Nimelizwa, nimeumizwa na kufadhaishwa mno na kifo cha kijana huyu

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,293
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Kabla ya yote, ningependa niweke wazi kuhusu jinsi nilivyofahamiana na huyu kijana kupitia uncle wake ambae niliwahi kufanya nae kazi katika kampuni fulan, miaka kadhaa iliyopita.

Kijana ninaemzungumzia hapa anaitwa Jems, na huyo mjomba wake ambae alikuwa rafiki yang alikuwa anaitwa Ramadhan. Ilikuaje hadi kufariki kwake, naomba unifuatilie hapo chini.

Jems ni kijana aliezaliwa mwaka 1997, katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Alikuwa mtoto wa kwanza katika familia ya watoto wa tatu, ambapo waliomfuata kwa kuzaliwa alikuwa mwanaume pia alieitwa Janvier (January) na wa mwisho mwanamk alieitwa Julieta.

Mwaka 2011, waasi wa M23 walivamia kijiji chao na kuuwa makumi ya wanavijiji. Hali hiyo ilipelekea Jems, ndugu zake na wazazi wake watoroke kwao ili kwenda kutafuta hifadhi sehem nyingine. Kwa vile ilikuwa usiku, basi Jems akapoteana na wazazi wake pamoja na ndugu zake.

Jems akakimbilia katika kambi ya ndan nje ya kijiji chao, ambapo alikutana na huyu rafiki yang alieitwa Ramadhan ambae alikuwa amekwenda kwao kutembea na kukutana na mkasa huo siku chache baada ya kufika.

Huyu rama hakuwa na undugu na Jems, lkn alijikuta anaguswa na yaliomkuta huyo dogo ambae tayari alikuwa ashapoteana na wazazi wake.

Baada ya kukaa kambini kwa muda, waliamua kukimbilia Tanzania kambini mkoani Kigoma ambapo walikaa kwa muda wa miaka miwili na nusu.

Mwaka 2014, Rama na dogo Jems wakaanza safari ya kuja Kaburu kutafuta hifadhi ya uhakika. Ikumbukwe Rama tayari alikuwa ni mkazi wa huku, ila alikwenda kwao kusalimia na kuona familia yake. So njia za kufika Kaburu alikuwa anazijua na pesa kidogo alikuwa nayo, ingawa nyingine pamoja na vitu aliviacha baada ya uvamizi ule wa ghafla wa waasi.

Baada ya kujikongoja na kijana wake huyo waliejuana nae njiani, mwaka 2015 wakafanikiwa kuingia Kaburu.

Baada ya kufika rama alianza kazi kama kawaida, ila Jems kwa vile alikuwa mgeni ilibidi aanze kwanza kukaa nyumban mpaka pale vibali vyake vya ukimbizi vitakavyokuwa tayari.

Baada ya vibali kuwa tayari Rama alimuuliza Jems kuwa anataka asome au afanye kazi, Jems akachagua kusoma. Basi Rama akafanya makeke dogo akafanikiwa kupata shule.

Baadae dogo akawa anasoma huku anajifunza kazi nyingine ya mkono (kunyoa)

Muda wote dogo hakuwa na amani moyoni mwake, maana hakuwa anafahamu mustakabali wa wazazi wake kwamba wamefariki au wako hai somewhere.

Mwaka 2019, akabahatika kupata mawasiliana na familia yake, kumbe inasemekana wazazi walikimbilia Uganda na baadae wakarudi, ila mdogo wake wa kumfuata Janvier alikuwa ameuwawa katika uvamizi mungine uliofanywa muda mfupi na waasi baada ya wazazi wake hao kurejea nyumbani toka ukimbizini Uganda.

Dogo alilia kwa uchungu mkubwa, ila sisi kama wajomba zake tulikuwa na kazi ya kumtuliza na kumliwaza.
Rama alimpenda, alimthamini na kumjali huyu dogo kama vile mtu anavyomjali mtoto wake au ndugu yake wa damu.

Hakuwahi kumbagua kwa lolote, na hata dogo Jems na yeye alipoanza kuongea na wazazi wake aliwambia kuhusu ambae alikutana nae njiani na kuamua kumsaidia kama mtoto wake au mtoto wa ndugu yake, kiasi kwamb wazazi waliguswa na msaada ule wa Rama na kuahidi siku atakayokwenda tena Congo kutembea watamwalika kwao na kumfanyia sherehe kubwa kama vile ndugu yao.

Mambo yalibadilika mwaka 2021, baada ya Rama kupatwa na maambukizi ya korona ambapo alifariki muda mfupi tu baada ya kufikishwa hospital. Kilio kile kilikuwa cha wote, lkn kilimuumiza zaidi Jems ambae kwake yeye Rama alikuwa ni sawa na mzazi wa kumzaa.

Baada ya kilio kuisha huku tukiendelea kumueleza kwamba ile ni kazi ya Mungu na kamwe huwa haina makosa. Basi ikabidi akubaliane na matokeo kwamba kweli Mungu amechukua kilicho chake. Dogo akakonda na kupoteza nguvu za mwili kutokana na kuwaza sana juu ya kifo cha uncle wake Rama.

Hajakaa sawa, mwaka huu miezi ya mwanzo akapokea tena taarifa kuwa wazazi wake wote wawili pamoja na dada yake waliuwawa na waasi huko Congo.

Wazazi waliuwawa kwa mapanga, huku dada yake akiuwawa kwa maumivu ya kubakwa na kundi la waasi hao.
Hapo ndo dogo alipotaka kuwa chizi kabisa, ilihitaji kazi ya ziada kutoka kwetu ili kumuweka dogo katika hali ya kawaida.

Ilifika kipindi mpaka tuliona dogo anaweza kujiuwa mwenyew, kwahiyo watu tukaamua awe anaishi na dogo mungine (rafiki yake) katika nyumba aliyokuwa anaishi na marehem Rama ambae alichukua nyumba nzima (flat) na kuweka wapangaji katika vyumba vingine.

Baada ya miezi kadhaa dogo akaomba tumsaidia kumchangia changia ili arudi kwao Congo maana haoni tena sababu ya kukiogopa kifo au kuishi mbali na kwao. Wengi tulijaribu kumsihi kuwa abaki tu huku maana kule hali bado haijawa shwari, lkn yey alikataa kwa madai kuwa wazazi wake waliacha nyumba na mifugo kwahiyo kwa sasa hajui ni nani anaeiangalia nyumba na mifugo hiyo.

Akasema ni bora aende akafanye mpango wa kuuza hiyo nyumba afu atafute nchi nyingine ya kwenda kama ni kurudi huku au aende Tanzania, au Kenya au Uganda.

Baada ya kuona dogo ashapoteza muelekeo wa kuishi au wa maisha ikabidi tukubaliane na ushauri wake, ila tulimtaka auze nyumba na kuwahi kutoka kabla wale jamaa hawajavamia tena kijiji chao, akakubali. Tukachanga ikapatikana kiasi fulan cha hela ambayo ilimsaidia nauli na nyingine ya kuanzia maisha huko aendako.

Dogo alisafiri na kufika kwao salama, na muda mwingi tulikuwa tunawasiliana nae na kushauriana mambo mbali mbali ya kimaisha.

Wakati akiwa katika mchakato wa kupata mteja wa kumuuzia nyumba, ghafla kijiji kikavamiwa na waasi tena ambapo yeye alikuwa ni mmoja wa waliouwawa na waasi hao.

Sisi tulipokuwa tunamtafuta tulimkosa, tukajua labda dogo amepoteza sim, au ashauza ila yuko njiania anakuja.

Ghafla tukapata taarifa kutoka kwa aliekuwa jirani yao ambae alikuwa anafamiana na mkongo mmoja anaeishi huku, kwamb Jems aliuwawa kwa kuchomwa moto na waasi hao akiwa ndani ya nyumba yao amelala usiku. Ni mauaji ambayo yamechukua maisha ya wakongo wengi katika eneo hilo.

Baada ya taarifa hiyo ki ukweli nilijukuta nalia bila kujijua. Dogo amepitia changamoto nyingi za maisha na sasa mwisho wake umekuwa wakusikitisha zaidi.

Walaaniwe hawa waasi wa M23 na wengineo wanaouwa maelfu ya raia wasiokuwa na hatia huko Congo na ulimwenguni kwa ujumla. Dah nimejikuta sina cha kuongea zaidi ya kumtakia pumziko jema dogo Jems.

Inna lillah wainna illayhi rajiun (Sisi wote ni wa Mungu, na kwake Mungu tutarejea)

Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Mungu ailaze roho yake na wazazi wake mahali pema peponi amiin.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Kabla ya yote, ningependa niweke wazi kuhusu jinsi nilivyofahamiana na huyu kijana kupitia uncle wake ambae niliwahi kufanya nae kazi katika kampuni fulan, miaka kadhaa iliyopita.

Kijana ninaemzungumzia hapa anaitwa Jems, na huyo mjomba wake ambae alikuwa rafiki yang alikuwa anaitwa Ramadhan. Ilikuaje hadi kufariki kwake, naomba unifuatilie hapo chini.

Jems ni kijana aliezaliwa mwaka 1997, katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Alikuwa mtoto wa kwanza katika familia ya watoto wa tatu, ambapo waliomfuata kwa kuzaliwa alikuwa mwanaume pia alieitwa Janvier (January) na wa mwisho mwanamk alieitwa Julieta.

Mwaka 2011, waasi wa M23 walivamia kijiji chao na kuuwa makumi ya wanavijiji. Hali hiyo ilipelekea Jems, ndugu zake na wazazi wake watoroke kwao ili kwenda kutafuta hifadhi sehem nyingine. Kwa vile ilikuwa usiku, basi Jems akapoteana na wazazi wake pamoja na ndugu zake.

Jems akakimbilia katika kambi ya ndan nje ya kijiji chao, ambapo alikutana na huyu rafiki yang alieitwa Ramadhan ambae alikuwa amekwenda kwao kutembea na kukutana na mkasa huo siku chache baada ya kufika.

Huyu rama hakuwa na undugu na Jems, lkn alijikuta anaguswa na yaliomkuta huyo dogo ambae tayari alikuwa ashapoteana na wazazi wake.

Baada ya kukaa kambini kwa muda, waliamua kukimbilia Tanzania kambini mkoani Kigoma ambapo walikaa kwa muda wa miaka miwili na nusu.

Mwaka 2014, Rama na dogo Jems wakaanza safari ya kuja Kaburu kutafuta hifadhi ya uhakika. Ikumbukwe Rama tayari alikuwa ni mkazi wa huku, ila alikwenda kwao kusalimia na kuona familia yake. So njia za kufika Kaburu alikuwa anazijua na pesa kidogo alikuwa nayo, ingawa nyingine pamoja na vitu aliviacha baada ya uvamizi ule wa ghafla wa waasi.

Baada ya kujikongoja na kijana wake huyo waliejuana nae njiani, mwaka 2015 wakafanikiwa kuingia Kaburu.

Baada ya kufika rama alianza kazi kama kawaida, ila Jems kwa vile alikuwa mgeni ilibidi aanze kwanza kukaa nyumban mpaka pale vibali vyake vya ukimbizi vitakavyokuwa tayari.

Baada ya vibali kuwa tayari Rama alimuuliza Jems kuwa anataka asome au afanye kazi, Jems akachagua kusoma. Basi Rama akafanya makeke dogo akafanikiwa kupata shule.

Baadae dogo akawa anasoma huku anajifunza kazi nyingine ya mkono (kunyoa)

Muda wote dogo hakuwa na amani moyoni mwake, maana hakuwa anafahamu mustakabali wa wazazi wake kwamba wamefariki au wako hai somewhere.

Mwaka 2019, akabahatika kupata mawasiliana na familia yake, kumbe inasemekana wazazi walikimbilia Uganda na baadae wakarudi, ila mdogo wake wa kumfuata Janvier alikuwa ameuwawa katika uvamizi mungine uliofanywa muda mfupi na waasi baada ya wazazi wake hao kurejea nyumbani toka ukimbizini Uganda.

Dogo alilia kwa uchungu mkubwa, ila sisi kama wajomba zake tulikuwa na kazi ya kumtuliza na kumliwaza.
Rama alimpenda, alimthamini na kumjali huyu dogo kama vile mtu anavyomjali mtoto wake au ndugu yake wa damu.

Hakuwahi kumbagua kwa lolote, na hata dogo Jems na yeye alipoanza kuongea na wazazi wake aliwambia kuhusu ambae alikutana nae njiani na kuamua kumsaidia kama mtoto wake au mtoto wa ndugu yake, kiasi kwamb wazazi waliguswa na msaada ule wa Rama na kuahidi siku atakayokwenda tena Congo kutembea watamwalika kwao na kumfanyia sherehe kubwa kama vile ndugu yao.

Mambo yalibadilika mwaka 2021, baada ya Rama kupatwa na maambukizi ya korona ambapo alifariki muda mfupi tu baada ya kufikishwa hospital. Kilio kile kilikuwa cha wote, lkn kilimuumiza zaidi Jems ambae kwake yeye Rama alikuwa ni sawa na mzazi wa kumzaa.

Baada ya kilio kuisha huku tukiendelea kumueleza kwamba ile ni kazi ya Mungu na kamwe huwa haina makosa. Basi ikabidi akubaliane na matokeo kwamba kweli Mungu amechukua kilicho chake. Dogo akakonda na kupoteza nguvu za mwili kutokana na kuwaza sana juu ya kifo cha uncle wake Rama.

Hajakaa sawa, mwaka huu miezi ya mwanzo akapokea tena taarifa kuwa wazazi wake wote wawili pamoja na dada yake waliuwawa na waasi huko Congo.

Wazazi waliuwawa kwa mapanga, huku dada yake akiuwawa kwa maumivu ya kubakwa na kundi la waasi hao.
Hapo ndo dogo alipotaka kuwa chizi kabisa, ilihitaji kazi ya ziada kutoka kwetu ili kumuweka dogo katika hali ya kawaida.

Ilifika kipindi mpaka tuliona dogo anaweza kujiuwa mwenyew, kwahiyo watu tukaamua awe anaishi na dogo mungine (rafiki yake) katika nyumba aliyokuwa anaishi na marehem Rama ambae alichukua nyumba nzima (flat) na kuweka wapangaji katika vyumba vingine.

Baada ya miezi kadhaa dogo akaomba tumsaidia kumchangia changia ili arudi kwao Congo maana haoni tena sababu ya kukiogopa kifo au kuishi mbali na kwao. Wengi tulijaribu kumsihi kuwa abaki tu huku maana kule hali bado haijawa shwari, lkn yey alikataa kwa madai kuwa wazazi wake waliacha nyumba na mifugo kwahiyo kwa sasa hajui ni nani anaeiangalia nyumba na mifugo hiyo.

Akasema ni bora aende akafanye mpango wa kuuza hiyo nyumba afu atafute nchi nyingine ya kwenda kama ni kurudi huku au aende Tanzania, au Kenya au Uganda.

Baada ya kuona dogo ashapoteza muelekeo wa kuishi au wa maisha ikabidi tukubaliane na ushauri wake, ila tulimtaka auze nyumba na kuwahi kutoka kabla wale jamaa hawajavamia tena kijiji chao, akakubali. Tukachanga ikapatikana kiasi fulan cha hela ambayo ilimsaidia nauli na nyingine ya kuanzia maisha huko aendako.

Dogo alisafiri na kufika kwao salama, na muda mwingi tulikuwa tunawasiliana nae na kushauriana mambo mbali mbali ya kimaisha.

Wakati akiwa katika mchakato wa kupata mteja wa kumuuzia nyumba, ghafla kijiji kikavamiwa na waasi tena ambapo yeye alikuwa ni mmoja wa waliouwawa na waasi hao.

Sisi tulipokuwa tunamtafuta tulimkosa, tukajua labda dogo amepoteza sim, au ashauza ila yuko njiania anakuja.

Ghafla tukapata taarifa kutoka kwa aliekuwa jirani yao ambae alikuwa anafamiana na mkongo mmoja anaeishi huku, kwamb Jems aliuwawa kwa kuchomwa moto na waasi hao akiwa ndani ya nyumba yao amelala usiku. Ni mauaji ambayo yamechukua maisha ya wakongo wengi katika eneo hilo.

Baada ya taarifa hiyo ki ukweli nilijukuta nalia bila kujijua. Dogo amepitia changamoto nyingi za maisha na sasa mwisho wake umekuwa wakusikitisha zaidi.

Walaaniwe hawa waasi wa M23 na wengineo wanaouwa maelfu ya raia wasiokuwa na hatia huko Congo na ulimwenguni kwa ujumla. Dah nimejikuta sina cha kuongea zaidi ya kumtakia pumziko jema dogo Jems.

Inna lillah wainna illayhi rajiun (Sisi wote ni wa Mungu, na kwake Mungu tutarejea)

Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Mungu ailaze roho yake na wazazi wake mahali pema peponi amiin.
R.I.P Jems
 
Poleni sana dah! Kuna muda najiuliza huu Umoja wa Afrika unafanya kazi gani!
Ardhi ya Congo haswa ile yenye madini mbali mbali inadhibitiwa na wakubwa wa dunia wakiongozwa na Marekani, na wao ndio chanzo cha yote yanayotokea kule.
Kwahiyo hao Umoja wa Afrika hawawezi kufanya lolote ili kudhibiti hali iliyopo kwa kuwa imeshaandaliwa muda mrefu.
 
Back
Top Bottom