Kauli hii inanikera, nifanyeje?

Kauli hii inanikera, nifanyeje?

Hujaona hapo nimemwambia sikubali apite bila kupingwa? Na nimemwambia awaombe radhi wanawake? Hao wengine nimewaita ili maandamano ya kupinga hiyo kauli yasikike zaidi na yawe na nguvu.
sawa mshindi wewe ila msimpeleke beijing akikataa kufuta kauli
 
Nkusa nilimaanisha JAMBO,kwa mtu ambaye kaenda shule anaelewa kuwa wakati unaandika unaweza kukosea lakini maana ya sentesi inabaki kuwa pale pale.
Mkuu inaonekana unapo type, kidole chako hupenda sana kwenda kushoto ===="N" badala ya "M" na "I" badala ya "O"
Au keyboard layout yako ni ya Japan standard
 
Fikiria kesi ndogo kama hii;
Amechelewa kurudi nyumbani; anakukuta uko nje; unamuuliza mbona umechelewa hivi ulikuwa wapi?
Jibu; Eh! Baba fulani nisiongee ma marafiki zangu eti kisa nitaulizwa? kama ni hivyo ni bora nikupishe waje wengine wajaribu
Dah! pole ndg yangu kama ndo hivyo bas kumbe unaroho ngumu,Mimi binafsi nisingeweza vumilia hata kidogo bora asepe huko kwao anapopataka kila mara!! Hongera umemvumilia sana
 
inabidi siku akisema nipishe wewe unachukua mabegi ake unamwekea nguo zake unampakiza kwenye ndinga unamwambia twende nikupeleke huko kwenu..kwan wewe mwenyewe hauna kwenu..anatingisha kiberiti huyo aisee
 
inabidi siku akisema nipishe wewe unachukua mabegi ake unamwekea nguo zake unampakiza kwenye ndinga unamwambia twende nikupeleke huko kwenu..kwan wewe mwenyewe hauna kwenu..anatingisha kiberiti huyo aisee

Kwetu ninako; lakini kwa kuwa nimeishapata kwangu sipaswi kuendelea kuhusudu kwetu; m2 na chake ndo maana namshangaa mwenzangu kutothamini kwake na kuendelea kuhusudu kwao! Ila ... mamo yanaelekea kueleweka.
 
Mkuu.@Tutor mvumilie ndio kauli za wanawake kauli zao kubwa hiyo pia mojawapo nipe Talaka yangu neende kwetu nimeshachoka kuishi na wewe anakutisha wala usibabaike mvumilie tu yatakwisha hayo kaka.

Tatizo ni kuisha na kujirudia tena mkuu!
 
Kama sababu ya huo ugomvi haihusiani na wewe kutembea nje au kutoitimizia familia mahitaji ya msingi
Waje kujaribu kwani kwako ni testing ground?
Uyo kuna mtu anamtia icho kiburi usikute anakatwa na kuhongwa mpige chini na ilo buzi lazima litampiga chini mwisho wa siku shida zikimzidi atarudi
Au usikute anatikisa kiberiti tuu

Umeona eh!
Wasiwasi wangu ndo huo mkuu!
 
mkuu Tutor B nipo mtu wangu
nilikuwa nawasoma akina snowhite, Blaki Womani na wengineo wenye kujua masuala ya ndoa na nione wanasemaje kwanza
Sio uone kama vile unafanya ila fanya mpaka ufikie kiwango chako na kamwe usimuulize au kumwambia mwanamke eti umekosa nini kwangu kama chakula nakupa na mavazi na malazi sijui na usafiri
hayo ni ya ziada wala sio ya muhimu kwake
Muhimu sana kwake ni wewe na unavyomhandle na kumjali na kumpa maneno mazuri na sifa za hapa na pale za kila siku
The way unavyoongea nae hata unapojua kwamba hapa kachemsha ila humuonyeshi kuwa kachemsha unamsifia hata pale ambapo unaona kwamba ni wrong
Nyama ya ulimi mkuu na maneno mazuri na zaidi usimlinganishe wala kumfananisha na mwanamke yeyote mliyewahi kukutana nae

Thankx Mr. Rocky! nimekusoma
 
kujisimamia na kuwa na dharau ni vitu viwili tofauti...........

Na unaposema tatizo dogo, dogo kwa nani kwake au kwako?
Mpaka kuita wasimamizi maana yake alishakuonya mara kadhaa hukusikia....
- hilo nalo ni tatizo inaelekea hujali hisia za mkeo na humsikilizi, ukifanya maamuzi humsikilizi, mkeo sio jiwe kwamba afate utakzcho,ni binadamu, ana akili timamu na uwezo wa kufanya maamuzi... Ndoa ni kusikilizana....... Huwezi dharau mwenzio kwa kisingizio cha 'kijisimamia',watu wanajisimamia na wenza wao wanawasikiliza....

Unasema uliwatimua waimamizi wa ndo walipofika, je ndo adabu hiyo?
+hilo nalo ni tatizo, ulipaswa uwaombe radhi kwa usumbufu, na kuwaeleza wawape muda mlishughulikie tatizo lililopo kwanza....then mkacheka, mkala, mkanywa na siku kupita....

KWA HAYA ULIYOYAOYAANDIKA......
KISHA PITIA MAJIBU YAKO KWENYE THREAD HII
UTAJITAMBUA WEWE NI MWANAUME WA AINA GANI
KINACHOMFANYA MKEO AKUJIBU ANAYOKUJIBU KIPO HATA KWENYE THREAD YAKO...

Pitia comments zako utapata jibu

Haya nimekusoma; natafakari la kufanya ila umenihukumu ndivyo sivyo!
 
Huu ndio ukweli, kila mmoja amemkinai mwenzie hivo hawapo tayari kukaa chini kurekebisha tofauti zao.
Na yawezekana kuna mmoja kati yao ni mmbabe, hayupo tayari kumsikiliza mwenzie, atakachosema yeye ndio amri.

Sijamkinai mama watoto wangu, sitegemei kumkinai hata siku 1!
 
Huyu wala asitupotezee muda wetu, anakipata anachokistahili..... Unawezaje kupanda bangi ukategemea kuvuna chai?

Wacha wenye ushauri washauri, kama huna muda endelea na suruba za boss wako! tuliojiajiri ndo tuna muda wa kutumia kushauriana mambo mbali mbali! We mtumwa muda utautoa wapi?
 
ingefaa kama hutojali kwa kifupi......... wengi tulikuwa tunataka kujua kauli yake ilikuwa na maana gani

kwa ufupi ni kwamba kuna wifi yake (dada yangu) ndo anam-feed maneno mabovu;
Eti sio chaguo la familia, ni kwa kuwa baba alikuwa ameishatoa kishika uchumba kwa binti mwingine kijijini; nikachomoa na kuoa chaguo langu na kufanya shughuli zote za utoaji mahali mimi mwenyewe!
 
Tutor B umetia aibu sana.

Mwanamke ni kioo cha mwanaume, nikiona na mkeo kabla ya kuonana na wewe nitaweza kujua wewe ni mtu wa namna gani. Tukimwangalia mkeo tunaweza kupata taswira yako kwake, ni juu yako kuifanya hiyo taswira kuwa njema au la!!

Kwa mfano maelezo haya tayari nimeshajua tabia yako na huyo mke wako anajutia sana kuishi na wewe hiyo ndoa na watoto ndio vinavyomkwaza la sivyo angesha kuacha.

Jaribu kubadilika na yeye atabadilika na utashangaa mwenyewe, ubabe haulipi.

Distazo; nime e-mail yako nikutumie picha yake umuone; then nitakuelekeza ni video gani unaweza kumuona akiwa on action, then utanambia mimi ni m2 wa namna gani - wala usisumbuke kumuona.
 
Back
Top Bottom