Kiapo cha kunywa damu kwenye mahusiano

Kiapo cha kunywa damu kwenye mahusiano

Geronimo Mafionso

New Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
1
Reaction score
0
Wadau naomba kuuliza kuhusu hivi viapo vya damu,

Nilikutana na demu kwa muda wa wiki hivi ni kabinti kama miaka 18 ndio kwanza kanaingia form 5, siku hiyo tupo nae namsindikiza akaniomba ninunue kiwembe, sikujua cha kazi gani, baadae akaniambia anataka anichanje afu kila mtu anywe damu ya mwenzake kama kiapo nisimsaliti.

Mimi nikaona kama masihara mtoto nimemzidi miaka kama 9, anajuaje hayo mambo, tulipokaribia kwao tupo ndani ya gari tukasimama akachukua kiwembe akanikata begani akanywa damu akaniambia na mimi nimkate, nikamkata mkononi akaniambia nyonya damu, nikanyonya!

Ila kile kiwembe sikumpa asepe nacho nilikivunja nikakitupa na niliamini ni kitendo cha kawaida tu coz damu zetu hatukuzigusanisha wala kuapa kwa maneno.

Tulipomaliza akaniambia cheat uone sasa na akanipa mfano wa rafiki yake alikula kiapo kama hicho na boy wake, demu akamsaliti mshkaji saizi demu kichaaa. Lakini na mimi nafanya hayo yote nina demu wangu wa siku nyingi ingawa yupo mbali.

Huwezi amini baada ya kama wiki hivi yule demu wangu wa kweli kabisa akaanza kuzingua kapata mtu mwingine mpaka tumeachana kabisaaa, yule future wife hanitaki tena na hakuna sababu ya muhimu.

Asa sijajua mpaka sasa ni ile kuchanjana na kiwembe imefanya kazi au lah??

Na ni kweli viapo vya hivi vinafanya kazi? Mnaojua haya mambo nisaidieni....
 
HILO NI "AGANO" MMEWEKA, NA ZAMANI (WAZEE) WALITUMIA NJIA HIYO HIYO....BUT NOW I WONDER...Vp kama ananguvu za kishirikina? next time don't allow it...
 
Hakuna madhara yoyote mkuu, huo mkwara tu. Watu wamekula yamini Kanisani na bado wamesalitiana sembuse ninyi wazinifu mliokubuhu!!
Alafu unaanzaje kunywa damu damu za wengine, wewe na mzinifu mwenzako mna viashiria vya vampire.
 
Duu mwanangu umelikoroga . hapo lazima umuoe LA maisha yako yatakuwa hivyo kupindukia. Yaani mtoto umemzidi 9 yrs halafu anakuzingua mpk unakubali kunywa damu!!? Poor You AGANO LA DAMU ni baya kupitiliza. MUNGU tu ndio atakayekuokoa
 
Me naona miaka 30 itakuusu mda si marefu kuwa makini mkuu ucje ukaisoma namba maana izi ni zama mpya
 
Duuu? Utabak nae hivohivo gusa mwingine uone [emoji12]
 
Du! Umewezwa.
1470152212243.jpg
ishu zinazohusika na damu ni za kuepuka kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom