Kinachonishangaza katika hili ni kuwa sio suala sensitive sana kwa watawala. Pengine wanalijua ukweli wake. Mbona hatusikii wakiomba msaada wa majeshi Kutoka Nje kama FBI, CIA, Interpol N.k? Au pengine wanaouawa na kujeruhiwa sio maaskofu na mapadri? Damu ile sio ya Watanzania?? Kwa nini iwe cheap hivyo?.
Tujiulize tulipofika hapa,
Leo hii kupigwa au kuuawa Sheikh, Mhariri au mwandishi wa habari, raia wa kawaida inaonekana sio tatizo na mambo yanafunikwafunikwa mpaka upepo unapita. Lakini akiuawa Askofu au Padri basi Majeshi yote duniani yanaitwa. Tena katika mambo waliyodhulumiana wenyewe kwa wenyewe. Tujiulize, Tumefikaje hapa??
Serikali itupe majibu ya maswali haya kwa uwazi. Kuwe na mijadala ya wazi. Na tusiogope kusema ukweli!! Hivi nani yuko salama????. Tutaunda tume ngapi na halafu hizo tume zitasaidia kurusha jicho au mkono au roho iliyopotea??