Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.
Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.
Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?
Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.
Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.
Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.
Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?
MSIKUBALI!
Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.
Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?
Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.
Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.
Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.
Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?
MSIKUBALI!