Kauli hii inanikera, nifanyeje?

Kauli hii inanikera, nifanyeje?

yani ni raha mfano hakuna sasa huyu anamaliza kujenga nyumba halafu hampi nafasi mkewe kutengeneza nyumbani!hapo ndo matokeo yake huwa hivi!

tutapata taarifa kesho nini kimejiri baada ya kupata maushauri........
 
Mkuu.@Tutor mvumilie ndio kauli za wanawake kauli zao kubwa hiyo pia mojawapo nipe Talaka yangu neende kwetu nimeshachoka kuishi na wewe anakutisha wala usibabaike mvumilie tu yatakwisha hayo kaka.
 
Kwanini usijisimamie mwenyewe kuipinga kauli hiyo mpaka uombe na wengine?

Hujaona hapo nimemwambia sikubali apite bila kupingwa? Na nimemwambia awaombe radhi wanawake? Hao wengine nimewaita ili maandamano ya kupinga hiyo kauli yasikike zaidi na yawe na nguvu.
 
Kama sababu ya huo ugomvi haihusiani na wewe kutembea nje au kutoitimizia familia mahitaji ya msingi
Waje kujaribu kwani kwako ni testing ground?
Uyo kuna mtu anamtia icho kiburi usikute anakatwa na kuhongwa mpige chini na ilo buzi lazima litampiga chini mwisho wa siku shida zikimzidi atarudi
Au usikute anatikisa kiberiti tuu
 
Wawezaje kujitambua kuwa una mapungufu ya namna hizo zote?

Kwa hali ya kawaida m2 yeyote mwenye tabia ya kujisimamia kwa mambo mengi huwa anasemekana kuwa na dharau. Mimi kama mimi napenda kujisimamia kwa mambo mengi, labda ndo tatizo.

Niwaelezeni kitu;
Kuliwahi kutokea mgogoro mdogo - akawaita wadhamini wa ndoa eti tuuongelee; niliwatimua na kuwambia kuwa sijawaita; mambo ya nyumbani kwangu hasa yanayohusiana na ndoa napenda niya-handle mwenyewe. Hivyo ndivyo nilivyo!

kujisimamia na kuwa na dharau ni vitu viwili tofauti...........

Na unaposema tatizo dogo, dogo kwa nani kwake au kwako?
Mpaka kuita wasimamizi maana yake alishakuonya mara kadhaa hukusikia....
- hilo nalo ni tatizo inaelekea hujali hisia za mkeo na humsikilizi, ukifanya maamuzi humsikilizi, mkeo sio jiwe kwamba afate utakzcho,ni binadamu, ana akili timamu na uwezo wa kufanya maamuzi... Ndoa ni kusikilizana....... Huwezi dharau mwenzio kwa kisingizio cha 'kijisimamia',watu wanajisimamia na wenza wao wanawasikiliza....

Unasema uliwatimua waimamizi wa ndo walipofika, je ndo adabu hiyo?
+hilo nalo ni tatizo, ulipaswa uwaombe radhi kwa usumbufu, na kuwaeleza wawape muda mlishughulikie tatizo lililopo kwanza....then mkacheka, mkala, mkanywa na siku kupita....

KWA HAYA ULIYOYAOYAANDIKA......
KISHA PITIA MAJIBU YAKO KWENYE THREAD HII
UTAJITAMBUA WEWE NI MWANAUME WA AINA GANI
KINACHOMFANYA MKEO AKUJIBU ANAYOKUJIBU KIPO HATA KWENYE THREAD YAKO...

Pitia comments zako utapata jibu
 
Eh! hiyo kali m2 wangu!

Imenikumbusha mshkaji wangu mmoja alosema hivi "wanawake si ndugu / rafiki wala .... ni watu tu! " Utawazaje kuacha kwako na kuamia kwa mwingine kama kweli zinakutosha?

umeona posti kama hii?

Adabu kwa mkeo ndugu.......... Na usipojirekebisha wenzio watakusaidia kumliwaza mkeo.....

You need to chang
 
lol!wanaume wenzio wanaofaidi utamu wa wanawake wakisikia maneno kama haya huwa waagiza mug tu za kilauri wanakata kilaji na nyama choma huku wakimsifu Muumba kwa heri alizowajalia na baraka za kumiliki wanawake wa aina yetu!wapi Kaizer , Asprin, Mtambuzi The Boss, Dark City , HorsePower ,pacha wangu mtoto wa mama yangu SnowBall na wengine woote MNAOJIAMINI NI WANAUME WA UKWELI bila kumsahau mtani wangu watu8, Erickb52, kakaangu moto2012 na mashosti zangu WANAWAKE WA UKWELI gfsonwin, mke mwanzangu wa sirini cacico, FP dadangu uvi koki dada mkubwa? na wengine woote wa mrengo wa kulia

Nipo mwanawane, bado sie huko hatujafikishana japo tuna miaka 9 sasa ya ndoa...........LOL
Ngoja nijifunze hapa toka kwa wadau maana huenda ndoa yetu ikifikisha miaka kumi, na mie nitajajibiwa hivyo.....

Haya tiririkeni hapa nijifunze mie.
 
Basi jaribu kukaa na huyo mwenzi wako akueleze nini haswa huwa kinamkera toka kwako....pengine huwa hamna wasaa wa kurekebishana pale mnapokoseana zaidi ya kutumia maneno ya hasira na kejeli...

Huu ndio ukweli, kila mmoja amemkinai mwenzie hivo hawapo tayari kukaa chini kurekebisha tofauti zao.
Na yawezekana kuna mmoja kati yao ni mmbabe, hayupo tayari kumsikiliza mwenzie, atakachosema yeye ndio amri.
 
sio kama namtetea,ila jamani mwanamme mpaka alalamike ujue maji yamefika shingoni.wanaume huwa hawapendi sana kulalamika.kaa chini na mke wako,ongea nae sio kwa ukali,muulize kitu gani kinachomfanya awe hivyo.na wewe pia kitu gani ambacho mke wako hakipendi kwako.kumbushaneni mwanzo wa mapenzi yenu yalivyokuwa,nakushauri kuna movie moja iangalie ya ki nigeria inaitwa mr and mrs.utajifunza mengi.kuhusu mambo ya ndoa na kuna mafunzo yake.
 
Ulikuwa wapi m2 wangu? nashukuru sana kwa ushauri wako; ila naamini mengi kati ya uloyataja najituma mkuu.

mkuu Tutor B nipo mtu wangu
nilikuwa nawasoma akina snowhite, Blaki Womani na wengineo wenye kujua masuala ya ndoa na nione wanasemaje kwanza
Sio uone kama vile unafanya ila fanya mpaka ufikie kiwango chako na kamwe usimuulize au kumwambia mwanamke eti umekosa nini kwangu kama chakula nakupa na mavazi na malazi sijui na usafiri
hayo ni ya ziada wala sio ya muhimu kwake
Muhimu sana kwake ni wewe na unavyomhandle na kumjali na kumpa maneno mazuri na sifa za hapa na pale za kila siku
The way unavyoongea nae hata unapojua kwamba hapa kachemsha ila humuonyeshi kuwa kachemsha unamsifia hata pale ambapo unaona kwamba ni wrong
Nyama ya ulimi mkuu na maneno mazuri na zaidi usimlinganishe wala kumfananisha na mwanamke yeyote mliyewahi kukutana nae
 
Last edited by a moderator:
lol!wanaume wenzio wanaofaidi utamu wa wanawake wakisikia maneno kama haya huwa waagiza mug tu za kilauri wanakata kilaji na nyama choma huku wakimsifu Muumba kwa heri alizowajalia na baraka za kumiliki wanawake wa aina yetu!wapi Kaizer , Asprin, Mtambuzi The Boss, Dark City , HorsePower ,pacha wangu mtoto wa mama yangu SnowBall na wengine woote MNAOJIAMINI NI WANAUME WA UKWELI bila kumsahau mtani wangu watu8, Erickb52, kakaangu moto2012 na mashosti zangu WANAWAKE WA UKWELI gfsonwin, mke mwanzangu wa sirini cacico, FP dadangu uvi koki dada mkubwa? na wengine woote wa mrengo wa kulia
Huyu wala asitupotezee muda wetu, anakipata anachokistahili..... Unawezaje kupanda bangi ukategemea kuvuna chai?
 
Nipo mwanawane, bado sie huko hatujafikishana japo tuna miaka 9 sasa ya ndoa...........LOL
Ngoja nijifunze hapa toka kwa wadau maana huenda ndoa yetu ikifikisha miaka kumi, na mie nitajajibiwa hivyo.....

Haya tiririkeni hapa nijifunze mie.
Mimi Nina miaka 13 ya ndoa na wala sijawahi hata kufikiria kuwa ninaweza kuwa na nyumba nyingine zaidi ya niliyonayo sembuse kumjibu mtu! Huyo dada angekuwepo huku labda angeweza kutuambia ni nini kinachomfanya amjibu mumewe hivyo. Unafikiri Kama mume anakutreat kama trash utashindwaje kuwaza kurudi kwenu? Kwa post zake humu naona mtoa mada Hana heshima kabisa kwa wanawake........sijui mwenzenu alzaliwa na nani?
 
Kuna mengi katika maisha ya ndoa zaidi ya watoto, haijalishi ni ndoa ya kanisani au msikitini,kama huna hawala ila mazingira yote yanayokuzunguka yanaonesha hivyo unategemea nini toka kwa mwenza wako?

Maisha ya ndoa ni magumu sana hasa kwa vile nyie mmekutana huku mkiwa mmelelewa katika mazingira tofauti hivyo kuoneshana tabia tofauti ni jambo la kawaida na yafaa ukawa mvumilivu kwa mwenzio,na kama unaona hukosei basi kaa nae chini na zungumza nae jambi hili na mtafikia muafaka maana kwangu mimi si rahisi mwanamke kukwambia ana kwao na kusiwe na sababu inayomfanya aseme maneno hayo.

Mkuu hapo kwenye Bold ulitaka kusema nn?
 
Kila tukiwa na mtafaruku na
mama watoto wangu ananambia kauli hii "Nitawapisha wengine waje
wajaribu, nina kwetu"
Hivi mwanamke aliyeolewa, yuko ndani ya ndoa
zaidi ya miaka 10 anaweza kuendeleaje kufikiria kurudi kwao badala ya
kufikiria kujenga mji wake ambao unaweza kuwa kimbilio kwa jamaa zake
wanaoweza kuwa na matatizo?
Akili au matope??????

KAULI HII INANIKERA SANA!

Ni utoto tu,akikua ataacha!
 
Tutor B umetia aibu sana.

Mwanamke ni kioo cha mwanaume, nikiona na mkeo kabla ya kuonana na wewe nitaweza kujua wewe ni mtu wa namna gani. Tukimwangalia mkeo tunaweza kupata taswira yako kwake, ni juu yako kuifanya hiyo taswira kuwa njema au la!!

Kwa mfano maelezo haya tayari nimeshajua tabia yako na huyo mke wako anajutia sana kuishi na wewe hiyo ndoa na watoto ndio vinavyomkwaza la sivyo angesha kuacha.

Jaribu kubadilika na yeye atabadilika na utashangaa mwenyewe, ubabe haulipi.
 
wanawake ni kama mvua inanyesha sehemu yoyote ile hata kama ni kwenye kinyesi kwa kifupi hata ufanyeje kikubwa ni uvumilivu tu. Nje ya hapo utavunja ndoa, utakuwa na wananwake hata zaidi ya 10 haijarishi umri wao maana ndio walivyo
 
Mkuu hapo kwenye Bold ulitaka kusema nn?
Nkusa nilimaanisha JAMBO,kwa mtu ambaye kaenda shule anaelewa kuwa wakati unaandika unaweza kukosea lakini maana ya sentesi inabaki kuwa pale pale.
 
Back
Top Bottom