Kijana wa namna hii tukimfukuza ni kosa?

Wanajamvi napenda kuwasalimu kwa jina la jamuhuri, na niwatakieni mapumziko mema.

Wakuu kuna dogo kaja Dodoma hapa yuko UDOM hapo anasoma tumempa hifadhi ghetto hapa. Ila vitabia vyake vinaenda kutushinda na tumefikiria kumtimua baada ya kumuonya sana ni hivi tuna kaofisi hapa ambako kanatusaidia kusogeza siku sasa dogo akitoka chuo anakuja tunashinda nae hapa sasa dogo anakatabia ka kumzunguka mtu unaongea na mteja badae na yeye anaenda ongea nae unashangaa dogo ndio anachukua kazi nikitoka kidogo ukirudi unakuta kapatania kazi yako pesa kachukua sasa tumemuonya mara kibao hasikii anafanya kama makusudi.

Huyu mwenzangu alitaka mtimua kitambo nikawa namwambia amwache tuone kama atajirekebisha lakini naona kijana ndio kwanza anakuja kwa kasi ya 5g sasa uvumilivu umetushindwa kweli dogo namuonea imani ila ni kichwa ngumu. Maana mimi binafsi nishapitia msoto Tanga huko nikapewa hifadhi na mshikaji so naelewa venye wanaume tunatakiwa tuishi ila huyu dogo ataturudisha kwenye dhiki.

Anamambo mengi ya ovyo kama kuchukua mademu wa washikaji n.k ila hayo yanavumilika maana unaona kabisa ni balehe inamsumbua ila hadi huku kwenye pesa waungwana.

Kwani tukimwambia aondoke tutakua tumekosea wakuu?
Ngoja akugongee demu wako ndio utajua kuw hujui
 
Dom vijana wengi ni mapusha wanauza bange usikute mmefundisha wenyewe kunyonga ganja sahiv amekua mtaalam zaid yenu
 
Kwa kuwa wewe walikuvumilia huko Tanga. Ukaamua kutoka moyoni usimfukuze basi kaa naye hata kama wenzako wakitaka muondoke ondoka naye mkaishi. Huo ndiyo upendo wa kweli
dogo ni wa kahama huko hata kwao sipajui ni tofauti na walioniop hifadhi tanga
 
Ubaya wa watu wa hivyo ni kuwa wewe unamuonea huruma lakini yeye anajiona mjanja na kukuona zuzu.
 
Hapo mchongo ni kachukua demu either way huyo mskaji au wako hayo masuala ya kuzungukana kwenye kazi geresha tu, jamaa kiwembe atawatombea Sana mademu wenu 🤣🤣
afu meku kwa umri nilioko sio wa kuwa na ushamba wa wanawake na pia level ya uchumi nilioko nikiwaendekeza hakuna mahali nitafika so na kingine huku changombe niliko huwezi sema huyu ni demu wako ukimkazia mshikaji ataenda gongwa na wengine. Ishu ya dogo ni kupatania kazi kwenye ofisi ya mtu na kuingia mitini na pesa yote bila aibu huku hata dawa ya mswaki hanunui kila kitu unamfanyia kama mwanao tena boom likimuisha na msosi na maji ya kunywa tunamsapport kiaina afu ukipatania kitu anakuzunguka tushamwambia mara kibao haelewi
 
Mpige marufuku kukanyaga ofisini kwako...uone kama atakuelewa asipokuelewa mpige Ban ya Maisha mazima kunusa harufu yako au ya popote utakapokuwa maana huo mwendo aliyo nao si wapolepole atamaliza pesa kwenye kibubu.
 
Wanaume tumebaki wachache Sana hili jambo nalo nila kuomba ushauri kweli
Man ushawahi kula msoto ivi afu ukapata hifadhi na watu hata huwajui wakusaidia kama ndugu ndio utajua kwanini huyu dogo hatujamtimua mpaka sasa na nikaja omba ushauri huku kila nikitaka mfukuza najihisi kama nitakua na hatia ndio maana nikaja huku kupata msukumo na nisijihisi kama na hatia maana mimi mwenyew sijamaliza hata mwaka dodoma na tulipokelewa hivo hivo
 
Back
Top Bottom