki kama mtumwa kisha kuachiwa huru kwenda Nyumbani.
Aliwahi fanya kazi ya kukusanya Kodi miaka ya 1584 alipoteza sana Hesabu, kitendo kilichomfanya awekwe jela, ndipo kuanza Uandishi.
Mpaka anakufa alikua maskini, sifa za Uandishi wake zimekuja kupatikana baadae sana.
Kitabu cha pili kutafsiriwa kwa lugha nyingi ni Don Quixote, riwaya iliyoandikwa na Miguel de Cervantes (Pichani), Riwaya hii huhesabiwa kuwa ni riwaya bora ulaya nzima, Na ilitafsiriwa kwa lugha zaidi ya 140.
Mwandishi wa Riwaya hii bwana Miguel alikua mtoto wa Daktari huko Uhispania, Alijiunga na jeshi akiwa na miaka 23 tu.
Alipokua akipigania nchi ya yake dhidi ya Milki ya Osman, Alijeruhiwa vibaya na kupoteza mkono wake wa Kulia.
Aliwahi kukamatwa na maharamia wa Algeria mwaka 1575 na kufungwa, Kisha akanunuliwa na Wamonaki Wakatoliki kama mtumwa kisha kuachiwa huru kwenda Nyumbani.
Aliwahi fanya kazi ya kukusanya Kodi miaka ya 1584 alipoteza sana Hesabu, kitendo kilichomfanya awekwe jela, ndipo kuanza Uandishi.
Mpaka anakufa alikua maskini, sifa za Uandishi wake zimekuja kupatikana baadae sana.