View attachment 1646303
Kuna aina nne za ukeketaji
1. Wanaoondoa kisimi pekee (kuna baadhi ya makabila ya Dodoma ambayo hutumia hii)
2. Wanaoondoa kisimi na labia ndogo (baadhi ya makabila ya kaskazini - Mara, Arusha, Manyara)
3. Wanaoondoa kisimi, labia kubwa na ndogo
4. Wanaoondoa kisimi, labia kubwa na ndogo, kisha kushona uke. (Haya zaidi ni makabila ya Somalia na Ethiopia)
Aina zote hizi zina madhara mbalimbali na kwa viwango tofauti. Hiyo ya nne, uke hufunguliwa pindi utakapofanya tendo la ndoa kwa mara ya kwanza na mumewe. Ukiwa na mume katili, anaruhusiwa kushona tena akienda safari ambayo atakaa muda mrefu.