Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Meseji za Mallya kwa Kabwe zanaswa, Ajitambulisha ni mtaalam wa kompyuta, Aomba tenda ya kuchapisha nyaraka, Siri ya kukutana na Wangwe yabainika


*Ajitambulisha ni mtaalam wa kompyuta
*Aomba tenda ya kuchapisha nyaraka
*Siri ya kukutana na Wangwe yabainika

Na Hassan Abbas

MBINU ya Bw. Deus Mallya, kijana aliyenusurika katika ajali iliyomuua mbunge wa Tarime, Bw. Chacha Wangwe, ambaye sasa anahusishwa na ujasusi, kuwaingia wanasiawa mashuhuri nchini na kujenga urafiki nao, imebainika.

Mbinu hiyo imefahamika kufuatia uchunguzi wa gazeti hili kuzinasa meseji zake kadhaa alizowahi kumtumia Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Bw. Zitto Kabwe, ikiwa ni kabla ya kufahamiana na marehemu Wangwe.

Imebainika Mallya akijitambulisha kuwa ni mtaalamu wa mifumo mbalimbali ya programu za kompyuta katika uchapishaji wa nyaraka na vitu mbalimbali kabla ya kufahamiana na marehemu Wangwe, alijipenyeza kupitia kwa Bw. Kabwe akijinasibu kuwa angeweza kuifanya biashara hiyo vyema.

Kwa meseji zake kwenda kwa Kabwe, ambazo Majira Jumapili linazo, Mallya, alianza 'kumuingia' mbunge huyo kijana na kufanikiwa kufanya naye kazi kadhaa za uchapishaji.

Chanzo chetu kinaonesha kuwa, Deus, ambaye baba yake mzazi alikaririwa hivi karibuni akidai kuwa mwanae huyo hana elimu zaidi ya darasa la saba, katika mawasiliano yake na Bw. Kabwe,alisisitiza pia kuwa yeye ni kijana wa chama kutoka mjini Moshi.Alianza kutuma meseji hizo Oktoba, 2006.

'Kijana wa CHADEMA'

Mallya alianza kwa kujitambulisha kwa Bw. Kabwe kuwa yeye ni kijana wa CHADEMA.

"Mhh. Hata hivyo Brother, mimi ni mmoja kati ya vijana wa CHADEMA," aliandika Mallya akimtumia Zitto Kabwe kupitia blogu rasmi ya mbunge huyo machachari.

'Chakula meza moja'

"...tulikuwa wote kwenye dinner party (hafla ya chakula cha usiku) ya vijana wafanyakazi iliyofanyika Istana Restaurant (mimi Mallya) ni kiongozi wa vijanaMoshi."

Mallya katika ujumbe wake huo ndipo akaanza kumuingia Bw. Kabwe kibiashara.

"Sasa ni mfanyakazi ktk (katika) kampuni ya THE CORPORATE IMAGE kama marketing (masoko) na Graphic Designer (mbunifu wa michoro katika kompyuta)."

Mallya akaendelea: "Kama una kazi yoyote ya printing (kuchapisha) like (kama) tshirts, kaps, wheelcovers, banners, coffee mugs, flayers,etc,."

Mallya aomba kazi

" Nakuomba uwasiliane nami muda wowote nitakufanyia kazi yako vizuri kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu sana. Pia tuna embroidery machine (mashine ya kudarizi) yenye high quality (ubora wa hali ya juu).

"Pamoja na kuwa siyo sehemu yake kuacha message ka (kama) hii, niwie radhi ndugu yangu mpendwa. Email yangu ni deusmallya@yahoo.com," alimaliza Mallya.

Katika blogu hiyo, Kabwe hakuonekana kumjibu chochote Mallya mbali ya kuwajibu watu wengine waliomtumia ujumbe katika mada mbalimbali alizokuwa akizijadili.

Alipoulizwa na gazeti hili kwa njia ya simu jana kuhusu 'sms' hizo na kama aliwahi kufanyabiashara na Bw. Mallya kama alivyoombwa kupitia blogu yake hiyo inayopatikana katika anuani ya www.chadema.net/blogu/zitto/, Bw. Kabwe alisema:

"Nina muda mrefu sasa sijaangalia blogu yangu, lakini hata hivyo siwezi kukana kwamba nnamfahamu Mallya. Ni kijana ambaye tumekuwa tukifanya naye kazi katika chama za printing (uchapishaji).

"Sifahamiani naye sana, niliwahi kuonana naye ana kwa ana Mei mwaka huu tu mjini Dodoma na juzi alipokuja bungeni (kabla ya tukio la ajali), alitaka kuonana nami lakini nikamuelekeza aende kwa msaidizi wangu."

Alipoulizwa kama alishawahi kufanyabishara na Mallya kama alivyokuwa ameomba kwenye 'sms' hizo za mwaka 2006, Kabwe alijibu:

"Ndiyo, Mallya tulifanya naye kazi za printing, kwa mfano nilimpa kazi ya kuchapisha kitabu chenye maswali yote niliyopata kuyauliza bungeni na majibu yake, kazi ambayo alishaikamilisha na tumeshakitoa kitabu hicho.

"Pia kuna kazi nyingine tulikuwa tukitaka kumpa ya kuchapisha maswali na majibu ya waheshimiwa wabunge kadhaa wa CHADEMA lakini hata hivyo katika matukio yote hayo sikuwa nikikutana naye, alikuwa akijishuhghulisha na msaidizi wangu anaitwa David Kafalalil, labda umtafute yeye atakueleza zaidi walikutana vipi." Bw. Kafalila hakupatikana alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi.

Ujasusi na kukutana na Wangwe

Akimzungumzia Mallya na tetesi za kuwa ni jasusi, Bw. Kabwe alisema hakumfahamu sana lakini anafahamu ndani ya CHADEMA alikuwa akifanya shughuli kadhaa za uchapishaji na hata mara ya mwisho kuna kazi alikuwa akitaka kumchapishia marehemu Chacha Wangwe na ndio maana wakawa wote.

"Huwa sipendi kutoa conclusion (hitimisho) kuhusu namna ninavyomuona mtu. Mallya sikumfahamu sana kama nilivyosema hivyo kuhusika kwake na masuala hayo (ujasusi) siwezi kujua, nampa benefit of doubt (hamtilii shaka sana)."

Kuibuka kwa hisia za Mallya kuwa ni jasusi kunaweza kumfanya kuonekana kuwa alianza siku nyingi kujipenyeza kwa viongozi wa CHADEMA, hata hivyo Jeshi la Polisi nchini, lilisema wiki hii kuwa ushahidi uliowasilishwa kwao na viongozi kadhaa wa upinzani ukimhusisha kijana huyo na ujasusi, haujitoshelezi.

Bw. Mallya kwa sasa ameshtakiwa kwa makosa ya kuendesha gari kizembe na kusababisha kifo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Dodoma.

source. Majira. 10.august'08
 
Chadema: Kifo cha Chacha Wangwe hakijaathiri chama
Na Boniface Meena

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) kimesema kifo cha aliyekuwa mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe hakijaathiri chama hicho kiutendaji.


Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu jana Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe alisema msiba ni kitu cha kawaida na makao makuu ya chama hicho shughuli zinaendelea kama kawaida.


"Msiba ni kitu cha kawaida na makao makuu ya chama chetu shughuli zinaendelea kama kawaida", alisema Kabwe.


Akizungumzia kuhusu majibu ya barua waliyoiandikia ubalozi wa Libya hapa nchini kuhusu taarifa za Deus Mallya ambaye alikuwa na Wangwe katika gari moja kabla ya kupata ajali, Kabwe alisema hadi hivi sasa bado majibu ya barua hiyo hayajapatikana.


"Majibu ya barua yetu bado hatujapata vile vile majibu ya maswali saba tuliyoyapeleka polisi hatujapata majibu yake", alisema Kabwe.


Awali Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alipoulizwa juu ya majibu hayo kutoa Polisi na ubalozi wa Libya alisema taarifa hizo atakuwa nazo John Mnyika ambaye ni Mkurugenzi wa Vijana Chadema.


Mnyika alipopigiwa simu alijibu kuwa bado hawajapata majibu ya barua zao kwa polisi wala ubalozi wa Libya kama ilivyoelezwa na Kabwe.


Kuhusu chama kuathiriwa na kifo cha Wangwe, Mnyika alisema hawezi kuzungumzia suala hilo ili kuepuka kuleta mjadala zaidi juu ya kifo cha Wangwe.


"Siwezi kuzungumzia suala hilo ili kuepusha mjadala kuhusu kifo cha Wangwe,"alisema Mnyika.

Source: Mwananchi 10/08/08
 
Nakumbuka,

Kipindi kile mama Medji walivyopandisha kodi ya mafuta na mafuta yakapanda bei (of course pamoja na tatizo la kitamataifa la mafuta) na inflation ikapanda... akaulizwa je uchumi umeathirika...

Akakanusha sana kwamba haujaadhirika hata kidogo.... baadaye yakaonekana hayo hata kwa vipofu...

Na hili la CHADEMA muda si muda utaona adhari za kutokuwepo Chacha Wangwe kwenye utawala wao.
 
Hivi kwanini wametupia hili zigo zitto?

hivi ni kwanini Mbowe hajawahi kuzungumza kuhusu hili...aeleze sababu ya yeye kufukuzwa na mapanga huko kemakorere?


Mnyika na Zitto wameachiwa msalaba?
 
Wako serious hawa kweli? Chama gani ambacho kinaweza kufiwa na Makamu Mwenyekiti wake, ambaye pia ni Mbunge na Mwenyekiti wa chama mkoa halafu kiseme hakijaathirika kiutendaji?
 
Chadema: Kifo cha Chacha Wangwe hakijaathiri chama
Na Boniface Meena

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) kimesema kifo cha aliyekuwa mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe hakijaathiri chama hicho kiutendaji.


Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu jana Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe alisema msiba ni kitu cha kawaida na makao makuu ya chama hicho shughuli zinaendelea kama kawaida.


"Msiba ni kitu cha kawaida na makao makuu ya chama chetu shughuli zinaendelea kama kawaida", alisema Kabwe.


Akizungumzia kuhusu majibu ya barua waliyoiandikia ubalozi wa Libya hapa nchini kuhusu taarifa za Deus Mallya ambaye alikuwa na Wangwe katika gari moja kabla ya kupata ajali, Kabwe alisema hadi hivi sasa bado majibu ya barua hiyo hayajapatikana.


"Majibu ya barua yetu bado hatujapata vile vile majibu ya maswali saba tuliyoyapeleka polisi hatujapata majibu yake", alisema Kabwe.


Awali Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alipoulizwa juu ya majibu hayo kutoa Polisi na ubalozi wa Libya alisema taarifa hizo atakuwa nazo John Mnyika ambaye ni Mkurugenzi wa Vijana Chadema.


Mnyika alipopigiwa simu alijibu kuwa bado hawajapata majibu ya barua zao kwa polisi wala ubalozi wa Libya kama ilivyoelezwa na Kabwe.


Kuhusu chama kuathiriwa na kifo cha Wangwe, Mnyika alisema hawezi kuzungumzia suala hilo ili kuepuka kuleta mjadala zaidi juu ya kifo cha Wangwe.


"Siwezi kuzungumzia suala hilo ili kuepusha mjadala kuhusu kifo cha Wangwe,"alisema Mnyika.

Source: Mwananchi 10/08/08

Hapo mmoja anasema Chama hakijaathirika na hapo hapo mwingine anakuja kusema kuwa hawezi kuzungumzia hiyo ishu ili kuepusha mjadala. Hapo kwa mtazamo wangu kwa majibu hayo mawili tofauti ndiyo wanatupa nafasi ya kuibua mijadala mingi zaidi.

Kwa mfano kauli ya Zitto kuwa chama hakijaathirika alikusudia kutupa picha gani ilhali kwa utamaduni wetu tunaamini kuwa pengo la marehemu halitazibika? Ndiyo tuseme kuwa pengo lake lilikuwa limeshazibwa hata kabla hajafa?

Pia kitendo cha Mnyika kuonesha msimamo tofauti na wa Kabwe, ina maana kuwa hawakujadiliana kwanza jinsi ya kukabiliana na maswali yeyote watakayoulizwa juu ya msiba huo?

Kwa ninavyoamini ni kuwa ili kuonesha ukomavu basi viongozi wakuu wa vyama vyetu nchini wawe na utaratibu wa kuwasiliana mara kwa mara kuhusu suala lolote linalojitokeza ili kuepusha mgongano wa mawazo kama walivyothibitisha hilo ndugu zetu hapo juu.
 
Haya ndiyo mapungufu ya kutisha ya wanasiasa wetu wa TZ, huwa wanashindwa kukubali ukweli hata kama upo wazi kiasi gani. Hivi huyu mhe aliona kuna ugumu gani kukubali kwamba kifo cha Wangwe kimewatikisa? Hata kama wangekuwa hawana mgogoro na Wangwe, bado kufiwa na mbunge, tena kwa chama ambacho wabunge wenyewe hawafiki kumi, kungekuwa na athari kubwa kwa chama chochote kile. It is too bad kwamba vijana ambao tunawategemea katika kubadilisha siasa zetu wanakuwa na gaffle kama za akina Kingunge.

These are the things that make some of us hate politics; but then should we hate politics or politicians?

kazi kwelikweli!
 
Kauli hizi zinasikitisha sana.

Haya tusubiri warudi kwenye vyombo vya habari tena kwenda kukanusha
 
Hivi kwanini wametupia hili zigo zitto?

hivi ni kwanini Mbowe hajawahi kuzungumza kuhusu hili...aeleze sababu ya yeye kufukuzwa na mapanga huko kemakorere?


Mnyika na Zitto wameachiwa msalaba?

Gembe,

Masters yako ilikuwa ya maisha ya Mbowe au unataka kumchukuria Phd. Mpe nafasi kijana mwenzio na acha majungu na wivu mbaya kiasi hicho. Hongera kwa kuwa na masters!
 
"Maandalizi" yalishafanywa kabla hajafariki akawekwa kando.
Upembuzi wa kale ka-Nzi mara nyingi huwa una ukweli ndani yake,kanajua 75%ya kinachoendelea ndani ya Chama.Mie nakasubiri tu,katatua na habari za UHAKIKA sasa hivi.
 
Hapo mmoja anasema Chama hakijaathirika na hapo hapo mwingine anakuja kusema kuwa hawezi kuzungumzia hiyo ishu ili kuepusha mjadala. Hapo kwa mtazamo wangu kwa majibu hayo mawili tofauti ndiyo wanatupa nafasi ya kuibua mijadala mingi zaidi.

Kwa mfano kauli ya Zitto kuwa chama hakijaathirika alikusudia kutupa picha gani ilhali kwa utamaduni wetu tunaamini kuwa pengo la marehemu halitazibika? Ndiyo tuseme kuwa pengo lake lilikuwa limeshazibwa hata kabla hajafa?

Pia kitendo cha Mnyika kuonesha msimamo tofauti na wa Kabwe, ina maana kuwa hawakujadiliana kwanza jinsi ya kukabiliana na maswali yeyote watakayoulizwa juu ya msiba huo?

Kwa ninavyoamini ni kuwa ili kuonesha ukomavu basi viongozi wakuu wa vyama vyetu nchini wawe na utaratibu wa kuwasiliana mara kwa mara kuhusu suala lolote linalojitokeza ili kuepusha mgongano wa mawazo kama walivyothibitisha hilo ndugu zetu hapo juu.

Hebu nionyeshe mahali ambapo wametofautiana kimsimamo. Kauli zao zipi zimetofautiana?

....ndiyohiyo
 
Gembe,

Masters yako ilikuwa ya maisha ya Mbowe au unataka kumchukuria Phd. Mpe nafasi kijana mwenzio na acha majungu na wivu mbaya kiasi hicho. Hongera kwa kuwa na masters!
Hapo kuna wivu gani au majungu gani...ushabiki mwingine ni noma
 
Sasa ukiona watu hawana kazi ya kufanya ni kama hao wanoishi kufuata ya kijijini kwa wangwe kila saa.huku ni kufilisika kimawazo
 
Mamia kushuhudia ushahidi kifo cha Wangwe leo

Wangwe wakamilika 11.09.2008 [Soma]

Na Mwandishi Wetu

SIKU chache tu baada ya familia ya aliyekuwa mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe kufanya shughuli ya kifamilia kuwashukuru wote waliojitokeza kuwafariji katika kipindi cha msiba huo, kitendawili cha nini hasa kilimuua mwanasiasa huyo kitateguliwa leo.

Kitendawili hicho kitateguliwa na Mwenyekiti wa asasi ya ukombozi ya Liberty Desk, Mchungaji Christopher Mtikila atakapozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuweka hadharani kile alichokiita 'ushahidi mzito.'

Akizungumzia hilo Dar es Salaam jana, Bw. Mtikila amesema ana ushahidi mzito kuwa Wangwe hakufa kwa ajali, bali aliuawa. Mkutano huo pia utahudhuriwa na ndugu na jamaa wa marehemu na unakadiriwa kuhudhuriwa na watu takribani 300.

Wangwe alikufa kwa ajali tata ya gari iliyotokea eneo la Pandambili mkoani Dodoma wakati akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam.

"Nimekusanya ushahidi na kesho (leo) nauweka hadharani, nitapasua jibu na kueleza jinsi alivyouawa," alisema Mchungaji.

Tangu kifo hicho kitokee zimekuwepo taarifa kuwa Bw. Wangwe aliuawa, madai ambayo hata hivyo madaktari wawili tofauti walioufanyia mwili wake uchunguzi saa chache kabla ya kuzikwa walishindwa kuyathibitisha.

Pamoja na Wangwe kuzikwa, watu wngi wakiwemo baadhi ya ndugu zake wa karibu, wamekuwa wakizungumza chini kwa chini juu ya kuendelea kubaki na hofu hasa kutokana na mazingira tata ya ajali yenyewe.

Alipobanwa zaidi ili aeleze kile anachotarajia kukisema na vyanzo vya ushahidi wake huo, Mchungaji Mtikila alisema akifanya hivyo atakuwa anamaliza uhondo, lakini alisisitiza kuwa anao ushahidi wa kuthibitisha kuwa Wangwe aliuawa.

Taarifa za madai ya kuuawa marehemu Wangwe zilisababisha kulipuka kwa vurugu kubwa wakati wa mazishi yake hadi yakaahirishwa ili kutoa nafasi ya uchunguzi wa pili uliofanywa na daktari kutoka nchini Kenya ambao nao haukusaidia kukidhi kiu ya wengi.

Kijana Deus Mallya aliyekuwa kwenye gari hilo na Wangwe kabla ya ajali naye ameibua utata zaidi baada ya kuibuka hisia kuwa aliwahi kupata mafunzo ya ujasusi. Mallya kwa sasa anakabiliwa na kesi kutokana na ajali hiyo na yuko rumande.

Iwapo ushahidi wa Mtikila atakaouanika leo utakuwa na nguvu, unaweza kufungua upya mjadala wa kisiasa juu ya kifo cha Mbunge huyo, mjadala ambao ulishaanza kupoa.

Katika hatua nyingine, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alichokuwa akikitumika Bw. Wangwe kimesema kitachukua hatua za kulitaka Jeshi la Polisi nchini kuunda Tume ya Uchunguzi Maalum wa Vifo tata (Inquest) ili jamii iweze kupata majibu kamili kuhusu utata wa kifo hicho.

Sheria ya Uchunguzi wa Vifo (The Inquest Act,1980), inaruhusu kufanyika uchunguzi dhidi ya kifo tata hata kama marehemu alishazikwa ambapo Jeshi la Polisi hufungua mashitaka ya uchunguzi huo kwenye Mahakama Maalum iliyoundwa kwa kazi hiyo (Coroners Court) au kupitia Mahakama ya Hakimu Mkazi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa, alisema sekratarieti ya Kamati Kuu ya chama hicho italiuliza Jeshi la Polisi nchini kama uchunguzi wanaoufanya sasa unahusisha utata wa kifo hicho ili kama si hivyo waombe rasmi kuundwa Tume ya Kuchunguza Vifo.

Alisema uamuzi huo wameuchukua kufuatia baadhi ya vyama vya siasa kutumia kifo hicho kujijenga kisiasa na kueleza kusikitishwa kwa Kamati Kuu ya CHADEMA na kitendo cha kumhusisha Mwenyekiti wa chama hicho, Bw. Freeman Mbowe na utata wa kifo cha marehemu Wangwe.

"Ni vizuri vyama vya siasa vikatumia ajenda kujijenga na sio kutumia misiba jambo ambalo ni kinyume na utamaduni wetu," alisema Dkt. Slaa.

Alisema chama hicho kinao ushahidi ya mkanda unaoonesha kiongozi mmoja wa chama (hakumtaja jina) akiwaeleza waandishi wa habari kuwa Bw. Mbowe aliandaa tafrija akiwa nchini Afrika ya Kusini kusherekea kifo cha marehemu Wangwe.

Dkt. Slaa alisema tabia hiyo ni mfano mbaya unaoweza kusababisha machafuko nchini na kubainisha kuwa baada ya kupokea taarifa ya jopo la wanasheria wao, watachukua hatua kali za kisheria muda wowote kuanzia sasa dhidi ya wote waliohusika kukichafua chama hicho.

Alifafanua kuwa pamoja na hayo Kamati Kuu bado ina imani na Bw. Mbowe na kumpongeza kwa jinsi alivyoweza kutulia na kuonesha busara ya hali ya juu wakati wote ambapo chama hicho kilikuwa kikikabiliana na kile alichokiita "mbinu chafu za mafisadi."

"Kamati Kuu ipo tayari kumpa ushirikiano wowote kukabiliana na hujuma yoyote dhidi ya CHADEMA kwa imani kuwa chama chetu chini ya Bw. Mbowe kinayo fursa ya kujizatiti kushinda," alisema.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi na CHADEMA, Bw. Mbowe anatarajiwa kuzungumza kwa mara ya kwanza hadharani kesho mjini Mwanza wakati chama hicho kitakapofanya mkutano wa hadharani kuwapatia wananchi tathimini ya mwaka mmoja tangu orodha ya mafisadi ilipowekwa hadharani na kutangaza mkakati mpya wa kupambana na mafisadi nchini.

Septemba 15 mwaka jana kwenye viwanja vya Mwembe Yanga, Dar es Salaam, CHADEMA kupitia Dkt. Slaa na Mkurugenzi wa Sheria na Katiba wa chama hicho, wakili Tundu Lissu kilitangaza orodha ya watu waliodaiwa kuwa mafisadi, orodha ambayo ilisheheni majina ya wanasiasa na viongozi wakuu kitaifa nchini.
 
Tusubiri, lakini Mtikila huwa akiamua kufanya kweli huwa nafanya kweli. MTIKILA anawazidi wanasiasa wetu wengi wa somi kwa uwezo wake wa kureserch na Kutumia DATA kujenga hoja. Tusubiri leo kama ataweza kumaintain hiyo record yake.
 
Wanajf muwe macho na huyo mtu,isiwe bunduki ameelekeza kwingine.Huyu jamaa anakabiliwa na kesi dhidi ya wanasiasa wa chama tawala,isije kuwa ni pact fulani.Juzijuzi alishinda kesi ya uchochezi aliyodaiwa kumkashifu Rais wa awamu ya tatu.Na ikumbukwe aliahidi kujibu mapigo dhidi ya Rostam Aziz alipofichua msaada wa milioni tatu.
 
Mbogela,
Huo uwezo wake wa ku-research ulitibuka alipokiri kupokea vijisenti toka kwa Rostam. Anaweza akaaminiwa leo hii?
 
Tatizo ni kijana Mlya ambae ndie shahidi anaeweza kutoa ukweli ,huyu kijana akipata mdhamini wa kweli anaweza kutoboa siri iliyojificha ,sielewi kwa nini hadi hii leo CHADEMA hawajamdhamini na kumuweka kiti moto katika anga zao au CHADEMA ni washiriki wa kifo ,kwani wao walikuwa wa mwanzo kukanusha kama risasi zilitumika baada ya daktari wa serikali kufanya uchunguzi wakati wenyeji wa maiti walikwisha sema tundu za risasi zilikuwepo na ndani ya gari hakuna kitu chenye ncha kali ambacho kingeweza kufumua kichwa ?
 
Mtikila anasema Mbowe, Dr. Slaa na Tundu Lisu ndio wauaji wa Wangwe .......na hili tumuamini au? Lakini nadhani watu tulitegemea atupe ushahidi wake na sio kutamka tu kwa maneno.

MTIKILA ARIPUKA TENA!

Mwenyekiti wa chama cha Democratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila, akiongea na Waandishi wa Habari
katika Hoteli ya Travertine iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam mapema leo. Katika mkutano huo amewataja Mbowe,
Dk Slaa na Lisu kuwa ndiyo waliohusika Na mauaji ya aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Marehemu Chacha Zakayo Wangwe,
kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa chama chake, Bwana Matwanga

Baadhi ya ndugu na jamaa wa Marehemu Chacha Zakayo Wangwe wakimsikiliza Mchungaji Christopher Mtikila
wakati akiripuka na tuhuma hizo nzito.

PICHA: MAKONGORO OGING/GPL
Bofya hapa
Global Publishers - Picha
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom