Katu usimkekete binti yako...

Katu usimkekete binti yako...

Eeeeeh... Nawewe unatetea mila za kipuuzi namna hii
Hakuna nilipo tetea mila yoyote.

Watu wa mila wao wana kosea ila jambo la kutahiri wanawake lipo ila inakatwa sehemu ndogo sana kwa lengo maalumu siyo hawa wanao kata kabisa.
 
Sio kila mtu anaandaliwa kwa kusuguliwa kisimi....mwingine ukimgusa njia ya haja kubwa anawika kama kuku na ndo raha yake. Analowa vizuri na kuwa tayari kwa tendo
Eeeeeh.....
 
Hakuna nilipo tetea mila yoyote.

Watu wa mila wao wana kosea ila jambo la kutahiri wanawake lipo ila inakatwa sehemu ndogo sana kwa lengo maalumu siyo hawa wanao kata kabisa.
Lengo maalumu lipi...Hebu nifananulie
 
Ujinga ni janga Sana kwa taifa hili nadhani huo ukeketaji umekaa kishirikina flani hivi Kama matambiko ya kikoo na kikabila na swala Hilo ni zaidi ya tujuavyo. Watanzania ni wagumu wa mabadiliko Kuna marafiki wametoka tarime na ni wasomi Ila wanashabikia huo ujinga
Hata kwenye uzi huu, kinachozungumziwa zaidi ni "tendo la ndoa" linavyoathiriwa na ukeketaji, kwasababu linamgusa mwanaume. Maumivu anayopata mwanamke wakati wa ukeketaji, uwezekano wa kupata maambukizi ya magonjwa au hata kuharibu njia ya mkojo na uzazi, hatari anayopata kipindi cha kujifungua - kwa maana lile kovu linazuia njia kufunguka vizuri, au madhara ya kisaikolojia..hayo ni nadra kusikia yakizungumziwa.

Tujitahidi pale tunapoweza na kuhitajika kutoa elimu na kukemea, tufanye hivyo.
 
Tanzania bado tuna Safari ndefu Yani mtu kuharibiwa viungo vyako unaona heshima but wanaoamini hayo mambo wako huko kijijini na hawasafiri Ila wanaokuja huku mjini wanapata saikolojiko effects wallah, uchi tu wenyewe unatisha sasa ukikatwa hvo vya ndani ni shida
Kule juu nimeandika, wengi wanaelezea kwakuongeza uongo mwingi sana kuliko uhalisia. Fanyeni tafiti muone, uliyemquote pia ameeleza kitu kinachofanana na mimi. Fanyeni tafiti za tohara za miaka ya nyuma kwa watoto wa kike na tohara za sasa.

Na hii ni moja kati ya faida ya elimu iliyotolewa. Tukianza kupaza sauti kuelezea uongo nadhani madhara yatakuwa makubwa zaidi (tutaharibu saikolojia kwa binti na ngariba nao wataona hawaaminiki) kuliko faida. Bahati nzuri baadhi ya mabinti waliokeketwa miaka ya karibuni (2014/2015_2018/2019) wako mashuleni/vyuoni, anzeni tafiti na hao. Waambieni habari za "mnaharibiwa" kisha muone kama hata watashtuka. Wengi wa wanawake wanaopaza sauti ni wale ambao wamenusurika kufanyiwa kwa lazima au wale waliofanyiwa miaka ya zamani wakati inafanyika ile yenyewe na ndio maana chumvi inazidi.

Sikatai kuwa tohara ina madhara makubwa kisaikolojia kuliko kiafya, lakini binti wa sasa aliyefanyiwa tohara ni ngumu kumtofautisha na binti ambaye hajafanyiwa. Naongea kama mwanaume niliyelelewa katika mazingira husika na nilichoandika nimekishuhudia kwa macho yangu na sio kusimuliwa.
 
Ukeketaji ni uonevu, usilipambe lionekane la kawaida,hata kama umetoka huko..
Kama umeona kupamba badala ya nilichoandika, ni haki yako kuamini kile unachoona ni sahihi. Hv kwenye huu uzi naonekana kama ngariba au mumewe ee? maana najitahidi kueleza uhalisia wa hili suala lakini naonekana kama nafaidi. Serikali na nguvu zake zote imebidi wakae meza moja na wazee wa kimila (muulize Glorias Luoga aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Tarime) ili yazungumzike na elimu kwa ngariba asifanye ya kufanya lakini kuna mtu hapa jf akiwa nyuma ya keyboard anfikiri ni rahisi kumaliza hili janga.

Kuna mabinti wanalazimisha wafanyiwe
Wengi hufanyiwa akishamaliza drs VII maana inaaminika ameshakuwa
Wazee wa kimila ndio walioelimishwa wakaacha kutumia ukale
Wapiga kelele ni wale ambao hawajui hata tohara inafanyikaje wamekaririshwa kinaondolewa kisimi
Ikitumika nguvu ndio kwaanza picha litaanza
Maeneo ambako nguvu haitumiki kuna mabinti waliokataa na wanaolewa
Maeneo nguvu zinakotumika mabinti wanakeketwa kwalazima tena usiku na hapo ngariba hupangusa haswaa.

Tupingane kwa hoja na sio kurushiana madongo, hakuna jambo lenye hasara pekee. Kama lipo mniambie.
 
Kitu ambacho hujui ni kwamba katika hizi jamii zenye mila za kukeketa mabinti wenyewe wanapenda na huwa wanajipeleka kukeketwa hata kama mzazi wake alikua hataki hayo mambo.
Wachache sana wataongea kuhusu hili. Wengi wanakimbilia kulaumu zaidi.
 
Hata kwenye uzi huu, kinachozungumziwa zaidi ni "tendo la ndoa" linavyoathiriwa na ukeketaji, kwasababu linamgusa mwanaume. Maumivu anayopata mwanamke wakati wa ukeketaji, uwezekano wa kupata maambukizi ya magonjwa au hata kuharibu njia ya mkojo na uzazi, hatari anayopata kipindi cha kujifungua - kwa maana lile kovu linazuia njia kufunguka vizuri, au madhara ya kisaikolojia..hayo ni nadra kusikia yakizungumziwa.

Tujitahidi pale tunapoweza na kuhitajika kutoa elimu na kukemea, tufanye hivyo.

Nakujibu kwaujumla mkuu.

Anza kufanya tafiti mwaka huu maeneo ambako tohara zinafanyika kisha mwakani leta mrejesho uniambie ni asilimia ngapi ya mabinti waliokeketwa wamepatwa na madhara uliyoainisha hapo juu. Nimejaribu kueleza lakini ni kama hatueleweki. Kwataarifa yako tu. Hakuna kovu, hakuna maambukizi kwa kuwa kila mmoja anaenda na wembe yake na gloves yake na mazingira huwa safi, hakuna mwanmke aliyeshindwa kuzaa kisa tohara, hakuna madhara kisaikolojia kwa ukubwa unaoelezwa labda kwawale wanaofahamiana lakini ni rahisi binti aliyefanyiwa tohara kudanganya kuwa hajafanyiwa na ukamuamini kwakuwa haifanyiki vile mnavyowaza.
 
Kama umeona kupamba badala ya nilichoandika, ni haki yako kuamini kile unachoona ni sahihi. Hv kwenye huu uzi naonekana kama ngariba au mumewe ee? maana najitahidi kueleza uhalisia wa hili suala lakini naonekana kama nafaidi. Serikali na nguvu zake zote imebidi wakae meza moja na wazee wa kimila (muulize Glorias Luoga aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Tarime) ili yazungumzike na elimu kwa ngariba asifanye ya kufanya lakini kuna mtu hapa jf akiwa nyuma ya keyboard anfikiri ni rahisi kumaliza hili janga.

Kuna mabinti wanalazimisha wafanyiwe
Wengi hufanyiwa akishamaliza drs VII maana inaaminika ameshakuwa
Wazee wa kimila ndio walioelimishwa wakaacha kutumia ukale
Wapiga kelele ni wale ambao hawajui hata tohara inafanyikaje wamekaririshwa kinaondolewa kisimi
Ikitumika nguvu ndio kwaanza picha litaanza
Maeneo ambako nguvu haitumiki kuna mabinti waliokataa na wanaolewa
Maeneo nguvu zinakotumika mabinti wanakeketwa kwalazima tena usiku na hapo ngariba hupangusa haswaa.

Tupingane kwa hoja na sio kurushiana madongo, hakuna jambo lenye hasara pekee. Kama lipo mniambie.

Jambo lenye hasara pekee ni hilo la FGM ....
Tupo hapa duniani tuzae tuiepeleke DNA yetu foward..
Na kuzaa hakuji spontaneous,ni mbegu ya kike na kiume kukutana...
Kukutana kwa mbegu hizi ni lazima kuwe 'facilitated'....
Kila kitu kimekua 'crafted' vizuri ili 'facilitation' ifanyike na yai litungwe..
Sasa unaharibu kitu ambacho kiko 'crafted' ili tuendeleze kizazi?!?
Huoni kama unaenda nje ya malengo yetu ya kuwa hapa duniani?
Namaanisha,
Kumkeketa mtu ni kumpunguzia chance zake za kuipeleka DNA yake foward..
Kwa sababu kama haienjoy sex,it means chance zake za kuichagiza penis imwage mbegu kwake ni ndogo,..
Kwa hio no yai kutungwa
Huu ni unyama!
By the way sijamaanisha waliokeketwa hawashiki mimba,au hawawezi kuwa na familia, nisome kwa makini kwanza...
Second sio kwa vile kama jambo halijaweza kutokomezwa then tuone lina faida,
Hapana, hizo hizo efforts unazozi undermine,zina matokeo chanya,
Im sure RATE ya waliokeketwa miaka labda ya 1950's huko itakua ilikua kubwa and severly compared to now, sina figures but i just believe this...
 
Nakujibu kwaujumla mkuu.

Anza kufanya tafiti mwaka huu maeneo ambako tohara zinafanyika kisha mwakani leta mrejesho uniambie ni asilimia ngapi ya mabinti waliokeketwa wamepatwa na madhara uliyoainisha hapo juu. Nimejaribu kueleza lakini ni kama hatueleweki. Kwataarifa yako tu. Hakuna kovu, hakuna maambukizi kwa kuwa kila mmoja anaenda na wembe yake na gloves yake na mazingira huwa safi, hakuna mwanmke aliyeshindwa kuzaa kisa tohara, hakuna madhara kisaikolojia kwa ukubwa unaoelezwa labda kwawale wanaofahamiana lakini ni rahisi binti aliyefanyiwa tohara kudanganya kuwa hajafanyiwa na ukamuamini kwakuwa haifanyiki vile mnavyowaza.
Mnhhhh kwa hio siku hizi mnaenda na gloves zenu? makubwa haya....

Hapo nilipo bold,wacha kutuongopea basi,

Madhara ya kisaikolojia yapo, pale binti atakapokuwa hainnjoy tendo la ndoa, sio madhara yenyewe haya?? au hujui kuto enjoy tendo la ndoa kunaweza kusababisha visirani,na irritability, ugomvi ndani ya ndoa...worse, ni pale atakapokua rejected na wanaume...mkuu pinga FGM.
 
Mnhhhh kwa hio siku hizi mnaenda na gloves zenu? makubwa haya....

Hapo nilipo bold,wacha kutuongopea basi,

Madhara ya kisaikolojia yapo, pale binti atakapokuwa hainnjoy tendo la ndoa, sio madhara yenyewe haya?? au hujui kuto enjoy tendo la ndoa kunaweza kusababisha visirani,na irritability, ugomvi ndani ya ndoa...worse, ni pale atakapokua rejected na wanaume...mkuu pinga FGM.
Unalazimisha nikuelewe ilhali wewe hunielewi.

Nimesema "hakuna madhara kisaikolojia kwaukubwa unaoelezewa" na sio kwamba hakuna madhara. Hizo ni sentensi mbili zenye maana tofauti.
 
namaanisha, yale yote yaliyofanywa na serikali na wananchi wa kawaida katika vita ya kupinga ukeketaji yana matokeo chanya japokuwa yanaonekana kwa juu juu kama hayataweza hii vita, so usidharau effort zao,
 
Unalazimisha nikuelewe ilhali wewe hunielewi.

Nimesema "hakuna madhara kisaikolojia kwaukubwa unaoelezewa" na sio kwamba hakuna madhara. Hizo ni sentensi mbili zenye maana tofauti.

mnhhhh ...kwa nini unataka 'kulidogolesha' hili jambo?..madhara hata kama ni mmoja anaathirika still ni mtu...
 
namaanisha, yale yote yaliyofanywa na serikali na wananchi wa kawaida katika vita ya kupinga ukeketaji yana matokeo chanya japokuwa yanaonekana kwa juu juu kama hayataweza hii vita, so usidharau effort zao,
Unajaribu kunifanya nionekane mbaya. Mimi sijasema nadharau juhudi.
 
mnhhhh ...kwa nini unataka 'kulidogolesha' hili jambo?..madhara hata kama ni mmoja anaathirika still ni mtu...
"Kwaukubwa unaoelezwa." Kama hayo mengine hatuelewani, baki hapa na neno "unaoelezwa." Wasimuliaji wanalikuza zaidi kuliko uhalisia.
 
"Kwaukubwa unaoelezwa." Kama hayo mengine hatuelewani, baki hapa na neno "unaoelezwa." Wasimuliaji wanalikuza zaidi kuliko uhalisia.
MNHHHHHH.....lazima uwe na evidence ama figures kuonyesha linakuzwa,najua hutaonyesha,good night mkuu,
 
MNHHHHHH.....lazima uwe na evidence ama figures kuonyesha linakuzwa,najua hutaonyesha,good night mkuu,
Ni kweli sitaweza kuonesha lakini nimetoa ufafanuzi jinsi ya kupata ukweli halisi. Wewe ni mwanamke, tembelea mkoa wa mara mwezi huu kuna tohara unafanyika. Fika mpaka eneo inapofanyika halafu uone kama ulichokiandika (ukiachana na madhara ya kisaikolojia kwani hayaonekani siku hiyohiyo) na uhalisia vinaendana. Hasa kutoka damu, kuonfolewa baadhinya sehemu n.k
 
Kumkeketa mtoto wa kike ni kumtia ulemavu,
Chondechonde wazazi msiwatie ulemavu mabinti zenu kwa kuendekeza mila za kijinga.
 
Back
Top Bottom