Magari ya kuwasha yamenunuliwa kwa ajili ya wale wanaojifanya vichwa ngumu. Kwa babu yangu na kwa babu yako ni sehemu tu ya Tanzania, kama sio leo kesho maendeleo yatapafikia. Ndio maana Ngosha kafuta safari za nje ya nchi. Ngosha anafanya mambo makubwa kwa sababu ni mzalendo wa kweli, tofauti na yule aliyetoa mabilioni ya fedha na kukinunua chama ili mradi agombee urais. Mtu aliyeutaka urais kwa nguvu zake zote, kama angeingia Ikulu fedha aliyotumia angeilipaje?, kama alikopa angeilipaje?. Na mpaka sasa anailipaje?. Mungu ni mwema, katukwepesha kuingia ndani ya mdomo wa Mamba.