Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Ukweli ni kuwa vigari hivi vidogo huwa control yake ovyo kabisa. Tena mbaya watu wanaviongezea 'bushes' kitu ambacho huaribu kabisa hata design yake. Na Chacha naona hakuwa na dereva na kumbuka kamtindo ketu ka kuendesha hata kwenye kona ukapokea simu... Halafu alikuwa na safari ya kurudi Tarime (nadhani katika msiba hivi) hivyo mawazo yalikuwa mengi tu, ninachoweza kusema ni kuwa katika hali kama hii Japhet alitakiwa kumsoma mbunge huyu na kumsisitiza kuwa na dereva wakati wote kwakuwa alishamhabarisha juu ya matatizo yake nyumbani.

RIP Chacha! Nenda murra, nasi tunakuja

..definatelly ..wabunge wana umuhimu wa kuwa na madereva....na magari yao yawe na minimum requirements..au bora waendelee kununuliwa kuzuia kuuziwa magari ya dubai....ishu ya wabunge kuwa na madereva..inanikumbusha makongoro ..

yeye alikuwa aliendesha gari kutoka arusha alikotoka kuijulia hali familia yake..na ni muendeshaji mzuri tu ..anayejiamni hata kama amepata...kufika chalinze akawa amechoka ..akamuuliza abiria wake kama anaweza kuendesha akasema sawa...kufika kati kati morogoro ..gari likaingia porini...jamaa akashuka akakimbia..nadhani pia alimuibia...yeye aliendelea kuwa usingizini...hadi alipostuka na kujikuta gari iko porini na ana maumivu makali mgongoni...alilazwa MOI kwa matibabu..all in all kwa mtu yeyote busy you need a proffessional driver....
 
RIP chacha Wangwe
Mungu akupumzishe kwa amani, nasi tuko nyuma yako twaja
Amen
 
Invisible,

Labda ongelea ubovu wa gari lakini kama unaongelea gari ambazo ni safi basi gari ndogo nyingi tu ni bora zaidi kuliko hizo shangingi inapokuja kwenye ajali.

Bahati nzuri wenzetu kila mara huwa wanapima ubora wa gari kwenye ajali na safari zote gari ndogo ni bora zaidi. Una nafasi ya kutoka salama kwenye gari ndogo kuliko hizo shangingi.

Tunadanganywa na hayo mashangingi, yanafaa kwenye kutanua lakini sio ubora kwenye ajali.
Kaka Mtanzania,

Mashangingi ndo ovyo kabisa haswa kwa upande wa stability. Gari ndogo ni stable kama haijanyanyuliwa (wao wanasema kuweka bush). Vinginevyo inakuwa juu lakini at your own risk. Kitu hiki wanakifanya wengi bila kujua side effect yake.
 
Watu wengine wana fikra za kichawichawi vile! Sasa haya yametokea wapi? Kichuguu, tanguliza ubinadamu kwanza...hata kama hujiheshimu na unadhani hufahamiki! Hata kama huheshimu wengine, na marehemu akiwamo, basi jiheshimu nafsi yako inayokusukuma hapa.

Poleni wanafamilia na wapambananaji wote. Mungu alitoa, Mungu ametwaa. Jina la Bwana lihimidiwe!

mkuu unamuheshimu marehemu leo? ungefanya alipokuwa hai kuliko ulivyomdhalilisha kaisi hiki,mmemfuta umakamu lakini bado mkaendelea kumsakama humu na jeshi lako lote.
 
Hamad Rashid Moh'd anasema habari za kifo cha Wangwe zimezua mshtuko mkubwa na ni pigo kubwa kwa kambi ya upinzani. Anasema alikuwa ni mhamasishaji mzuri bungeni na ni pigo kubwa kwa kambi yao.

Huu ni unafiki si jamaa alisema chacha alikua anawatenga bungeni.Imekuaje baada ya kifo kusema alikua muhamasishaji??
 
ni wakati mwingine kwa watanzanania sote tumepoteza mtu muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania haswa katika suala zima la watanzania kuielewa katiba kwani kama sikosei tumepoteza mbunge mahiri na makini katika kutumia katiba ya Jamhuri katika kutetea hoja na kuonyesha upungufu pale ambapo hoja zimejengwa katika mfumo usio thabit kama ni taifa litakuwa limepata pigo kubwa sana kwa msingi huo. kwani elimu yake kwa njia ya vipindi vingi vya bunge tuliweza kuisoma na kuona ya kuwa hali halisi ya viongozi walio wengi kutokujua katiba ni moja ya tatizo kubwa

napenda kumkumbuka kwa hili la muhimu kwani tuna elimu mfumo wa kumaliza syllubus na mfumo wa elimu kwa njia ya kusikia na nina hakika alikuwa mwalimu mzuri wa kutufundisha sisi tulio nje ya ulingo wa siasa lakini ni wapiga kura hivi leo siyo tu Tarime wameondokewa na mwakilishi wao Bungeni bali watanzania tulio wengi tutakosa mtu mwenye hoja pana na anayejua namna ya kuweka bayana mambo kwa mujibu wa katiba ya nchi

mfano wake ni wa kuigwa kwa kweli kwani utawala wa sheria unanzia katika viongozi kuijua katiba ya nchi na hii aliweza kuchangia kwa namna ya pekee kuifanya katiba iwe ndo muhimili mkubwa pale aliposimama bungeni na kutoa hoja mbali mbali zikiwemo kutetea hali tete ya jimbo lake la Tarime haswa kuhusu mapigano ya koo

R I P Mh. Chacha Wangwe
 
Jamani, naona kumekuwa na kulaumiana na kunyoosheana vidole hapa. Nawaomba tuombolezeni kwa amani na tuendelee kutoa sala zetu bila kutoa lawama. Ajali ni ajali, na tulifundishwa kuwa ajali haina kinga. Mheshimiwa Mudhihir alipata ajali wakati akiwa anendesha gari zuri sana. Marehemu Sokoine alipata ajali huku akiwa anaendeshwa na dereva professional tena akiwa na walinzi. Tujifunze kukubali matokeo ya kazi ya Mungu, ingawe wakati mwingine matokeo yake huwa magumu kwetu kumeza, lakini ndiyo ilivyo: Kazi ya Mungu haina makosa
 
Invisible,

Labda ongelea ubovu wa gari lakini kama unaongelea gari ambazo ni safi basi gari ndogo nyingi tu ni bora zaidi kuliko hizo shangingi inapokuja kwenye ajali.

Bahati nzuri wenzetu kila mara huwa wanapima ubora wa gari kwenye ajali na safari zote gari ndogo ni bora zaidi. Una nafasi ya kutoka salama kwenye gari ndogo kuliko hizo shangingi.

Tunadanganywa na hayo mashangingi, yanafaa kwenye kutanua lakini sio ubora kwenye ajali.

LAKINI AIRBAG SYSTEM YA MASHANGINGI NI BORA KULIKO YA MARK 11...,NDIO MAANA WATAALAMU WA USALAMA WANAPENDEKEZA MASHANGINGI KWENYE OFFROAD AU SAFARI NDEFU.......HATA UKICHUNGUZA MISAFARA YA RAIS..OR THE LIKE KAMA ANAENDA SAFARI NDEFU ZAIDI YA KM 100 AU KWENYE BARABARA MBAYA ..HUPANDA MASHANGINGI..YAPO SECURED ZAIDI...

...AIRBAG INASAIDIA SANA..UKIONA ILIVYOMSAIDIA MTU KAMA KAPUYA ..UTAAMINI ...NA UKIONA NAMNA MAMA MBATIA AMBAYE KWA BAHATI MBAYA ILE NISSAN PATROL YAKE ILIKUWA OLD MODEL KIDOGO NA HAIKUWA NA AIRBAG...INGEKUWEPO ANGEWEZA KUTOKA MZIMA.....hata mtu kama MUDHIHIR alipopata ajali na cruizer yake kama sio AIRBAG zaidi ya kuumia angeweza hata kupoteza maisha...

SIKU ZA KARIBUNI WABUNGE WAMEKUWA HAWAPEWI CHAGUO LA MAGARI AMBAYO WANATAKIWA KUYANUNUA YAKIWA MAPYA..BUT I REMEMBER KABLA ..KILA BUNGE JIPYA LINAPOANZA DEALERS WA MAGARI MAPYA...LANDROVER,TOYOTA,NISSAM,MITSUBISHI ..ets walikuwa wanakaribishwa bungeni na wabunge walitakiwa wachague magari miongoni mwa make zinazoaminiwa na serikali.....baadaye naona huu utaratibu umeachwa na hii imesababisha wabunge wengi kuingizwa mkenge na wauzaji wa USED.....najua wabunge wengi tu ambao sasa hivi magari yao yanawasumbua sana...na hayakidhi mahitaji ya wanakotokea ..kutokana na kuchakaa haraka....
 
Inna Lillah Wainna Ilaih Rajiuun!

Uffffffuh!..sina nguvu wala la kusema zaidi ya kumwombea Pepo!..
 
Jamani, naona kumekuwa na kulaumiana na kunyoosheana vidole hapa. Nawaomba tuombolezeni kwa amani na tuendelee kutoa sala zetu bila kutoa lawama. Ajali ni ajali, na tulifundishwa kuwa ajali haina kinga. Mheshimiwa Mudhihir alipata ajali wakati akiwa anendesha gari zuri sana. Marehemu Sokoine alipata ajali huku akiwa anaendeshwa na dereva professional tena akiwa na walinzi. Tujifunze kukubali matokeo ya kazi ya Mungu, ingawe wakati mwingine matokeo yake huwa magumu kwetu kumeza, lakini ndiyo ilivyo: Kazi ya Mungu haina makosa
Mudhihir alipata ajali baada ya kulumbana na Zitto Kabwe. na chacha Wangwe amelumbana na chadema sana hivi karibuni kama mawazo amesababishiwa na mambo kadhaa wa kadhaa.
 
mkuu unamuheshimu marehemu leo? ungefanya alipokuwa hai kuliko ulivyomdhalilisha kaisi hiki,mmemfuta umakamu lakini bado mkaendelea kumsakama humu na jeshi lako lote.

Mgagagigikoko, nadhani una matatizo yako unatafuta wa kumuambukiza, bahati mbaya hapa wote ni watu wazima, watoto mko wachache sana. Unayoandika na unayemwandikia (siju unamwaddress nani?) ni vitu viwili ambavyo vinaonyesha hicho ninachokisema. Pole, kama unataka kutumia msiba kuonyesha udhaifu wako. pole. Hapa si mahali pake, na sina dawa kwa ugonjwa wako. Utajadiliana na watoto wenzio...
 
Kaka Mtanzania,

Mashangingi ndo ovyo kabisa haswa kwa upande wa stability. Gari ndogo ni stable kama haijanyanyuliwa (wao wanasema kuweka bush). Vinginevyo inakuwa juu lakini at your own risk. Kitu hiki wanakifanya wengi bila kujua side effect yake.

Invisible,

Ni kweli, hawa jamaa wameongelea matatizo ya 4WD kwenye ajali:

Crashworthiness
Risk of fatality is related to change in velocity ("delta V"). For a two vehicle collision the delta-V is proportional to mass. Therefore, IN THEORY, a vehicle that has twice the mass of the other vehicle should experience half the delta-V. However, IN PRACTICE many other factors come into play. Crash tests and studies of real world crashes suggest that, on average, four-wheel-drives are not as safe as large passenger cars even though they are typically much heavier than cars. Some possible reasons:


-They tend to be much stiffer than a car and this can cause higher crash forces on the occupants even though the delta-V of the vehicle is probably lower the delta-V experienced by the 4WD occupant is higher (the ultimate example of this effect is the army tank it is said that a head-on collision between two tanks at 20km/h is likely to be fatal for the occupants).
-Many crashes involve collisions with roadside objects or vehicles or similar or heavier mass so the mass-ratio advantages do not apply.
-4WDs tend to roll more easily than cars and a rollover crash is more likely to be life-threatening
- Design of life-saving occupant restraint systems is typically less advanced with 4WDs

Hasa hizo points mbili za mwisho ni tatizo kwenye 4WD.
 
Inna Lillah Wainna Ilaih Rajiuun!

Uffffffuh!..sina nguvu wala la kusema zaidi ya kumwombea Pepo!..
Tunashukuru pole yako inatoka moyoni, ulimuenzi akiwa hai wale wanafiki wamekuja mbio kuleta pole za kinafiki.
Mkandara ulitetea na kuamini ya Marehemu Wangwe tunakushukuru kwa hilo. pole yako tunaipokea ni ya dhati si ya kinafiki.
 
Polen kwa familia,jamaa zake wa karibu pamoja na Taifa kwa ujumla.

Uchunguzi wa kifo cha CW ni muhimu ili kuondoa utata unaoweza kujitokeza,lengo lisiwe kutafta mchawi,bali kujua chanzo na kupata ushauri wa kuzuia vifo vya aina hiyo utasaidia.

Wapinzani ntawashangaa wakikaa kimya maana wamekuwa wakitaka uchunguzi ufanyike kwa mambo mengine ya wazi
 
RIP Chacha Wangwe, tunakuombea ufike kwa mola wako na akupe pumziko la milele. Poleni wafiwa wooooote waliofikwa na msiba huu mungu awape nguvu muweze kuupokea na kumtumainia yeye atoae uzima na kuuchukua pindi atakapo, Jina lake lihimidiwe, Apumzike kwa amani, Amina

Hata hivyo, Sasa Chadema ikae mkao wa tahadhari. Nina imani kubwa sana wapinzani wa Chadema na chama cha mazimwi kitatumia kifo hichi kukibomoa CHADEMA kwa kueneza propaganda mbali mbali. Na propoganda hizi zitaongozwa na mafisadi either kubadili attention ya watu, wabunge na media kuhusu ufisadi ama kukibomoa CHADEMA ili kuhakikisha hakiendelei kuwafichua mafisadi.

Tusubiri, kuanzia kesho na media moja itaanza chokochoko kesho
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom