Tetesi: Kigogo: Humphrey Polepole aomba hifadhi Sweden!

Tetesi: Kigogo: Humphrey Polepole aomba hifadhi Sweden!

Sijastushwa na kitendo cha Balozi Polepole kujiuzulu ubalozi na utumishi wa umma kama alivyosema kwenye barua yake kwa kuwa toka mwanzo hakupenda jinsi alivyotolewa kwenye ubunge na nafasi yake akapewa Vuai Shamsi Nahodha.

Haikueleweka kipindi kile kama mbunge wa kuteuliwa anaweza kuvuliwa ubunge na nafasi yake kupewa mtu mwingine!.Kwa kuwa tulikuwa na kawaida ya kukaa kimya na kupuuza mambo hatukuona lile ni tatizo lakini sasa ndiyo jipu limepasuka tunaparanganga kutafuta matambara ya kufuta usaha unaosambaa kwa kasi sana.!

Balozi Polepole amestafu na ameandika barua nzito na kali sana na imetoa shutuma kali sana dhidi ya uongozi wa nchi!. Kitendo cha Balozi Polepole kusema nchi imekosa uongozi ni shutuma nzito sana na hazipaswi kuachwa zipite kimya kimya! Lazima tukiri kuwa kuna tatizo mahali na lazima litazamwe kwa makini sana kama tunaipenda hii nchi.

Kilichonistua zaidi ni kitendo cha Balozi Polepole kukimbilia Sweden na kuomba hadhi ya ukimbizi na kupewa mara baada ya kuandika barua ya kujiuzulu yenye shutuma kali sana dhidi ya uongozi wa nchi.

Kitendo hiki ni kizito na kigumu na kibaya sana kwa taifa na uongozi wa taifa.! Balozi Polepole kaomba ukimbizi Sweden maana yake anahofia usalama wake baada ya kusema aliyoyasema!

Tunapaswa kujitafakari kama taifa!.. Hatuko kwenye njia sahihi na kwa kweli giza ni nene sana huko tuendako.

Pia soma > Humprey Polepole ajiuzulu Ubalozi, asema hawezi kuendelea kuwa sehemu ya uongozi usiohamasika na utii wa misingi ya katiba na chama
hivi mke wake si mswiss?
 
Sweden lazima apate bwana wa kizungu aolewe apate na uraia kabisa.
huyo ameoa mzungu ndio mke wake wanalala kitanda kimoja, sio kama wewe sifuri wa uhambingeto huko umejua kupiga mswaki juzi kwanza unaamini wazungu tu ndio wanapiga mswaki.
 
Sijastushwa na kitendo cha Balozi Polepole kujiuzulu ubalozi na utumishi wa umma kama alivyosema kwenye barua yake kwa kuwa toka mwanzo hakupenda jinsi alivyotolewa kwenye ubunge na nafasi yake akapewa Vuai Shamsi Nahodha.

Haikueleweka kipindi kile kama mbunge wa kuteuliwa anaweza kuvuliwa ubunge na nafasi yake kupewa mtu mwingine!.Kwa kuwa tulikuwa na kawaida ya kukaa kimya na kupuuza mambo hatukuona lile ni tatizo lakini sasa ndiyo jipu limepasuka tunaparanganga kutafuta matambara ya kufuta usaha unaosambaa kwa kasi sana.!

Balozi Polepole amestafu na ameandika barua nzito na kali sana na imetoa shutuma kali sana dhidi ya uongozi wa nchi!. Kitendo cha Balozi Polepole kusema nchi imekosa uongozi ni shutuma nzito sana na hazipaswi kuachwa zipite kimya kimya! Lazima tukiri kuwa kuna tatizo mahali na lazima litazamwe kwa makini sana kama tunaipenda hii nchi.

Kilichonistua zaidi ni kitendo cha Balozi Polepole kukimbilia Sweden na kuomba hadhi ya ukimbizi na kupewa mara baada ya kuandika barua ya kujiuzulu yenye shutuma kali sana dhidi ya uongozi wa nchi.

Kitendo hiki ni kizito na kigumu na kibaya sana kwa taifa na uongozi wa taifa.! Balozi Polepole kaomba ukimbizi Sweden maana yake anahofia usalama wake baada ya kusema aliyoyasema!

Tunapaswa kujitafakari kama taifa!.. Hatuko kwenye njia sahihi na kwa kweli giza ni nene sana huko tuendako.

Pia soma > Humprey Polepole ajiuzulu Ubalozi, asema hawezi kuendelea kuwa sehemu ya uongozi usiohamasika na utii wa misingi ya katiba na chama
hana athari wala madhara yoyote ya kisiasa, kijamii na hata kiuchumi nchini.

hata hivyo,
inafaa aje ajibu tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na uhujumu uchumi 🐒
 
Kwa hiyo wakati anajiandaa kuandika barua alishajiandaa na pa kukimbilia!
Lazima atakuwa ameshajipanga anajua pa kutimkia. Polepole ni mjamaa na ameishi kwenye nchi ya Cuba ambayo ni nchi ya ujamaa yenye mizizi mikubwa. Ukiangalia kwa jicho la tatu Kuna faida kubwa sana kwake kutoka ubalozini Malawi na kupelekwa Cuba.
 
Lazima atakuwa ameshajipanga anajua pa kutimkia. Polepole ni mjamaa na ameishi kwenye nchi ya Cuba ambayo ni nchi ya ujamaa yenye mizizi mikubwa. Ukiangalia kwa jicho la tatu Kuna faida kubwa sana kwake kutoka ubalozini Malawi na kupelekwa Cuba.
hapo ndipo walipokosea mahesabu. wao walijua wanamtupa kisiwani huko.
 
hana athari wala madhara yoyote ya kisiasa, kijamii na hata kiuchumi nchini.

hata hivyo,
inafaa aje ajibu tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na uhujumu uchumi 🐒
Nyie vilaza mnaoinajisi katiba na kuitumia mahakama vibaya kwa masilahi yenu binafsi ya hovyo, mwisho wenu wa kubambikia wananchi wasio na hatia kesi unakaribia. Yote mnayofanya yameanza kuwageuka.
 
Mkuu kipenseli2021 hata wewe pia unaweza kuomba hifadhi kama Kuna viashiria hatarishi ambavyo vitathibitisha maisha yako yapo hatarini na kuendelea kuishi bongo ni hatari kwa usalama wako au familia yako. Kuna michongo ipo UNHCR na shirika la IOM inafanyika. Ishi na watu vizuri upate michongo.
Nitakutafuta Mkuu unipe huo mchongo
 
Sasa Polepole kajihudhuru bila hata kukabidhi office. 🤣🤣🤣
 
hapo ndipo walipokosea mahesabu. wao walijua wanamtupa kisiwani huko.
Kwa ambao wanamfahamu Polepole tokea akiwa Azania, kwenye bunge la maoni ya mchakato wa katiba mpya.
Jamaa ana unyerere mwingi ndani yake na ameuishi. Marehemu Magufuli licha ya mapungufu yake pia alikuwa na unyerere ndio maana walitengeneza perfect combination.
Kule Cuba kwa Mzee Fidel Castro jamaa atakuwa ameiva sana kwenye ujamaa.
 
acha akauzee supermarket akichoka atarudi kuomba msamaa. Huyu hana la kulaumu serikali kwa sababu alikua kwenye serekali iliyo tesa sana watu, alikua kijana wa magufuli huyu, anatakiwa kufatwa huko sweden afungiliwe kesi, atatoa siri zote za walio kuwa wanaokotwa kwenye viroba.
 
Back
Top Bottom