Da Womanizer
JF-Expert Member
- May 24, 2010
- 1,577
- 151
Siku nyingine akitishia nyau mwambie kama vipi asepe uone atasemaje
usiwe na wasiwasi mamdogoumemkalishaaaaa!aminia haya akueleze tatizo lake umtatulie!
Mume ni kichwa cha nyumba. Mume asipoimiliki nafasi yake sawasawa kunakuwa na udhaifu wa mahusiano. Chukueni nafasi zenu kama viongozi wa nyumba. Pia msisahau kuwa Mungu amewataka wanawake wawatii waume zao na wanaume wawapende wake zao. Je mnawapenda wake zenu?? Jichunguzeni kwanza ili owte mvumiliane na kuishi kwa upendo.
snowhite mhhh haya maswali akiweza kuyajibu atajua umuhimu wa ndoa yake na nini kina kasoro katika ndoa yakekukua sio umri kakangu ni uzoefu na busara jinsi ya kuishi na watu!
kwanza pole na yote!ndo ukubwa huo!
nimekuuliza maswali yangu kama sita hizi kwenye post imepita
1.wewe na mkeo mna mawasiliano ya aina gani?
2.unamsikiliza kihisia,yani unaweza kumuelewa hata kabla hajaongea kitu?
3.mkeo anajivunia wewe kuwa mume wake?
4.wewa unafahamu thamani ya ndoa,mke na familia?
5.unatimiza wajibu wako kama mume(hii ni zaidi ya kuwa baba yani kuwa na uwezo wa kuleta watoto duniani)
6.mna nafasi ya kusali na mkeo pamoja?
7.mkeo ana fahamu hili linakukera kiasi gani?ulishawahi kumwambia na kumuonyesha kuwa hupendi?
8.mkeo anajua nafasi yake yeye kama mwanamke kwenye akili yako?
9.wewe unajua mapungufu yako kama mume na kama mwanaume?(hivi ni vitu viwili tofauti)
10.value ndoa yako katika makundi yafutayo
A)NI NZURI NAITHAMINI NA NI MIMI KATIKA UKAMILIFU WANGU
B)YA KAWAIDA NAKUBALI CHANGAMOTO
C)SI MUHIMU NAWEZA KUISHI MWENYEWE
nimekubali hoja nimeshuhudia ndoa mbili zikivunjika sababu ya mambo uliyoyataja hapo juu mkuuKero za ndoa sio kuwa na mahawara tu, inawezekana huna mahawara ila labda
-una kauli mbaya
-una ghubu, kosa la miaka kumi iliyopita utalikumbusha weee
-mchoyo
-mbinafsi
-humjali
-mkorofi
-mbabe
-hushauriki
-una dharau na nyodo
na mengineyo, hivyo jichunguze
Mume ni kichwa cha nyumba. Mume asipoimiliki nafasi yake sawasawa kunakuwa na udhaifu wa mahusiano. Chukueni nafasi zenu kama viongozi wa nyumba. Pia msisahau kuwa Mungu amewataka wanawake wawatii waume zao na wanaume wawapende wake zao. Je mnawapenda wake zenu?? Jichunguzeni kwanza ili owte mvumiliane na kuishi kwa upendo.
Ciello hakupenda pesa alimipenda mimi ndio maana akanieleza anachohitaji, ila ndo ivyo watu wachawi wametimia unafiki hata mke kaniacha, nam chukua Baba V, Mtambuzi na ErickB52 hawa ndio chanzo.... Cha kunitenganisha na wife
Pole sina cha kukushauri ila nitakuombea ili hiyo hali iishe ukae kwa amani kwani umeshapewa ushauri mzuri humu.Nilivyosoma majibu yako unaelekea you are very good man.Ongea na mkeo mweleze kinachokukera waziwazi mweleweshe na umwonjeshe mmekua sasa na siyo wakati wakutupiana maneno kama hayo.
Unamjua Mkeo better than anyone in this world ukitoa labda wazazi wake.
Tutor B hapo ndipo unapofanya kosa kudhani kuwa mwanamke anahitaji hayo tuu usafiri, chakula, mahitaji yake ya kawaida ambayo wanakuambia hata kwao yapo na angeweza kuyapata hata akiwa kwaoKwenye kuwapenda sijui wamaanisha nini?
Nilim-aproach;
Nikatoa mahali;
Nikafunga naye ndoa;
Nikaanza kuishi naye tukiwa tunapanga;
Tumekaa na kushauliaana hadi tukajenga nyumba (sio mojatu);
Usafiri upo; na si kwamba nautumia mimi mara kwa mara;
Kwa ujumla mambo ya nyumbani (matumizi) sio mgogoro hata kidogo;
Ndugu zake wakiwa na matatizo nawasaidia kama kawaida;
Yeye akiwa na shida inakuwa shida yetu wote;
NIMPENDEJE?
hebu hama hapo!Kwenye kuwapenda sijui wamaanisha nini?
Nilim-aproach;
Nikatoa mahali;
Nikafunga naye ndoa;
Nikaanza kuishi naye tukiwa tunapanga;
Tumekaa na kushauliaana hadi tukajenga nyumba (sio mojatu);
Usafiri upo; na si kwamba nautumia mimi mara kwa mara;
Kwa ujumla mambo ya nyumbani (matumizi) sio mgogoro hata kidogo;
Ndugu zake wakiwa na matatizo nawasaidia kama kawaida;
Yeye akiwa na shida inakuwa shida yetu wote;
NIMPENDEJE?
mwanaume wa ukweli ni zaidi ya kuwa na mtoto wa kwanza sekondariKwa umri wa utambuzi, mimi ndo nimeishi naye miaka mingi zaidi ya m2 yeyote hapa duniani, ninaposema over 10 years yaweza kuwa hata 18/20; nieleweni; mnaonibeza kuwa mi ni mvulana nawashangaa sana tena sana. Just immagine mtoto wetu kwa kwanza yuko Secondary! Nashukuru kwa ushauri wako.
Kila tukiwa na mtafaruku na mama watoto wangu ananambia kauli hii "Nitawapisha wengine waje wajaribu, nina kwetu" Hivi mwanamke aliyeolewa, yuko ndani ya ndoa zaidi ya miaka 10 anaweza kuendeleaje kufikiria kurudi kwao badala ya kufikiria kujenga mji wake ambao unaweza kuwa kimbilio kwa jamaa zake wanaoweza kuwa na matatizo?
Akili au matope??????
KAULI HII INANIKERA SANA!
Ulikuwa wapi m2 wangu? nashukuru sana kwa ushauri wako; ila naamini mengi kati ya uloyataja najituma mkuu.Tutor B hapo ndipo unapofanya kosa kudhani kuwa mwanamke anahitaji hayo tuu usafiri, chakula, mahitaji yake ya kawaida ambayo wanakuambia hata kwao yapo na angeweza kuyapata hata akiwa kwao
Suala kubwa ni ile nyama ya ulimi wenyewe wanasema unaongea nae vipi unamtreat vipi, unamhandle vipi mkeo katika suala zima la upendo na mahitaji yake kama mwanamke, unamlinda, unamjali, sio kimwili zaidi kwenye nguo na mavitu kama hayo ila kiupendo kama mke, unamsikiliza hata kama sometime anaongea mambo yanakukera humkatizi maongezi yake, uko tayari kuwa nae hata mbele ya marafiki zao uko proud kuwa nae yaani ni vitu vidogo vidogo sana ila most important kwake
Kwenye kuwapenda sijui wamaanisha nini?
Nilim-aproach;
Nikatoa mahali;
Nikafunga naye ndoa;
Nikaanza kuishi naye tukiwa tunapanga;
Tumekaa na kushauliaana hadi tukajenga nyumba (sio mojatu);
Usafiri upo; na si kwamba nautumia mimi mara kwa mara;
Kwa ujumla mambo ya nyumbani (matumizi) sio mgogoro hata kidogo;
Ndugu zake wakiwa na matatizo nawasaidia kama kawaida;
Yeye akiwa na shida inakuwa shida yetu wote;
NIMPENDEJE?
FirstLady1 huyu hana hawara wala sijui pombe labda!tatizo lake KIBRI!MWANAUME ANARINGA NA KUJISIKIA KA HAENDI CHOO HUYU!KHA!Tutor B hebu jichunguze labda una makero yanayopita mipaka
Maana kauli zingine ni ngumu kutoka mdomoni...nashindwa kuelewa kwanini kila mnapogombana akwambie hivo
Inawezekana umejaza vinyumba ndogo na wife anajua
Inawezekana kila siku ukirudi home umelewa tilalila usiku wa manane ..
Ni vizuri kumweleza ukweli kuwa lengo lako la kuoana nae ni kuishi pamoja mpaka pale kifo kitakapowatenganisha (au kutenganishwa na uzinzi). Sasa kama objectives zake zimekuwa achieved ni vizuri kumwambia ajisikie huru ashuke kwenye gari safari iendelee.......! Tatizo kubwa ni kuwa wengi huwa wanasema hivyo akijua kuwa kiuhalisia hatua hiyo haitafikia. Kwa hivyo ndugu usichoke kama vile ng'ombe asivyoelemewa na nundu yake.
Kwanini usijisimamie mwenyewe kuipinga kauli hiyo mpaka uombe na wengine?