"...Katika uhai wake marehemu alikutana na mengi, alikutana na wengi, na kwa namna moja au nyingine hisia zake ziligusa ama kuwakwaza wengi. Kwa niaba ya ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu tunaomba msamaha kwa yote aliyewakosea, kwani kabla hujafa hujaumbika.
Ingelikuwa mwenyezi Mungu anatoa siri ya kifo na kujua lini utakufa, naamini marehemu na hata waliomkosea wangechukua nafasi kuombana msamaha, kwani maisha ya dunia ni mapitio tu.
Kama kuna anayemdai marehemu, ama kuna anayedaiwa na marehemu, mlango uko wazi, aonane na mwenyekiti wa kamati kuyajadili hayo. Tunamwomba mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi ndugu yetu huyu!"
Achana na imani hizi potofu maana mwisho utafikia kutafuta kiungo cha Albino.Tragedy! kumbe huko Chadema nako kuna Ku-Kolimbana. Pole mjane na ndugu wote
Nimepokea habari hizi za msiba kwa masikitiko Makubwa sana,Naungana na Familia ya Chacha Wangwe katika Msiba huu Mzito,Tumepoteza Mtetezi wa Ruzuku za wananchi,Mtu aliyepinga Ukabila na sijui nani atachukua Nafsai yake.
Mungu ametoa na Mungu ametwaa na tutakukumbuka Kipindi kirefu sana MArehemu Wangwe
Amefariki muda si mrefu kwa ajali ya gari akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam eneo la Pandambili (kama sijakosea).
Zaidi nitawafahamisha
Watu wasijehusisha hiyo accident na mgogoro wa kiuongozi aliokuwa nao ndani ya CHADEMA.
Mungu aiweke roho ya marehemu pema peponi. Sote ndiyo njia yetu hiyo.
Watu washaanza kuulizana could it be CHADEMA's mission?? or is it CCM's as usual????
Na raia wa kawaida ndio watumie yasiyo salama?
Kasheshe unachemka!
Mmefuatilia lakini mahojiano ya TV na mtoto wa Wangwe yaliyokatwa ghafla hivi punde?
Tuhabarishe Comanero kasemaje?