Mbona kila kitu nimeeleza, jaribu kutuliza akili yako na andika kwa paragraph mkuu.
Mungu yupo kama binadamu , siku zote binadamu anataka ufanikiwe ila sio kufanikiwa kumzidi, huyo Ndo Mungu , na kumbuka alisema yeye ni Mungu mwenye wivu , hakati tumwabudu Miungu yeyote zaidi yake , apo inamaanisha kuna miungu mingine powerful kumzidi
Aliwafukuza adam na hawa bustanini kwa kuhofia watakula mti wa uzima na kuishi milele, Sasa hapo ndo ujiulize why Mungu hakutaka tuishi milele? Na anasema anatupenda
Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu jibu maswali yangu niliyokuuliza,kuna vitu naona unajichanganya mwenyewe,Mungu aliposema yeye ni Mungu mwenye wivu ni kweli imeandikwa hivyo,wewe unatoa wapi maelezo kwamba kama ni mwenye wivu maana yake anaonea wivu miungu wengine
wenye nguvu kuliko yeye?
Wewe ni wapi kwenye biblia imeandikwa hao miungu wengine wana nguvu kuliko yeye?Hapo ndipo unakua unakosea .
Unaelewa maana ya Mungu Mwenyezi?Almighty God?Kasome biblia vizuri kisha jitahidi kuelewa majina aliyokuwa anayatumia Mungu yana maana gani.Kumbuka maswali yangu kwako yajibu mkuu.Mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu hii haimanishi mwanadamu analingana kila kitu na Mungu,kasome biblia yako kwanini anasema njia zake si kama njia za wanadamu na akili ya juu ya mwanadamu haifikii hata upumbavu wa Mungu ingawa Mungu si mpumbavu hapa anajaribu kuelezea kuna knowledge gap kubwa sana kati ya Mungu na wanadamu.Sasa wewe naona unasoma biblia kweli ila kuna kitu kimezuiwa kwako na ndiyo maanda nikauuliza wewe ni devoted christian au unasoma biblia kwa sababu zako fulanifulani?
Mpango wa Mungu ni tuishi milele na kwa taarifa yako unaposema kifo kuna vifo vya aina mbili kuna kifo cha mwili kwa maana ya mwili kutengana na nafsi na mwili hiki tulichokizoea na kuna kifo cha nafsi na Roho ambayo ni kutupwa katika ziwa la moto.
Ndiyo maana Mungu akasema msimwogope awezaye kuangamiza mwilil tu bali mwogopeni awezaye kuangamiza mwili pamoja na Roho,Mungu pekee anaweza akaangamiza mwili na Roho wengine ni mwili tu.
Mkuu piamkumbuka Mungu wa kwenye biblia ni Mungu wa miungu,hapa sijui kama unaelewa,ni kweli anatambua uwepo wa miungu wengine lakini hawana uwezo kama yeye na wala hao miungu wengine hawakuumba bali yeye ndiye aliyetuumba.Sasa anakuwa na wivu akiona mwanadamu anaabudu miungu wengine na kumwacha yeye.
Kama unataka kuishi milele mbona solution yake ipo ni kumpokea Yesu kufanyika kuwa Bwana na mwokozi wako,ishi maisha matakatifu kama ambavyo biblia inatufundisha utaulithi uzima wa milele.
Unajua sikuelewi kama kweli unasoma biblia kwa nia ya kujifunza au kuikosoa injili,Yesu alipokutana na mwanamke msamaria alimwambia yeye ni maji ya uzima.Kifo cha kwanza kinatokana na dhambi ya Adam na Hawa,lakini Mungu aliamua kumtoa mwanaye wa pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.Haya maandiko hujawahi kukutana nayo au ni ubishi tu mkuu?
Mimi nikushauri endelea kusoma biblia,ukitaka maelezo just pm me nitakusaidia kuliko kuja hapa ,kuandika vitu ambavyo vitawapotosha wengine wasiosoma maandiko na mwishoni uwe na cha kujibu mbele ya Jehova.Sikuzuii kuandika ila nakutahadhalisha kuna adhabu kubwa kwa walimu,unapokuwa unawafundisha watu make sure una uhakika na unachoandika.
Mambo haya tunayoyaandika na kuyaongea yatatumika juu yetu kama ushahidi mbele za Mungu hata kama unatumia jina ambalo si lako lakini Mungu ananijua mimi ni nani na wewe ni nani na nitatoa hesabu ya yote ninayoyafanya kwenye mitandao.
Waswahili wanasema ukitaka kujua utamu wa ngoma ingia ucheze,tumeona matendo makuu ya Bwana,tumeona mapepo yakiomba yapelekwe kwa miungu wengine huko hakuna moto ila huku kwetu tukiliita jina la Yesu moto unawaka.Sasa huwezi kuwa nje kisha ukadai unayajua sana ya ndani,ingia full na si mguu nje mguu ndani,you will never know the full picture.
Mkuu nilitumia muda sana kufuatilia haya mambo njoo pm ukitaka kujua zaidi nitakuambia na vitu uvifuatilie mwenyewe katika dunia hii ndiyo utajua Jehova ni Mungu mwenye uweza na nguvu wala hakuna mwingine kama yeye.
Shida ya siku hizi za mwisho watu wanataka watumie akili zao kureason mambo ya Mungu ,huwezi kuujua ukweli utapotea.
Kasome
kumbukumbu la torati29:29.Kuna mambo Mungu ameyafunua kwetu na mengine hajayafunua kwetu,kuwa makini hapo shetani hata leo ameendelea kuwakamata watu kwa kuwaletea elimu mpya,nao wanaona ni uhuru waomkujifunza hayo mambo bila kujali chanzo chake ni nini Mungu au shetani.