Katuni: Bunge letu na dhihaka toka Kenya

Katuni: Bunge letu na dhihaka toka Kenya

JOY.JPG

HII YOTE NI KUTOKANA NA BUNGE LETU KUPOTEZA MWELEKEO NA KUWA KAMA KIJIWE CHA WAHUNI AMBAO HAWAJUI WAMEKWENDA KUFANYA NINI MJENGONI .....................lol

Huyu mtu yuko creative sana! Hapa ndipo Makinda na Ndugai walipoufikisha Tanzania kimataifa. Muangalie serukamba anavyo kojoa bungeni ila yuko sawa. Wanaotetea haki na kanuni wanatolewa nje na kupigwa ban five dsys. Maamuzi ya kilevi.
Shame to Ccm
 
idadi ni kubwa ya wabunge bungeni ila wameshindwa kutatua matatizo ya watanzania, maslai kwanza tanzania baadae ndio kaulimbiu yao.
 
Robert mwampembwa yupo juu kama povu la beer! Kanifurahisha sana! This is exactly the definition of tanzanians horrible parliament!
 
Mimi naona kama hii picha imekwenda mbali sana na uhalisia...naona watanzania tumetukanwa.
Hizo nguo zilizoanikwa yamaanisha Wabunge wetu wanajuana mpaka nguo zao za ndani,nani anavaa chupi gani na nani anavaa kitu gani.maana mule kuna wamama na vijana wao pamoja na wababa na mabinti zao.
Japo sikatai kuwa hayo mengine kweli yapo.Ila hii ni dhihaka sana kwa watanzania na serikali yetu...nasisi pia tunaweza kuchora zaidi yao kwani majanga ya kuchorwa na wao pia wanayo.
 
Aliyechora hii katuni ni Mbongo, tena Mnyakyusa wa Mbeya.

Jadili hoja ya katuni na si kugeuza mada tuanze kujadili ni nani kachora. Tukianza kujadili nani aliyechora, basi kwa nini isiwe ni wewe au baba yako.

Na kama nimechora mimi so what, unataka nini baada ya kunijua ni mimi.

Peleka upuuzi wako kunakoshahili.
 
Haya yote tumeyataka wenyewe aisee, tuwe wapole kama hatuko tayari kubadili hali ya hewa. Wala tusihangaike kumtafuta mchawi
 
inaonesha jinsi wabunge wa CHADEMA wasivyo na nidhamu ndio maana spika anawatoa sana nje
Huyo anaye mkojolea spika ni wa chama tawala na hakupewa adhabu coz alikuwa sahihi.
 
jinsi gani watanzania 2livyo na mawazo finyu. mi sioni umuhimu wa wabunge kwani wakuu wa mikoa na wilaya hawawezi kusikiliza shida za wananchi na wakazitatua? laiti ningekalia kiti cha rais sidhani kama kungekuwa na bunge tanzania.
 
Ukiangalia document zote zimetupwa. Maana yake nini? hakuna anayesoma kwani huwa wanasubiri Spika aulize "Je, kifungu hiki kimeafikiwa" na wao wanajibu "Ndiyooooo".

Inanikumbusha makala moja ya Freeman Mbowe mwaka 2004.
 
Jamaa alivyomchola serukamba ndo kaua kabisa aisee!!!!!!!

the best mchoro kabisaa! wabunge wanao kubali kufuta matokeo eti ya me kosewa yafanyiwe standardaization, wbunge wanao pitisha bajeti kwa ku sema tu Ndioooooo, au siooooooo katika karne hii ya 21 wanachukua laki tatu zao per day wana sepa, wabunge wanao jibu hoja zinazo jenga maisha ya watanzania kwa mipasho ka waimba taarbu stejini! they deserve it shame on them na sisi wa tanzania kwa ku select such representatives
 
Ukiangalia document zote zimetupwa.

Maana yake nini? hakuna anayesoma kwani huwa wanasubiri Spika aulize "Je, kifungu hiki kimeafikiwa" na wao wanajibu "Ndiyooooo".

Inanikumbusha makala moja ya Freeman Mbowe mwaka 2004.
 
Inamaana boxer na bikini zinaanikwa katika bunge letu tukutu la jamhuri ya muungano wa tanzania??
 
Katuni imechorwa kwa utaalamu ambao wengi sijui kama mmegundua. Unajua upande wa kulia wa Spika huwa wanakaa mawaziri na nyuma yao ni wabunge wa CCM.

Upande wa upinzani unakaa upande wa kushoto mwa Spika yaani Mbowe, Tundu Lissu na wenzake.

Sasa ukiangalia picha utaona watu wote wenye vituko wako upande wa Serikali. Upande wa upinzane hakuonekana hata mmoja sanasana mikono miwili inabishana na desk la katibu wa bunge.

Hivyo, mimi sina wasiwasi kabisa kwamba katuni hii inaichamba Serikali moja kwa moja. Upinzani haujaguswa hata kidogo.
 
Back
Top Bottom