Chongolo anapaswa kupongezwa na sio kubezwa wasomi kwenda Veta kupata mafunzo ya ufundi stadi

Witiri

Member
Dec 12, 2022
38
68
Nitasema kweli daima,fitina kwangu mwiko. Na nitajielimisha kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu hiyo kwa manufaa yangu na wenzangu.

Hizi ni tu ya ahadi za kila mwana ccm mwenye kufuata itikadi na misingi ya cChama Cha Mapinduzi ambacho kwa sasa ndugu Daniel Chongolo ndiye katibu wake mkuu.

Ndugu Chongolo hivi karibuni alitoa ushauri wake kwa vijana wasomi wa kitanzania ambao wanasubiri ajira serikalini. Chongolo akiwa kama sehemu ya watunga ilani na wasimamizi wa sera aliwaeleza wasomi ushauri wenye nia ya kuwakwamua walipokwama kwenye mtego huitwao ajira.

Badala ya kupokea na kuanza kufanyia kazi ushauri ule, Vijana wasomi wakitanzania wameubeza na kudhani kwamba Chongolo ameaonesha dharau dhidi yao, wengine wakafika mbali na kuhoji kulikuwa na haja ipi ya vyuo vikuu kuanzishwa na muda wote huo ccm ilikuwa wapi?

Vijana wenzangu kwenda Veta sio dharau, wala sio matusi, kusomea ufundi sio laana kama mlevi mmoja aliyechoka kulamba asali kimya kimya sasa akaamua kupayuka na kuwaita vijana wenzetu wa boda boda kuwa wana laana, Vijana wenzangu vichwa vyenu vijazeni maarifa badala ya ujinga na kucheua upumbavu.

Nchi yetu bado ni changa mno kiumri bado hajitoshelezi kuajiri mamia kwa mamia, kwenda shule lengo kuu ni kukuweza kuyamudu mazingira yanayokuzunguka.

Ukiona elimu uliyokuwa nayo haijakuletea tija basi jaribu nyingine ili ikufae kwa mazingira ya sasa na sio kushupaza shingo kama wale wapumbav.

Mwaka 2021 Chama Cha Mapinduzi kiliagiza Ofisi ya Waziri mkuu kuanzisha programu kabambe ya kutoa nafasi ya ufadhili ya mafunzo ya ufundi stadi(uanagenzi) kwa vijana wa kitanzania wenye umri wa miaka 15 mpaka 35 katika Vyuo vyake vya ufundi.

Mwaka 2023 tarehe 22 mwezi wa 2 ofisi hiyo imetoa tena nafasi hizo nchi nzima na mwisho wa maombi ni tarehe 10 mwezi wa 3 na kufanya program hii sasa kutimu miaka mitatu (3).

Nahitimisha kwa kusema kwamba ndugu Chongolo alizungumza huku akiwa amebeba maono na mapenzi makubwa kwa vijana wote wa kitanzania wenye ari na nia ya kuitumikia na kufaidi matunda ya nchi yao, maono ya kupambana na wale maadui watatu ambao baba wataifa Mwalimu Nyerere alituachia ambao ni Ujinga, Maradhi na Umasikini.

MIMI KITILINGO RAMADHANI NAENDA VETA.
(0699826969) SARANGA, UBUNGO.
 
Mawazo kama hayo yangetoka kwa kiongozi wa kambi ya upinzani, labda kidogo angaliweza kueleweka japo kidogo kwa kuwa vyama hivyo havina uzoefu wowote ule wa kuiongoza serikali. Lakini kwa huyu KM wa CCM, ni kichekesho cha mwaka.

Yaani mhitimu wa chuo kikuu kurud chini VETA kwa ajili ya kupata mafunzo ya kazi za vitendo, na kwa ajili ya tuzo ya daraja la chini la astashahada! Hapana! Nakataa nasema tena hapana. Hivi kweli mtu huyu anatambua thamani na hadhi ya shahada ya chuo kikuu!? Naweza tu kusema ni kiazi mwingine katika ubora wake, na niishie hapo.
 
Ni vizuri chongoro kaonyesha elimu yetu ilivo mbovu na wao watawala hawana sera maalumu kwa wahitimu wao wa vyuo tuanzie hapo
 
Nitasema kweli daima,fitina kwangu mwiko. Na nitajielimisha kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu hiyo kwa manufaa yangu na wenzangu.

Hizi ni tu ya ahadi za kila mwana ccm mwenye kufuata itikadi na misingi ya cChama Cha Mapinduzi ambacho kwa sasa ndugu Daniel Chongolo ndiye katibu wake mkuu.

Ndugu Chongolo hivi karibuni alitoa ushauri wake kwa vijana wasomi wa kitanzania ambao wanasubiri ajira serikalini. Chongolo akiwa kama sehemu ya watunga ilani na wasimamizi wa sera aliwaeleza wasomi ushauri wenye nia ya kuwakwamua walipokwama kwenye mtego huitwao ajira.

Badala ya kupokea na kuanza kufanyia kazi ushauri ule, Vijana wasomi wakitanzania wameubeza na kudhani kwamba Chongolo ameaonesha dharau dhidi yao, wengine wakafika mbali na kuhoji kulikuwa na haja ipi ya vyuo vikuu kuanzishwa na muda wote huo ccm ilikuwa wapi?

Vijana wenzangu kwenda Veta sio dharau, wala sio matusi, kusomea ufundi sio laana kama mlevi mmoja aliyechoka kulamba asali kimya kimya sasa akaamua kupayuka na kuwaita vijana wenzetu wa boda boda kuwa wana laana, Vijana wenzangu vichwa vyenu vijazeni maarifa badala ya ujinga na kucheua upumbavu.

Nchi yetu bado ni changa mno kiumri bado hajitoshelezi kuajiri mamia kwa mamia, kwenda shule lengo kuu ni kukuweza kuyamudu mazingira yanayokuzunguka.

Ukiona elimu uliyokuwa nayo haijakuletea tija basi jaribu nyingine ili ikufae kwa mazingira ya sasa na sio kushupaza shingo kama wale wapumbav.

Mwaka 2021 Chama Cha Mapinduzi kiliagiza Ofisi ya Waziri mkuu kuanzisha programu kabambe ya kutoa nafasi ya ufadhili ya mafunzo ya ufundi stadi(uanagenzi) kwa vijana wa kitanzania wenye umri wa miaka 15 mpaka 35 katika Vyuo vyake vya ufundi.

Mwaka 2023 tarehe 22 mwezi wa 2 ofisi hiyo imetoa tena nafasi hizo nchi nzima na mwisho wa maombi ni tarehe 10 mwezi wa 3 na kufanya program hii sasa kutimu miaka mitatu (3).

Nahitimisha kwa kusema kwamba ndugu Chongolo alizungumza huku akiwa amebeba maono na mapenzi makubwa kwa vijana wote wa kitanzania wenye ari na nia ya kuitumikia na kufaidi matunda ya nchi yao, maono ya kupambana na wale maadui watatu ambao baba wataifa Mwalimu Nyerere alituachia ambao ni Ujinga, Maradhi na Umasikini.

MIMI KITILINGO RAMADHANI NAENDA VETA.
(0699826969) SARANGA, UBUNGO.
Yaani Mtu akimaliza darasa la Saba na mwandiko mbaya arudi la Kwanza afundishwe jinsi ya kuumba herufi? Huwa mko tayari kusapoti ujinga ilimradi umesemwa na kiongozi wa CCM. Kwa nini hamkuona mwanzo umuhimu wa cheti cha ufundi mkawaacha Vijana wakasoma shahada ya uhandisi halafu Leo mnamtaka mhandisi akasomee ufundi mchundo?
 
Ishu hapa ni hoja iliyotolewa tuichambue tusimchambue mtoa hoja, kiukweli haina maana kuwa na cheti cha chuo kikuu wakati kwa kazi hiyohiyo practically Huna hata uwezo wiwote unashindwa hata na kijana aliyeishia darasa la saba na kwenda veta kupata ujuzi wa kazi za mikono
 
Back
Top Bottom