Maanadamano yasiyoifanya Katiba Mpya kuwa ni ajenda kuu ni maandamano ya wasaka vyeo

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,504
51,099
Katika nchi yetu tatizo la msingi siyo sheria za uchaguzi, Tatizo la msingi ni katiba mbovu inayozaa mfumo mbovu wa uongozi na utawala, mfumo mbovu wa haki na mfumo mbovu wa uwajibikaji.

Nashangaa chama kikuu cha upinzani ambacho kinajua wazi kuwa mzizi wa fitina ni katiba mbovu, hakina interest ya kuifanya katiba mpya kuwa ndiyo KILIO KIKUU cha kuwaingiza watu barabarani, lakini chenyewe kinaweka mbele mambo ya uchaguzi as if uchaguzi ndiyo tatizo kuu.

Hii inatoa taswira gani?, inatoa Taswira kuwa viongozi wa CHADEMA wao kinachowakera zaidi hadi kupata ujasiri wa kutaka kuwaingiza watu mabarabarani ni sheria zinazowakwaza kuingia bungeni au kupata udiwani. Otherwise kama kweli wana uchungu na wananchi kwa ujumla wake kwa nini Maandamano wanayoitisha yasiwe na AJENDA KUU YA MSINGI AMBAYO NI KUDAI KATIBA MPYA?

Uchaguzi wa mwaka 2020 ulipofanyika, Magufuli akawapiga akina Mbowe na kitu kizito kichwani waliwaambia wananchi kuwa kamwe hawawezi kushiriki tena uchaguzi chini ya katiba ya sasa na tume hii ya uchaguzi. Sasa Magufuli hayupo, wanahisi wana chance ya kuingia mjengoni tena kwa hiyo wako tayari kusettle na "minimum" reforms za kuwawezesha kuingia tena mjengoni kula kodi za wananchi!.

Mimi nasema kama CHADEMA wanataka kuandamana kama chama ili watngenezewe sheria watakazozipenda za kuwawezesha kupata hivyo viti vya ubunge na ruzuku iongezeke, basi ni kheri kwao wacha waandamane, LAKINI sisi wananchi tatizo letu KUU na la MSINGI ni KATIBA MPYA!

BILA KUIFANYA KATIBA MPYA KUWA NDIYO AJENDA MAMA
ya maandamano basi haya maandamano ni JOKE yaani ni KICHEKESHO na ni muendelezo uleule tu wa wanasiasa kutaka kututumia wananchi kama ngazi ili kufikia malengo yao ya kisiasa ambayo kimsingi siasa ni ajira yao!.

Haitoshi kuchomekea vijmaneno vya hapa na pale kuhusu katiba mpya ili kulainisha mioyo ya watu, tunataka ajenda KUU iwe ni KATIBA MPYA.

Nje ya hapo, Mbowe na Wanachadema wenzako kama mnadhani uchaguzi ndiyo tatizo kuu nchini basi kaandamaneni. lakini nawajulisha tu kuwa Ajenda yenu imekaa kivyama, haijakaa kitaifa na kwa hiyo hata wanaCCM ambao wangewaunga mkono kuandamana kama ajenda yenu kuu ingekuwa ni KATIBA mpya hawataandamana kwa sababu mmeweka mbele mambo ya uchaguzi.
 
Kwa nini wewe usiidai hiyo katiba badala yao?Timiza wajibu wako.Wao wamechagua lililowijia vichwani mwao kwa uhitaji.Au na katiba mpya unapenda nayo wakudaie?
Waende tu wakaandamane, wasitushawishi na sisi kuandamano kwa kitu ambacho siyo tatizo letu kuu!.

Siku wakija na ajenda kuu ambayo ni katiba mpya hapo tutazungumza na tutakuwa tayari kuandamana kwa moyo wote!
 
Waende tu wakaandamane, wasitushawishi na sisi kuandamano kwa kitu ambacho siyo tatizo letu kuu!.

Siku wakija na ajenda kuu ambayo ni katiba mpya hapo tutazungumza na tutakuwa tayari kuandamana kwa moyo wote!
Wewe unajipa madaraka ya kunisemea mimi why?,wewe kama umeona katiba no mbovu why usifanye push back ili upate katiba bora?,uoga wako wa kizuzu ndio unakusumbua na kujifanya ni warrior wa key boards, ingia mitaani ili udai katiba bora, usitegemee watu wengine wakupiganie na acha upumbavu huu
 
Sidhani kama wamemlazimisha mtu yoyote kuandamana.

Na unfortunately uwezo wa kumlazimisha mtu hawana. Wanahitaji ushawishi zaidi, na kwa ajenda hii waliyokuja nayo hata ushawishi wenyewe ni mdogo sana!. Kiufupi ajenda yao ya mambo ya uchaguzi ni JOKE haina ushawishi wa maana kwa umma!
 
Na unfortunately uwezo wa kumlazimisha mtu hawana. Wanahitaji ushawishi zaidi, na kwa ajenda hii waliyokuja nayo hata ushawishi wenyewe ni mdogo sana!. Kiufupi ajenda yao ya mambo ya uchaguzi ni JOKE haina ushawishi wa maana kwa umma!
Mbona wewe ndiyo unalalamika zaidi kama umelazimishwa?Kwa nini usitulie uwaache na mambo yao?
 
Katika nchi yetu tatizo la msingi siyo sheria za uchaguzi, Tatizo la msingi ni katiba mbovu inayozaa mfumo mbovu wa uongozi na utawala, mfumo mbovu wa haki na mfumo mbovu wa uwajibikaji.

Nashangaa chama kikuu cha upinzani ambacho kinajua wazi kuwa mzizi wa fitina ni katiba mbovu, hakina interest ya kuifanya katiba mpya kuwa ndiyo KILIO KIKUU cha kuwaingiza watu barabarani, lakini chenyewe kinaweka mbele mambo ya uchaguzi as if uchaguzi ndiyo tatizo kuu.

Hii inatoa taswira gani?, inatoa Taswira kuwa viongozi wa CHADEMA wao kinachowakera zaidi hadi kupata ujasiri wa kutaka kuwaingiza watu mabarabarani ni sheria zinazowakwaza kuingia bungeni au kupata udiwani. Otherwise kama kweli wana uchungu na wananchi kwa ujumla wake kwa nini Maandamano wanayoitisha yasiwe na AJENDA KUU YA MSINGI AMBAYO NI KUDAI KATIBA MPYA?

Uchaguzi wa mwaka 2020 ulipofanyika, Magufuli akawapiga akina Mbowe na kitu kizito kichwani waliwaambaia wananchi kuwa kamwe hawawezi kushiriki tena uchaguzi chini ya katiba ya sasa na tume hii ya uchaguzi. Sasa Magufuli hayupo, wanahisi wana chance ya kuingia mjengoni tena kwa hiyo wako tayari kusettle na "minimum" reforms za kuwawezesha kuingia tena mjengoni kula kodi za wananchi!.

Mimi nasema kama CHADEMA wanataka kuandamana kama chama ili watngenezewe sheria watakazozipenda za kuwawezesha kupata hivyo viti vya ubunge na ruzuku iongezeke, basi ni kheri kwao wacha waandamane, LAKINI sisi wananchi tatizo letu KUU na la MSINGI ni KATIBA MPYA!.

BILA KUIFANYA KATIBA MPYA KUWA NDIYO AJENDA MAMA
ya maandamano basi haya maandamano ni JOKE yaani ni KICHEKESHO na ni muendelezo uleule tu wa wanasiasa kutaka kututumia wananchi kama ngazi ili kufikia malengo yao ya kisiasa ambayo kimsingi siasa ni ajira yao!.

Haitoshi kuchomekea vijmaneno vya apa na pale kuhusu katiba mpya ili kulainisha mioyo ya watu, tunataka ajenda KUU iwe ni KATIBA MPYA.

Nje ya hapo, Mbowe na Wanachadema wenzako kama mnadhani uchaguzi ndiyo tatizo kuu nchini basi kaandamaneni. lakini nawajulisha tu kuwa Ajenda yenu imekaa kivyama, haijakaa kitaifa na kwa hiyo hata wanaCCM ambao wangewaunga mkono kuandamana kama ajenda yenu kuu ingekuwa ni KATIBA mpya hawataandamana kwa sababu mmeweka mbele mambo ya uchaguzi.
Wala huna haja ya kuwazodoa, wao wamechagua waliyoyachagua, sasa ni wewe tu kuandamania hiyo katiba unayoisema.
 
usidanganyike wote ni wamoja hao wanazuga tu ili waonekane au kuonekane kuna upinzani lkn wote wana bosi mmoja …
 
Katika nchi yetu tatizo la msingi siyo sheria za uchaguzi, Tatizo la msingi ni katiba mbovu inayozaa mfumo mbovu wa uongozi na utawala, mfumo mbovu wa haki na mfumo mbovu wa uwajibikaji.

Nashangaa chama kikuu cha upinzani ambacho kinajua wazi kuwa mzizi wa fitina ni katiba mbovu, hakina interest ya kuifanya katiba mpya kuwa ndiyo KILIO KIKUU cha kuwaingiza watu barabarani, lakini chenyewe kinaweka mbele mambo ya uchaguzi as if uchaguzi ndiyo tatizo kuu.

Hii inatoa taswira gani?, inatoa Taswira kuwa viongozi wa CHADEMA wao kinachowakera zaidi hadi kupata ujasiri wa kutaka kuwaingiza watu mabarabarani ni sheria zinazowakwaza kuingia bungeni au kupata udiwani. Otherwise kama kweli wana uchungu na wananchi kwa ujumla wake kwa nini Maandamano wanayoitisha yasiwe na AJENDA KUU YA MSINGI AMBAYO NI KUDAI KATIBA MPYA?

Uchaguzi wa mwaka 2020 ulipofanyika, Magufuli akawapiga akina Mbowe na kitu kizito kichwani waliwaambaia wananchi kuwa kamwe hawawezi kushiriki tena uchaguzi chini ya katiba ya sasa na tume hii ya uchaguzi. Sasa Magufuli hayupo, wanahisi wana chance ya kuingia mjengoni tena kwa hiyo wako tayari kusettle na "minimum" reforms za kuwawezesha kuingia tena mjengoni kula kodi za wananchi!.

Mimi nasema kama CHADEMA wanataka kuandamana kama chama ili watngenezewe sheria watakazozipenda za kuwawezesha kupata hivyo viti vya ubunge na ruzuku iongezeke, basi ni kheri kwao wacha waandamane, LAKINI sisi wananchi tatizo letu KUU na la MSINGI ni KATIBA MPYA!

BILA KUIFANYA KATIBA MPYA KUWA NDIYO AJENDA MAMA
ya maandamano basi haya maandamano ni JOKE yaani ni KICHEKESHO na ni muendelezo uleule tu wa wanasiasa kutaka kututumia wananchi kama ngazi ili kufikia malengo yao ya kisiasa ambayo kimsingi siasa ni ajira yao!.

Haitoshi kuchomekea vijmaneno vya apa na pale kuhusu katiba mpya ili kulainisha mioyo ya watu, tunataka ajenda KUU iwe ni KATIBA MPYA.

Nje ya hapo, Mbowe na Wanachadema wenzako kama mnadhani uchaguzi ndiyo tatizo kuu nchini basi kaandamaneni. lakini nawajulisha tu kuwa Ajenda yenu imekaa kivyama, haijakaa kitaifa na kwa hiyo hata wanaCCM ambao wangewaunga mkono kuandamana kama ajenda yenu kuu ingekuwa ni KATIBA mpya hawataandamana kwa sababu mmeweka mbele mambo ya uchaguzi.

..Nadhani Press release ya Chadema imejibu hoja yako.

..Mswada wa kuandika katiba mpya ni sehemu ya madai ktk maandamano.
 
Katika nchi yetu tatizo la msingi siyo sheria za uchaguzi, Tatizo la msingi ni katiba mbovu inayozaa mfumo mbovu wa uongozi na utawala, mfumo mbovu wa haki na mfumo mbovu wa uwajibikaji.

Nashangaa chama kikuu cha upinzani ambacho kinajua wazi kuwa mzizi wa fitina ni katiba mbovu, hakina interest ya kuifanya katiba mpya kuwa ndiyo KILIO KIKUU cha kuwaingiza watu barabarani, lakini chenyewe kinaweka mbele mambo ya uchaguzi as if uchaguzi ndiyo tatizo kuu.

Hii inatoa taswira gani?, inatoa Taswira kuwa viongozi wa CHADEMA wao kinachowakera zaidi hadi kupata ujasiri wa kutaka kuwaingiza watu mabarabarani ni sheria zinazowakwaza kuingia bungeni au kupata udiwani. Otherwise kama kweli wana uchungu na wananchi kwa ujumla wake kwa nini Maandamano wanayoitisha yasiwe na AJENDA KUU YA MSINGI AMBAYO NI KUDAI KATIBA MPYA?

Uchaguzi wa mwaka 2020 ulipofanyika, Magufuli akawapiga akina Mbowe na kitu kizito kichwani waliwaambia wananchi kuwa kamwe hawawezi kushiriki tena uchaguzi chini ya katiba ya sasa na tume hii ya uchaguzi. Sasa Magufuli hayupo, wanahisi wana chance ya kuingia mjengoni tena kwa hiyo wako tayari kusettle na "minimum" reforms za kuwawezesha kuingia tena mjengoni kula kodi za wananchi!.

Mimi nasema kama CHADEMA wanataka kuandamana kama chama ili watngenezewe sheria watakazozipenda za kuwawezesha kupata hivyo viti vya ubunge na ruzuku iongezeke, basi ni kheri kwao wacha waandamane, LAKINI sisi wananchi tatizo letu KUU na la MSINGI ni KATIBA MPYA!

BILA KUIFANYA KATIBA MPYA KUWA NDIYO AJENDA MAMA
ya maandamano basi haya maandamano ni JOKE yaani ni KICHEKESHO na ni muendelezo uleule tu wa wanasiasa kutaka kututumia wananchi kama ngazi ili kufikia malengo yao ya kisiasa ambayo kimsingi siasa ni ajira yao!.

Haitoshi kuchomekea vijmaneno vya hapa na pale kuhusu katiba mpya ili kulainisha mioyo ya watu, tunataka ajenda KUU iwe ni KATIBA MPYA.

Nje ya hapo, Mbowe na Wanachadema wenzako kama mnadhani uchaguzi ndiyo tatizo kuu nchini basi kaandamaneni. lakini nawajulisha tu kuwa Ajenda yenu imekaa kivyama, haijakaa kitaifa na kwa hiyo hata wanaCCM ambao wangewaunga mkono kuandamana kama ajenda yenu kuu ingekuwa ni KATIBA mpya hawataandamana kwa sababu mmeweka mbele mambo ya uchaguzi.
Naunga Mkono hoja
 
Chadema ni chama cha siasa, sasa sijui kwanini hutaki chama cha siasa kifanye yale yaliyo ndani ya mahitaji yao, hiyo ni interest yao, hawawezi kuacha mambo ya uchaguzi wakapiganie mambo ya pembejeo za kilimo na mengine, hayo yana wenyewe pia.

Suala la Katiba Mpya ni jumuishi, linahitaji muunganiko wa makundi tofauti kwenye kuidai, sasa hayo makundi yako wapi kuidai? kama hayaonekani kwanini unawalaumu Chadema kwa kutoonekana kwao?

Kwenye andiko lako ni kama vile umewafanya Chadema ndio wawe viongozi wa hili taifa kwenye kila jambo, sio vibaya ni jambo zuri.

Lakini pale mahitaji yanapokuwa mengi, huku wakati ukiwa hauruhusu, basi tukubaliane, na makundi mengine nayo lazima yajitokeze kusogeza mbele ajenda nyingine, Chadema wasiachiwe kila kitu watachoka, kwani nasi wengine huwa tunakuwa wapi kujiongeza badala ya kulalamika kila siku?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
..Nadhani Press release ya Chadema imejibu hoja yako.

..Mswada wa kuandika katiba mpya ni sehemu ya madai ktk maandamano.
Kwa muda uliobaki kupata katiba mpya ni ndoto .

Ccm wameweza kuwapiga chenga Chadema na Watanzania kwa ujumla baada ya kufanikiwa kumghilibu Mbowe.

Mbowe nae aliamua kupuuza ushauri wa Watanzania kuhusu kinachoitwa maridhiano akiamini ataweza kuwakabili na kuwazidi kete Ccm peke yake.

Kiufupi hayo maandamano ni njia ya Mbowe kutuonyesha umma kwamba japo wamerubuniwa na genge la Ccm ila bado yupo imara, sidhani kama hii itasaidia sana hasa baada ya yeye kuwadharau watoa maoni kuhusu mwenendo wa kile kilichoitwa maridhiano.

Hayo maandamano hayawezi kuitisha Ccm maana wameshapata walichokitaka, kiufupi Ccm wamemtumia Mbowe kuishinda sauti ya wadai mabadiliko.

Hakuna cha kujifunza kwenye hili zaidi ya kusema ni vizuri kusikilizwa maoni hata kama huyakubali ila yasikilize tu na usiyatekeleze.

brazaj econonist Tindo zitto junior Nguruvi3
 
Kwa muda uliobaki kupata katiba mpya ni ndoto .

Ccm wameweza kuwapiga chenga Chadema na Watanzania kwa ujumla baada ya kufanikiwa kumghilibu Mbowe.

Mbowe nae aliamua kupuuza ushauri wa Watanzania kuhusu kinachoitwa maridhiano akiamini ataweza kuwakabili na kuwazidi kete Ccm peke yake.

Kiufupi hayo maandamano ni njia ya Mbowe kutuonyesha umma kwamba japo wamerubuniwa na genge la Ccm ila bado yupo imara, sidhani kama hii itasaidia sana hasa baada ya yeye kuwadharau watoa maoni kuhusu mwenendo wa kile kilichoitwa maridhiano.

Hayo maandamano hayawezi kuitisha Ccm maana wameshapata walichokitaka, kiufupi Ccm wamemtumia Mbowe kuishinda sauti ya wadai mabadiliko.

Hakuna cha kujifunza kwenye hili zaidi ya kusema ni vizuri kusikilizwa maoni hata kama huyakubali ila yasikilize tu na usiyatekeleze.

brazaj econonist Tindo zitto junior Nguruvi3

..Ccm hawataki Katiba Mpya. Haijalishi Mbowe angesikiliza wakosoaji wake toka mwanzo au la.

..Ccm walishaandika Katiba Mpya iliyotokana na bunge maalum. Na wameificha Katiba hiyo. Hawataki.

..Alichofanya Mbowe ni sahihi. Huwezi kuwaambia wananchi waandamane wakati hujajaribu to the FULLEST njia ya mazungumzo.

..Kwa hapa tulipofika maamuzi ni yetu wananchi. Tunaweza kumuunga mkono Mbowe, au kumsusia. Maamuzi yote yana matokeo yake.
 
Katika nchi yetu tatizo la msingi siyo sheria za uchaguzi, Tatizo la msingi ni katiba mbovu inayozaa mfumo mbovu wa uongozi na utawala, mfumo mbovu wa haki na mfumo mbovu wa uwajibikaji.

Nashangaa chama kikuu cha upinzani ambacho kinajua wazi kuwa mzizi wa fitina ni katiba mbovu, hakina interest ya kuifanya katiba mpya kuwa ndiyo KILIO KIKUU cha kuwaingiza watu barabarani, lakini chenyewe kinaweka mbele mambo ya uchaguzi as if uchaguzi ndiyo tatizo kuu.

Hii inatoa taswira gani?, inatoa Taswira kuwa viongozi wa CHADEMA wao kinachowakera zaidi hadi kupata ujasiri wa kutaka kuwaingiza watu mabarabarani ni sheria zinazowakwaza kuingia bungeni au kupata udiwani. Otherwise kama kweli wana uchungu na wananchi kwa ujumla wake kwa nini Maandamano wanayoitisha yasiwe na AJENDA KUU YA MSINGI AMBAYO NI KUDAI KATIBA MPYA?

Uchaguzi wa mwaka 2020 ulipofanyika, Magufuli akawapiga akina Mbowe na kitu kizito kichwani waliwaambia wananchi kuwa kamwe hawawezi kushiriki tena uchaguzi chini ya katiba ya sasa na tume hii ya uchaguzi. Sasa Magufuli hayupo, wanahisi wana chance ya kuingia mjengoni tena kwa hiyo wako tayari kusettle na "minimum" reforms za kuwawezesha kuingia tena mjengoni kula kodi za wananchi!.

Mimi nasema kama CHADEMA wanataka kuandamana kama chama ili watngenezewe sheria watakazozipenda za kuwawezesha kupata hivyo viti vya ubunge na ruzuku iongezeke, basi ni kheri kwao wacha waandamane, LAKINI sisi wananchi tatizo letu KUU na la MSINGI ni KATIBA MPYA!

BILA KUIFANYA KATIBA MPYA KUWA NDIYO AJENDA MAMA
ya maandamano basi haya maandamano ni JOKE yaani ni KICHEKESHO na ni muendelezo uleule tu wa wanasiasa kutaka kututumia wananchi kama ngazi ili kufikia malengo yao ya kisiasa ambayo kimsingi siasa ni ajira yao!.

Haitoshi kuchomekea vijmaneno vya hapa na pale kuhusu katiba mpya ili kulainisha mioyo ya watu, tunataka ajenda KUU iwe ni KATIBA MPYA.

Nje ya hapo, Mbowe na Wanachadema wenzako kama mnadhani uchaguzi ndiyo tatizo kuu nchini basi kaandamaneni. lakini nawajulisha tu kuwa Ajenda yenu imekaa kivyama, haijakaa kitaifa na kwa hiyo hata wanaCCM ambao wangewaunga mkono kuandamana kama ajenda yenu kuu ingekuwa ni KATIBA mpya hawataandamana kwa sababu mmeweka mbele mambo ya uchaguzi.

1. Hoja iliyopo si ya kubeza bali kusikilizwa na kufanyiwa kazi.

2. Uzi huu hapa ulikuwa na agenda kama hii hii:

Jan 23/24, Maandamano yahusishe wadau wote

3. Unawahusisha wadau wote kwa agenda ya pamoja si vinginevyo.

4. Mleta mada ana hoja, isikilizwe.

5. Kuwa tayari kusikiliza na kupokea Ushauri si unyonge bali a way of enormous strength.

Proved, Economist, JokaKuu
 
Katika nchi yetu tatizo la msingi siyo sheria za uchaguzi, Tatizo la msingi ni katiba mbovu inayozaa mfumo mbovu wa uongozi na utawala, mfumo mbovu wa haki na mfumo mbovu wa uwajibikaji.

Nashangaa chama kikuu cha upinzani ambacho kinajua wazi kuwa mzizi wa fitina ni katiba mbovu, hakina interest ya kuifanya katiba mpya kuwa ndiyo KILIO KIKUU cha kuwaingiza watu barabarani, lakini chenyewe kinaweka mbele mambo ya uchaguzi as if uchaguzi ndiyo tatizo kuu.

Hii inatoa taswira gani?, inatoa Taswira kuwa viongozi wa CHADEMA wao kinachowakera zaidi hadi kupata ujasiri wa kutaka kuwaingiza watu mabarabarani ni sheria zinazowakwaza kuingia bungeni au kupata udiwani. Otherwise kama kweli wana uchungu na wananchi kwa ujumla wake kwa nini Maandamano wanayoitisha yasiwe na AJENDA KUU YA MSINGI AMBAYO NI KUDAI KATIBA MPYA?

Uchaguzi wa mwaka 2020 ulipofanyika, Magufuli akawapiga akina Mbowe na kitu kizito kichwani waliwaambia wananchi kuwa kamwe hawawezi kushiriki tena uchaguzi chini ya katiba ya sasa na tume hii ya uchaguzi. Sasa Magufuli hayupo, wanahisi wana chance ya kuingia mjengoni tena kwa hiyo wako tayari kusettle na "minimum" reforms za kuwawezesha kuingia tena mjengoni kula kodi za wananchi!.

Mimi nasema kama CHADEMA wanataka kuandamana kama chama ili watngenezewe sheria watakazozipenda za kuwawezesha kupata hivyo viti vya ubunge na ruzuku iongezeke, basi ni kheri kwao wacha waandamane, LAKINI sisi wananchi tatizo letu KUU na la MSINGI ni KATIBA MPYA!

BILA KUIFANYA KATIBA MPYA KUWA NDIYO AJENDA MAMA
ya maandamano basi haya maandamano ni JOKE yaani ni KICHEKESHO na ni muendelezo uleule tu wa wanasiasa kutaka kututumia wananchi kama ngazi ili kufikia malengo yao ya kisiasa ambayo kimsingi siasa ni ajira yao!.

Haitoshi kuchomekea vijmaneno vya hapa na pale kuhusu katiba mpya ili kulainisha mioyo ya watu, tunataka ajenda KUU iwe ni KATIBA MPYA.

Nje ya hapo, Mbowe na Wanachadema wenzako kama mnadhani uchaguzi ndiyo tatizo kuu nchini basi kaandamaneni. lakini nawajulisha tu kuwa Ajenda yenu imekaa kivyama, haijakaa kitaifa na kwa hiyo hata wanaCCM ambao wangewaunga mkono kuandamana kama ajenda yenu kuu ingekuwa ni KATIBA mpya hawataandamana kwa sababu mmeweka mbele mambo ya uchaguzi.


Watu wengi ambao wanadai katiba mpya, ukiwauliza changamoto ya katiba ya sasa hawajui hata moja

That's why serikali haina mpango wala uharaka wa kuchange katiba
 
Kwa nini wewe usiidai hiyo katiba badala yao?Timiza wajibu wako.Wao wamechagua lililowijia vichwani mwao kwa uhitaji.Au na katiba mpya unapenda nayo wakudaie?

1. Nikadhani hapa tunapewa changamoto za kuyavutia makundi mengi zaidi kushiriki?

2. Kwani makundi mengi yakishiriki si ni kwa maslahi zaidi?

3. Haya yalikuwa maoni kuntu ya kukumbatiwa kama yaliyomo humu:

Jan 23/24, Maandamano yahusishe wadau wote

4. Mleta mada (Missile of the Nation) alipaswa kupongezwa, si kubagazwa.

5. Kuyaleta makundi mengi kwa kadri iwezekanavyo ni fursa isiyostahili kubezwa:

F4coIWrWkAI9Dlw.jpeg


5. Alicholeta mleta mada ni maujanja au chachandu ya nyongeza.

6. Umoja ni nguvu.

Proved, JokaKuu, Economist
 
Mimi nilishawashtukia kitambo sana, janja janja hawa. Bora Mama mara 1000 mia.
 
Kwa muda uliobaki kupata katiba mpya ni ndoto .

Ccm wameweza kuwapiga chenga Chadema na Watanzania kwa ujumla baada ya kufanikiwa kumghilibu Mbowe.

Mbowe nae aliamua kupuuza ushauri wa Watanzania kuhusu kinachoitwa maridhiano akiamini ataweza kuwakabili na kuwazidi kete Ccm peke yake.

Kiufupi hayo maandamano ni njia ya Mbowe kutuonyesha umma kwamba japo wamerubuniwa na genge la Ccm ila bado yupo imara, sidhani kama hii itasaidia sana hasa baada ya yeye kuwadharau watoa maoni kuhusu mwenendo wa kile kilichoitwa maridhiano.

Hayo maandamano hayawezi kuitisha Ccm maana wameshapata walichokitaka, kiufupi Ccm wamemtumia Mbowe kuishinda sauti ya wadai mabadiliko.

Hakuna cha kujifunza kwenye hili zaidi ya kusema ni vizuri kusikilizwa maoni hata kama huyakubali ila yasikilize tu na usiyatekeleze.

brazaj econonist Tindo zitto junior Nguruvi3

1. Kwenye vita vya ukombozi kuna kupiga na kupigwa. Huwezi kutegemea kupiga kila siku.

2. Hatuna sababu ya kukata tamaa kwa sababu tulipo tumepigwa. Tatizo si kuwa tumeanguka bali tumeangukia wapi na tufanye je.

3. Uchaguzi unafanyika au haufanyiki bIla kuwapo katiba mpya hilo liko mikononi mwetu. Mleta mada (Missile of the Nation ) ana Ushauri kuntu hapa.

4. Anasema yaunganishwe makundi yote kudai katiba mpya ambamo humo hata CCM ya akina Pascal Mayalla wanaotaka katiba mpya watakuwamo.

5. Uzi wangu huu hapa chini ni mwendelezo wa maoni hayo hayo:

Jan 23/24, Maandamano yahusishe wadau wote

6. Uchaguzi si lazima ufanyike mwaka huu au mwakani.

7. Tukomae kudai katiba mpya.

8. Kudos mleta mada. Kwa hakika unastahili mada maua yako.
 
Back
Top Bottom