rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 15,204
- 20,185
Kesho Kuna mkutano mkuu wa timu ya Simba ,mojawapo ya ajenda ni mabadiliko ya katiba ili kukamilisha mchakato wa uwekezaji.
Tayari kamati iliyokusanya maoni kupitia mwenyekiti wake Husein Kitta umesema umemaliza kazi take na kukabidhiaoni tayari kwa ajili ya kupitishwa na mkutano mkuu lakini baadhi ya wanachama wametoa maoni tofauti, mwenyekiti wa tawi la wekundu terminal ameunga mkono maoni hayo wakati mweka hazina wa tawi la roho mbaya ameyapinga kwa kusema kamati imeleta maoni yanayompendelea zaidi mwekezaji hivyo hatakuwa tayari kuyapitisha.
Waliowahi kuwa viongozi wa Simba kwa nyakati tofauti wametoa maoni yao, Godfrey Nyange Kabutu amesema anaenda kuyapinga maoni hayo kwani yamemweka mwenyekiti wa Simba Kama mjumbe hivyo Hana mamlaka yoyote wakati ismai Aden Rage ameshauri swala la mabadiliko ya katiba lilitakiwa liandaliwe mkutano wake maalumu badala ya ya kuchanganua na mkutano mkuu.
Ukipitia harakaharaka hizi hoja utaona kuwa kamati ya mabadiko ya katiba iliteuliwa na Bodi hivyo lazima walinde maslahi ya mwekezaji kwani Rita walikataa kuipitisha katiba ya Simba baada ya kuona mwekezaji mwenye asilimia pungufu ana nguvu kuliko wanachama wenye asilimia nyingi.
Kitendo cha kuweka ajenda ya mabadiliko ya katiba kwenye mkutano mkuu ni kutaka wanachama wajikite kwenye katiba badala ya kuhoji kipigo kikubwa kwa siku za karibuni toka kwa mtani wao wa Hadi, dirisha la usajili limeshafungwa hivyo hawawezi kuwaleta kina manzoki kuwadanganya wanachama njia pekee ni kuleta mada itakayoleta ubishi na mkutano kuvunjika.
Simba ndio walianzisha mfumo wa mageuzi, wenzao yanga wakiangalia mapungufu yao na kuja na mfumo Bora zaidi hivyo Simba hawajachelewa bado wanayo nafasi ya kuboresha mfumo wao kwani wao ndio waasisi.
CEO anatoa taarifa, mtunza fedha anatoa taarifa.
Ni mapumziko baada ya mapumzikow Mwenyekiti wa kamati ya maboresho ya katiba ndio anatoa taarifa.
Tayari kamati iliyokusanya maoni kupitia mwenyekiti wake Husein Kitta umesema umemaliza kazi take na kukabidhiaoni tayari kwa ajili ya kupitishwa na mkutano mkuu lakini baadhi ya wanachama wametoa maoni tofauti, mwenyekiti wa tawi la wekundu terminal ameunga mkono maoni hayo wakati mweka hazina wa tawi la roho mbaya ameyapinga kwa kusema kamati imeleta maoni yanayompendelea zaidi mwekezaji hivyo hatakuwa tayari kuyapitisha.
Waliowahi kuwa viongozi wa Simba kwa nyakati tofauti wametoa maoni yao, Godfrey Nyange Kabutu amesema anaenda kuyapinga maoni hayo kwani yamemweka mwenyekiti wa Simba Kama mjumbe hivyo Hana mamlaka yoyote wakati ismai Aden Rage ameshauri swala la mabadiliko ya katiba lilitakiwa liandaliwe mkutano wake maalumu badala ya ya kuchanganua na mkutano mkuu.
Ukipitia harakaharaka hizi hoja utaona kuwa kamati ya mabadiko ya katiba iliteuliwa na Bodi hivyo lazima walinde maslahi ya mwekezaji kwani Rita walikataa kuipitisha katiba ya Simba baada ya kuona mwekezaji mwenye asilimia pungufu ana nguvu kuliko wanachama wenye asilimia nyingi.
Kitendo cha kuweka ajenda ya mabadiliko ya katiba kwenye mkutano mkuu ni kutaka wanachama wajikite kwenye katiba badala ya kuhoji kipigo kikubwa kwa siku za karibuni toka kwa mtani wao wa Hadi, dirisha la usajili limeshafungwa hivyo hawawezi kuwaleta kina manzoki kuwadanganya wanachama njia pekee ni kuleta mada itakayoleta ubishi na mkutano kuvunjika.
Simba ndio walianzisha mfumo wa mageuzi, wenzao yanga wakiangalia mapungufu yao na kuja na mfumo Bora zaidi hivyo Simba hawajachelewa bado wanayo nafasi ya kuboresha mfumo wao kwani wao ndio waasisi.
CEO anatoa taarifa, mtunza fedha anatoa taarifa.
Ni mapumziko baada ya mapumzikow Mwenyekiti wa kamati ya maboresho ya katiba ndio anatoa taarifa.