Si kihivyo; ila kama inawezekana itoe in general;
kukua sio umri kakangu ni uzoefu na busara jinsi ya kuishi na watu!
kwanza pole na yote!ndo ukubwa huo!
nimekuuliza maswali yangu kama sita hizi kwenye post imepita
1.wewe na mkeo mna mawasiliano ya aina gani?
2.unamsikiliza kihisia,yani unaweza kumuelewa hata kabla hajaongea kitu?
3.mkeo anajivunia wewe kuwa mume wake?
4.wewa unafahamu thamani ya ndoa,mke na familia?
5.unatimiza wajibu wako kama mume(hii ni zaidi ya kuwa baba yani kuwa na uwezo wa kuleta watoto duniani)
6.mna nafasi ya kusali na mkeo pamoja?
7.mkeo ana fahamu hili linakukera kiasi gani?ulishawahi kumwambia na kumuonyesha kuwa hupendi?
8.mkeo anajua nafasi yake yeye kama mwanamke kwenye akili yako?
9.wewe unajua mapungufu yako kama mume na kama mwanaume?(hivi ni vitu viwili tofauti)
10.value ndoa yako katika makundi yafutayo
A)NI NZURI NAITHAMINI NA NI MIMI KATIKA UKAMILIFU WANGU
B)YA KAWAIDA NAKUBALI CHANGAMOTO
C)SI MUHIMU NAWEZA KUISHI MWENYEWE