PPM
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 838
- 230
Marehemu huenziwa.Husifiwa na kukumbukwa kwa mema yake. Isiwe haramu kusema na alipoteleza pia.Aliposema au kufanya tofauti ya matarajio ya wengi au wote. Maneno ya tahadhari au ya mafunzo wakati wa msiba si kwa ajili ya marehemu.Yeye hausiki tena.Kusema na kutenda.
Alichoposti mtandaoni J.J.Mnyika ni kukumbusha tu kauli ya Hayati Kapteni John Damian Komba aliyoitoa katika Bunge la Katiba. Kauli ya kumsimanga na kumtabiria kifo Waziri Mkuu Mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,Jaji Joseph Sinde Warioba. Hayati Komba alimwita Warioba 'mzee anayekaribia kufa'. Haikuwa kauli rafiki.Ilikera na kukwaza kwelikweli.
Kukumbusha kauli hiyo wakati wa msiba wa mtoa-kauli si matusi wala kejeli.Ni mafunzo kwa sisi tuliobakia.Tunaaswa kusema na kutenda kwa mipaka hata pale tunapoghadhibika.Tujitahidi sana kuzuia kughafilika. Kifo ni fumbo. Kujua haiwezekani. Tunaaswa kuwa makini na kauli na matendo yetu hasa kuhusu masuala ya kifo.
Tukimtetea Hayati Komba kwa kauli yake,Mzee Warioba atajisikiaje? Misiba itufunze zaidi ya kuhuzunika na kuomboleza kwetu. R.I.P. Captain (Rtd.) John Damian Komba!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Tuondolee umasabiri hapa