Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,214
- 128,976
Manyerere Jacton, asante kwa taarifa.
Mwanajf mwenzetu. Abs K. Get well soon!.
P.
Mwanajf mwenzetu. Abs K. Get well soon!.
P.
Kauli za jk dhidi ya uhai hazina tija!
Na msitarajie wahusika kukamatwa.
huyu jamaa hapa namnukuu "Neville C. Meena,
Secretary General,
Tanzania Editors Forum - TEF,
Dar es Salaam - Tanzania." ni mnafiki sana.....kulikuwa na haja gani ya kuripoti upasuaji na kutuambia ya Jekey?.....ni heri wange kuumiza wewe Neville kwa kuwa ni mnafiki kuliko watu wote ninao wajua
kama wahusika ni serekali ya Tanzania chini ya fast jet usitegemee wasika kukamatwa rejea kifo cha RPC wa mwanza wahisika walikamatwa ndani ya week .
Mheshimiwa ana list ndefu ya kuhakikisha wahalifu wanakamatwa, waliompiga kubenea,ulimboka,shehe znz,padri znz,padri aliyeuwawa znz na sasa kibanda, kazi kweli.
hivi hajaenda kwenye mazishi na jua kwasasa ameshanunua suti ya kujiandaa kwenda kesha..kama ni raisi tunae yaani ningekuwa polisi ningemkamata uzururaji..........Kikwete nae mara yupo south..
Ya kubenea ilimkutia huko na hii ya kibanda hukohuko. Sijui ni coincidence au ndo kutotulia nyumbani?
Ya kubenea alikuwa na meseji za wahusika mbona hawajakamatwa mpka leo...wale simu ndo ilichangia kunaswa haraka,lakini hata hawa waliompiga sibanda kama makachero wako serious hawatachukua round.
Taarifa kutoka South Africa, kupitia Jukwaa la Wahariri Tanzania
1. Kibanda leo ameingizwa theater ili kuanza kufanyiwa upasuaji na kujengwa sura baada ya kupungua kwa majeraha na uvimbe vilivyokuwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake, hususan kichwani na usoni.
2. Upasuaji huo unazingatia matokeo ya uchunguzi ulifanywa kwa zaidi ya saa 48 na jopo la madaktari na kubaini kwamba mbali na madhara ya awali, Kibanda pia aliumizwa taya lake la kushoto.
3. Kuhusu jicho lake la kushoto ambalo pia lilijeruhiwa, madaktari walisema wangetoa uamuzi kuhusu aina ya upasuaji ambao wangeufanya baada ya kubaini hali halisi wakati watakapokuwa wakijenga sura yake ambayo iliharibiwa kwa majeraha.
4. Wakati akipelekwa theater ambako alikuwa akifanyia upasuaji ambao uliotarajiwa kuchukua saa zaidi ya nne, alikuwa akilalamikia maumivu kutokana na kidonda kilichopo kwenye mguu wake wa kushoto. Kidonda hicho pia ni matokeo ya unyama aliyofayiwa.
5. Jana Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana ambao wako Afrika Kusini kikazi, walimtembelea Kibanda hosipitalini kumjulia hali. Rais Kikwete alisema Serikali inajitahidi kuwasaka wahusika wa tukio la utesaji wa Kibanda na kwamba wakikamatwa watafikishwa mahakamani.
Tutaendelea kufahamishana kila hatua ya tiba ya Mwenyekiti wetu, na tunaomba tuendelee kumwombea ili apone haraka.
--
Neville C. Meena,
Secretary General,
Tanzania Editors Forum - TEF,
Dar es Salaam - Tanzania.
Cell: +255 - 787 - 675555
+255 - 753 - 555556
wale simu ndo ilichangia kunaswa haraka,lakini hata hawa waliompiga sibanda kama makachero wako serious hawatachukua round.