Katu usimkekete binti yako...

Katu usimkekete binti yako...

Kwangu ni kitu cha kawaida kwakuwa nimekulia mazingira inakofanyika lakini hakuna sehemu niliyosema naunga mkono. Hii ni mila ya baadhi ya makabila hapa nchini hivyo kwabaadhi ya mabinti hufikia hatua ya kutoroka na kwenda kufanyiwa au wengine huomba wenyewe wafanyiwe.

Tofauti ya zamani na sasa ni kwamba zamani binti alikatwa na sehemu ya kisimi kuondolewa, lakini siku hizi ni kuchanjwa tu hii huitwa kiccm (enzi za mzee wa msoga na ufisadi iliomekana jambo lolote la maana linaweza kufanywa kizembe na kusiwe na shida).

Ilikuwa nadra sana baada ya binti kukeketwa umkute anacheza ngoma ya asili (litungu) tena mchana wa jua kali kwani damu huvuja sana lakini kwasasa wanaume ndio hufanyiwa tohara asubuhi na mapema ili kabla ya jua kuwa kali wawe kivulini (nyumbani) ilhali kwa mabinti hufanyiwa kuanzia saa nne hadi mchana kulingana na idadi na eneo tukio linapofanyika.

Naomba nihitimishe kwakusema kuwa kwasasa madhara ya ukeketaji katika uhalisia wake ni madogo sana kuliko inavyoelezwa kwa vyombo vya habari. Kama nasema uongo nawaruhusu watafiti waingie kazini. Mchukue mwanamke aliyefanyiwa ukrketaji kuanzia 2000 kurudi nyumba na aliyefanyiwa kuanzia 2002 kuendelea kisha linganisha maumbile yao kwa kuzingatia mikato ya kisimi. Utagundua kabisa sikuhizi ni kama mabinti huenda eneo la tukio kutimiza mila na desturi na sio kukatwa sehemu zao. Zamani mwanamke anakaa ndani hata miezi miwili akiuguza kidonda wakati kwasasa baada ya wiki moja tu mabinti huanza kubananishwa uchochoroni au magetoni kwa wanaume.

Nimeandika matusi wanajf mnisamehe, kuna maneno ambayo nimelazimika kuyatumia ili nieleweke. Sio kwamba nafurahia lakini huo ndio uhalisia hasa kwa mila za kwetu wakurya (hasa wanyamongo) ila kwa koo zingine sina uelewa nako kwakuwa koo ya wanyamongo na watimbalu (wakira kwa mbali) huwa na tamaduni zinazoingiliana na hata maeneo yao yameendelea kidogo hii huwafanya kutotumia nguvu sana kwenye tohara.

Kwakuchomekea tu. Zamani kijana ili aonekane jasiri na ametimiza mila ilikuwa lazima atahiriwe kimila, wale waliotahitiwa hospitali ilifika mahali wakawa wanatengwa ama kutukanwa na wenzao wa rika sawa (saiga) na ilip3leka baadhi kurudiwa upya kutahiriwa na wazee. lakini siku hizi ni ngumu kukuta haya yakifanyika isipokuwa kwa kutaniana tu na ukimtukana mwenzako kwakuwa tu alitahiriwa hospitali utajuta.

You are very wrong...
i nearly lost best friend during derivery, she nearly lost her her two sisters, she was dumped by lover kwa huu upuuzi and her life is not stable for eversince ukiutetea huu upuuzi nashindwa kukuweka kundi gani...mbali na kujitoa sana ktk majeshi wakurya ni jamii ya hovyo sana kuwai kutokea hapa tanganyika
 
Aisee!! Nisiseme sana. Mpaka stationary ilipotolewa hii kadi napafahamu.

unaweza kuwasaidia polisi kwa siri. polisi walioko humu kadi ina jina na namba za simu please act upon hizi mila potofu zinatakiwa kuisha
 
Swala la ukeketaji hata wamisionari walisalimu amri. Walishindwa kulitokomeza kabisa.

Kuna mengi sana nyuma ya ukeketaji. Ni ukatili kweli, ila utashangaa wakina mama pia wanataka ukeketaji uendelee. Katika baadhi ya makabila niliyotembelea kuhusu hili swala, wakina baba wakotayari kuachana nalo kuliko wakina mama. Ukiangalia ukeketaji kama mila, kiimani, kiuchumi na ngazi ya kimamlaka kwenye jamii, utaona mengi.

Kule Dodoma kuna makabila yanaamini usipomkeketa mtoto kabla hajafikisha umri wa miaka mitano atakufa kwa ugonjwa wa lawalawa. Na kuna wanaotoa ushuhuda kabisa. Lazima kuna sababu nyingine ila niimani yao. Mpaka nikajiuliza kama kuna tafiti za kisayansi zimefanyika kwenye hili ila sijakutana nazo bado, kama zipo.

Ndani ya miaka zaidi ya miwili nimekuwa nikifuatilia hili swala kwa Tanzania, nimejifunza mengi. Ila mwisho wa siku lina madhara makubwa sana ya kimwili na kisaikolojia pia.
jamii, itikadi, dini, mawazo au mtu anayetetea fgm kwa sababu yyte ile ni wakupingwa na kila mtu
 
unaweza kuwasaidia polisi kwa siri. polisi walioko humu kadi ina jina na namba za simu please act upon hizi mila potofu zinatakiwa kuisha
mkuu hili jambo sio siri. Kadi kama hizo husambazwa na hao mabinti hupita barabara kuu
 
jamii, itikadi, dini, mawazo au mtu anayetetea fgm kwa sababu yyte ile ni wakupingwa na kila mtu
Kuna wakati inabidi uelewe kwa nini mwenzako anamtazamo tofauti. Ukishaelewa upande wake, ni rahisi kufahamu jinsi utakavyomvuta akubaliane na mtazamo wako.
 
Faida yake ni nini mkuu mbona hamzitaji hizo faida?
Suala la binti kutahiriwa ni jambo jema na lenye kufaa, ila siyo lazima na lina faida kubwa sana kwao.

Tatizo hawa wetu wanafyeka kabisa kitu ambacho si sawa. Ama kuhusu kupata raha hao walio fyekwa wanapata raha tena sana (Hili halina shaka kabisa).

Ahsanteni.
 
Mkuu hiyo namba 4 wanapomshona uke akienda chooni atakojoa vipi?
View attachment 1646303
Kuna aina nne za ukeketaji
1. Wanaoondoa kisimi pekee (kuna baadhi ya makabila ya Dodoma ambayo hutumia hii)
2. Wanaoondoa kisimi na labia ndogo (baadhi ya makabila ya kaskazini - Mara, Arusha, Manyara)
3. Wanaoondoa kisimi, labia kubwa na ndogo
4. Wanaoondoa kisimi, labia kubwa na ndogo, kisha kushona uke. (Haya zaidi ni makabila ya Somalia na Ethiopia)

Aina zote hizi zina madhara mbalimbali na kwa viwango tofauti. Hiyo ya nne, uke hufunguliwa pindi utakapofanya tendo la ndoa kwa mara ya kwanza na mumewe. Ukiwa na mume katili, anaruhusiwa kushona tena akienda safari ambayo atakaa muda mrefu.
 
Tanzania bado tuna Safari ndefu Yani mtu kuharibiwa viungo vyako unaona heshima but wanaoamini hayo mambo wako huko kijijini na hawasafiri Ila wanaokuja huku mjini wanapata saikolojiko effects wallah, uchi tu wenyewe unatisha sasa ukikatwa hvo vya ndani ni shida
Eti uchi unatisha,kumbe hata nyinyi wenyewe huwa mnajiogopa mkiangalia?
 
Hiyo ya kukata kidogo nayo ina faida gani
Hakuna nilipo tetea mila yoyote.

Watu wa mila wao wana kosea ila jambo la kutahiri wanawake lipo ila inakatwa sehemu ndogo sana kwa lengo maalumu siyo hawa wanao kata kabisa.
 
kuhusu waarabu sio kweli
Asilimia kubwa ya wanawake wa Kiarab wanakatwa visimi kwa sababu ni jadi yao.
"Data collected in 2015 from household surveys show female genital mutilation exists in Yemen, Iraq, and Indonesia and in some places in South America such as Colombia, India, Malaysia, Oman, Saudi Arabia, and the United Arab Emirates. The practice is also found in pockets of Europe and in Australia and North America."

Note: Australia na Marekani si wazungu wafanyao hivyo bali ni wakimbizi wa Kiislam (Waarab) waishio huko ndiyo wanafanya huo unyama kwa ajili ya imani ya dini yao. wazungu wa Ulaya wanaokatwa visimi ni wale wazungu waislam wa nchi kama Bosnia, Romania, Albania, nakadhalika.

Source: www.dw.com/eng
 
Back
Top Bottom