mcshonde
Member
- Jul 15, 2022
- 66
- 152
Kifo cha Norah Vicent kiliibua hisia kwa jamii kutokana na namna utafiti alioufanya ulivyommaliza yeye mwenyewe. Norah alitaka kujua maisha ya mwanaume yakoje..ni changamoto zipi anapitia? Mwaka 2003, bila kubadili jinsia yake, akaamua ajifanye kuwa mwanaume; akaajiri mtu wa make up,mtaalamu wa sauti, pamoja na mwalimu wa mazoezi ya viungo.
Kwa miezi 18 akawa na jina jipya, Ned. Akajiunga timu ya mpira wa wanaume, akaanzisha mahusiano na wanawake, na kufanya kazi kwenye ofisi ya wanaume pekee. Lakini Norah, sasa Ned, hakuona raha yoyote na bila kujijua akaanza kupata msongo wa mawazo...depression. Kwenye kitabu chake "Self-Made Man" akakiri kuwa wanawake, pamoja na wanaharakati, huwa wanaamini wanawake ndio wanapitia magumu mengi katika jamii lakini ukweli ni kwamba wanaume wana machungu mengi katika maisha yao.
Wanaume wanateseka, Wana matatizo tofauti na ya wanawake, lakini bora sisi, wao wanahitaji zaidi upendo, kuonewa huruma" alisema Norah.
Zamani ukizaliwa mwanaume ilionekana ni bahati na nafasi ya upendeleo; lakini kaitka kizazi hiki kuwa mwanaume ni shida. Utafiti uliofanyika mwaka 2020, ulionyesha kuwa 70% ya watu wasio na makazi (homeless) ni wanaume. Pia hatari ya mwanaume kujiua ni mara 4 zaidi ya mwanamke. 90% ya ajali za sehemu ya kazi ni za wanaume
kwa aliyokutana nayo Norah, alipata matatizo ya akili yaliyotesa kwa zaidi ya miaka 17, na mwishowe julai 6, 2022 akaamua kujiua huko Switzeland. Kuwa mwanaume ni kazi.