Katika hili, namwamini Shetani

Kwanini Mungu aumbe mti wa utambuzi wa mema na mabaya na mti wa uzima na kuiweka bustanini,lengo lake lilikuwa ni nini? Kwani miti mingine haikuwa na matunda yakutosha kwa chakula hadi akaumba hiyo miti miwili?,si asingeiumba tu kama alijua italeta janga kati yake na wanadamu,akaacha Adam na Hawa waishi kwa kula matunda ya miti mingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NGOJA NIKARIBISHE WANAWAKE MAANA PALE EDEN ALIEWEZA KUONANA N KUONGEA NAE MAMBO MENGI KWA WAKATI ULE ALIKUW HAWA, NA SIJUI WALIONGE NIN NJE YA KULA TUNDA LILE, MAYBE TUTAANZA KUPATA UFUNUO WA MENGINE TUSIYOYAJUA KATI YA HAWA NA SHETANI.
 
Adam na Eva hawakufa?
Wako wapi leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo uyasemayo unayajua, umeambiwa au umesoma? Unless Kuwa unajua for sure la sivyo huna rights ya kuwashuhudia uwongo wayaminiayo na wayaishio wengine.
 
Huku ni kumfikiri mungu. Finity thinking of the infinity how is that possible?
 

Ok ni hiviiiiii Mungu sio shetani.Mungu hufunua jambo Kama anaona litaponya lakini Kama halitaponya anaweza asiamue kufunua kulingana Na anavyokuona wewe ukoje.Kwa mfano unaweza ukawa umeokoka Tena vizuri tu Na ukawa umepanga let's say apartment karibu Na mshirikina anaekuroga Na Mungu akakuepusha nae bila kukufunulia kuwa huyo mtu anahangaika kukuroga Ila aka hakikisha anakulinda Na Huyo mshirikina anaehangaika kukuroga hafanikiwi.Na ukawa Na mwingine umepanga nae jirani yako Mwenzio yeye Mungu akamfunulia kuwa huyo jirani yenu Ni mshirikina.Mungu hutuangalia kwanza Kama yafaaa wakat gani kutufunulia yote au kutufunulia baadhi ya mambo au wakati gani asitufunulie kabisa.Kweny huo mfano maybe Mungu ana kujua wwe mtumishi wake una hasira hutoweza ku control Na utatengeneza uadui unnecessarily Na huyo jirani yako hivyo Mungu anakuepushia Na huo mfarakano.so Mungu akaamua kukuepushia Hilo kwa kutokufunulia lakini akakulinda.Ila mwenzako sababu Mungu ameona anaweza ku handle Na kupambana naye kimya kimya Mungu akamfunulia yote.Lakini Kama utaenda Kwa mganga (mchawi) yeye atasema kila kitu haijalishi wewe ukitoka hapo utasababisha maafa Kwa huyo jirani yako anaekuroga au la.Sababu shetani huwa haangalii maafa Na actually ndo anayoyapenda.Ila Mungu hufunua Kwa lengo zuri Na ndo maana andiko linatuambia "unabii haukuwajia Ila Kwa kuponya.Sasa hii ndo ilitokea Eden.(Najibu swali lako sasa).Mungu alimwmbia Adam asile maana atakufa lakini hakusema kuwa ule mti akila atajua jema Na baya why ???Ni sababu alijua akiwaambia hivyo Kwa akili zao fupi Na tamaa zao wangetamani tu kulila Hilo tunda Kwa ajili ya kuupata huo ujuuzi wa jema Na baya bila kuwaza gharama ya huo ujuzi(hukumu).Na hivyo wangesukumwa kula Na mwishowe kufa.Lakini shetani aliamua kulifunua sababu yeye hufunua tu hata Kwa kuharibu Na alijua Kwa kuyasema hayo ambayo Mungu hakutaka kuyasema angewavutia Adam Na Eva kula kitu ambacho Mungu alijua ndo maana hakusema ndo mbeleni tukaona kuwa Kweli baada ya Eva kuambiwa Hilo la ujuzi basi tamaa ikamuingia akala tunda.Ili dhambi iwe dhambi.,lazima kuwa Na uwezo wa kutambua jema Na baya wewe mwenywe kitu ambacho awali Adam Na Eva hawa kuwa nacho.Yaani walikuwa Kama watoto wachanga hivyo Kwa kutokujua Kwao jema Na baya wangeishi bila kuwa Na hatia yoyote Mbele za Mungu maana walikuwa hawajui lolote Na Mungu alitaka waishi hivyo sababu ha kutaka kuwatia hatiani.(Tunajua hata mahakama ikutie hatiani lazima kuwepo na ujuzi wa mema Na mabaya kwa mtenda kosa ndo maana kichaa hahukumiwi au hata mtoto mchanga akiua hahukumiwi)Ndo maana aliwazuia wasile ili wasije kuingia hatiani endapo wakifanya kitu lakini Kwa kutokutii kwao wakala na wakajua jema Na baya Na ukijua baya ukatenda lazima utiwe hatiani na mtu yoyote akitiwa hatiani maana yake lazima aadhibiwe .Nao walipewa kifo Kama adhabu .So Kwa lugha ingine Mungu kuwazuia kula tunda la kujua jema Na baya alikuwa anawasaidia wao wenywe wasiingie katika hatia wakikosea akaona bora wabaki illiterates awaongoze kwa maagizo yake tu Kama mtoto anavyopewa Maagizo Na mzazi Ili wasiwe guilt(maana ukiwa guilt lazima uadhibiwe).Na alijua akiwaambia tu hilo la kujua jema Na baya baada ya kula tunda Kwa akili zao wangeona Ni jambo zuri (Kama Eva alivyoona Ni jambo zuri alivyodangnywa Na shetani)lakini mwisho wa siku kujua mema Na mabaya kuna gharama Yaani adhabu ambayo ndo hii Mungu alikuwa anajaribu kuwasaidia


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Papa Francis amesema,So what?
Loyalty To country Alyways,To government When it deserves
 
Ulitegemea aseme nini cha tofauti.
Usianzishe vita ya mawe ukiwa katika nyumba ya vioo.Hapa JF kuna watu wenye kufikirisha bongo zao sawasawa jiupeshe kuleta habari nusunusu na vi-stori vya udaku tu kutoka mitaani.

Loyalty To country Alyways,To government When it deserves
 
Mimi kwanza hata siamini kama shetani yupo kweli...kuna siku nimeingia room na demu, binti akanichomolea, sasa kama shetani yupo kazi yake nini?

[Kidding, lol]
 
Hapo mkuu umeandika kweli hata sisi tulio kuwa wagumu kuelewa naona somo limeingia shukrani!
Kupata ufahamu wa kujua mema na mabaya hiyo haiwezi kufanya uwe sawa na Mungu hapo inadhibitisha hata shetani mwenyewe alikua mwongo kwa kuwaambia wakila wangekua sawa na Mungu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo mkuu umeandika kweli hata sisi tulio kuwa wagumu kuelewa naona somo limeingia shukrani!
Kupata ufahamu wa kujua mema na mabaya hiyo haiwezi kufanya uwe sawa na Mungu hapo inadhibitisha hata shetani mwenyewe alikua mwongo kwa kuwaambia wakila wangekua sawa na Mungu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kila mtu Ana uhuru wa kuabudu anachojisikia kuabudu, na ndio maana kuna wanaoabudu sanamu , Ng'ombe, Nyoka na Miti

Acha kuwa na mawazo Mgando ndugu na nidhamu ya uoga, kwa hiyo unamuabudu Mungu kwa kuwa unaogopa kufa au ? , ebu jisikilize Tena , come out of your shell , be free , emancipate yourself from mental slavely

It's me

ISHMAEL
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…