Izato
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 5,162
- 11,128
Kuna wanawake wengi bungeni, lakini wingi wao hauwafanyi kuwa na sauti wala mamlaka juu ya maamuzi yenye tija katika mambo ya msingi yanayolikabili Taifa letu.
Kwa muktadha huo "tokenism" katika muhimili huu muhimu wenye jukumu kubwa la kuishauri na kuisimamia serikali inahusishwa na jinsi ambavyo wanateuliwa kimkakati kwa ajili ya kuonekana tuna Bunge lenye usawa wa kijinsia, na wala si kwa sababu ya kuwapa mamlaka halisi ya kutaka kubadilisha mambo muhimu yahusuyo jinsia, kisera, na utawala bora.
Tanzania inatumia mfumo wa Viti Maalum kwa wanawake hivyo basi 30% ya wabunge wanatoka katika kundi hili
Wabunge hawa hawana jimbo la kuwajibika nalo moja kwa moja, hivyo teuzi zao hupitia katika michakato ya ndani ya vyama vyao. Teuzi zao hutolewa kama "token" tu kwao kupitia ushindani dhaifu ndani ya chama husika. Hii inapunguza hadhi yao ya kisiasa na kuwafanya waonekana ni dhaifu zaidi ya wale wanaipitia mchakato mgumu wenye ushindani mkali majimboni mwao dhidi ya wagombea wengine wa vyama shindani.
Wabunge wengi wa Viti Maalum hawapewi fursa ya kushiriki katika kamati nyeti wala hawapewi nafasi za uongozi wa juu katika kamati hizo. Kwa kuwa wanachukuliwa kama wapambaji wa picha ya bunge, na wala siyo wabunge wenye uzito wa kimaamuzi ndani ya Bunge
Ndiyo! Kuna wabunge wanawake wengi ndani ya Bunge la Jamuhiri ya Muungano wa Tanzania, lakini mjadala wa "tokenism" unajitokeza hasa pale tunaposhuhudia idadi hiyo haileti mabadiliko ya kimamlaka na kisera. Wapo wachache wenye ushawishi mkubwa, lakini waliokuwa wengi wapo kwa ajili ya kujazia namba tu.
Kwa muktadha huo "tokenism" katika muhimili huu muhimu wenye jukumu kubwa la kuishauri na kuisimamia serikali inahusishwa na jinsi ambavyo wanateuliwa kimkakati kwa ajili ya kuonekana tuna Bunge lenye usawa wa kijinsia, na wala si kwa sababu ya kuwapa mamlaka halisi ya kutaka kubadilisha mambo muhimu yahusuyo jinsia, kisera, na utawala bora.
Tanzania inatumia mfumo wa Viti Maalum kwa wanawake hivyo basi 30% ya wabunge wanatoka katika kundi hili
Wabunge hawa hawana jimbo la kuwajibika nalo moja kwa moja, hivyo teuzi zao hupitia katika michakato ya ndani ya vyama vyao. Teuzi zao hutolewa kama "token" tu kwao kupitia ushindani dhaifu ndani ya chama husika. Hii inapunguza hadhi yao ya kisiasa na kuwafanya waonekana ni dhaifu zaidi ya wale wanaipitia mchakato mgumu wenye ushindani mkali majimboni mwao dhidi ya wagombea wengine wa vyama shindani.
Wabunge wengi wa Viti Maalum hawapewi fursa ya kushiriki katika kamati nyeti wala hawapewi nafasi za uongozi wa juu katika kamati hizo. Kwa kuwa wanachukuliwa kama wapambaji wa picha ya bunge, na wala siyo wabunge wenye uzito wa kimaamuzi ndani ya Bunge
Ndiyo! Kuna wabunge wanawake wengi ndani ya Bunge la Jamuhiri ya Muungano wa Tanzania, lakini mjadala wa "tokenism" unajitokeza hasa pale tunaposhuhudia idadi hiyo haileti mabadiliko ya kimamlaka na kisera. Wapo wachache wenye ushawishi mkubwa, lakini waliokuwa wengi wapo kwa ajili ya kujazia namba tu.