Quote: Mtanzania
Mkandara,
Nafikiri kwenye suala la Msekwa kulikuwa na siri kubwa maana hata hapa JF tulishindwa kabisa kutabiri.
Habari haikutoka mpaka baada ya kikao cha CC.
Mtanzania, si kweli jina la Msekwa lili leak a weak ago.... tatizo watu hawakuliwekea maanani..
__________________
Jambo jingine litakalozingatiwa na Mkutano Mkuu ni nafasi ya Makamu Mwenyekiti, inayoshikiliwa sasa na John Malecela.
Malecela hakuwania nafasi ya u- NEC na kuna kila dalili kwamba anaweza kubadilishwa. Baadhi ya majina ambayo yamekuwa yakitajwa ni ya pamoja na Pius Msekwa na mkewe, Anna Abdallah; Sumaye, Kinana na wengine wanamtaja hata Mangula, wote wakionekana kutokua ndani ya kundi maarufu la wanamtandao lililotajwa kusaidia ushindi wa Rais Kikwete.
Malecela amekalia umakamu kwa kipindi kirefu na dhahiri kwa hali ya mambo ilivyo kurejea kwake katika nafasi hiyo kuna utata. Wakati ule wa awamu ya tatu, inaelezwa, kwamba ilihitaji nguvu ya ziada ya Mwenyekiti Mkapa kutetea uteuzi wake, japo baadaye ilikuja kuonekana kuwa nafasi hiyo ilistahili mtu kama Malecela.
Nafuu, pengine ya Malecela (hata kama akiukosa umakamu) na wazee wenzake kama Cleopa Msuya, imo katika sehemu ya mabadiliko ya katiba ya CCM yanayopendekezwa ya kuwafanya wazee kama hao kuwa wanachama wa kudumu wa NEC.
Kwa sasa wanachama hao dumu ni pamoja na Rashidi Kawawa, Mwinyi, Mkapa na Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk Salmin Amour.
Awali, jina la Msekwa halikuwa miongoni mwa wadadisi wa masuala ya kisiasa, huku majina yaliyokuwa yakipigiwa chapuo ni Mbunge wa zamani wa Ngara, Pius Ngeze, Mbunge wa Sumbawanga, Paul Kimiti, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.
Nafasi ya Katibu Mkuu wa CCM inashikiliwa na Makamba nayo inaelezwa kuwa huenda ikakumbwa na mabadiliko, huku nafasi kubwa ikitolewa kwa Naibu Katibu wake, Kapteni Jaka Mwambi na Spika mstaafu wa Bunge la Afrika Mashariki, Kanali Abdulrahman Kinana na nafasi ya Mwambi huenda
ikishikiliwa na Mbunge wa Songea, Dk Emmanuel Nchimbi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM.
GAzeti la Mwananchi la Novemba 2, 2007, siku tatu baada ya kutoka kwa toleo la kwanza la Raia Mwema, liliandika:
Na hii si pekee, kwani Mwandishi Taseni ameandika pia katika gazeti la Citizen kwamba hakuna mtu hata mmoja aliyemtaja Msekwa. Hii ni dalili mbaya sana ya waandishi kutokua makini na kusoma habari za wengine, lakini pia ni aibu kwani habari kuhusu Msekwa baada ya kuandikwa na Raia Mwema ziliwekwa humu JF. Lakini kwa waandishi wengi makini walikua wakijua kuhusu Msekwa hasa baada ya JK kupelekewa majina matatu la Mangula, Sumaye na Msekwa, na hivyo kwa wanaomjua Msekwa walijua fika ndiye anayetakiwa. Lakini pia, Msekwa alitafutwa na IKULU katikati ya Oktoba, 2007 kwa juhudi zote na alikwishajulishwa kama atakua tayari kushika wadhifa huo na yeye kukubali, kuendelea kukitumikia chama chake. WAANDISHI MAKINI walifahamu na humu JF kuna mahali ilitajwa kuhusu majina matatu akiwamo Msekwa.
Mkandara,
Nafikiri kwenye suala la Msekwa kulikuwa na siri kubwa maana hata hapa JF tulishindwa kabisa kutabiri.
Habari haikutoka mpaka baada ya kikao cha CC.
Lt Makamba bado anafaa sana kuendelea kushika nafasi ya Ukatibu Mkuu. Utendaji wake upo katika kiwango cha juu kupita wakati wote wa uongozi wake kwa sasa. Tatizo ni mitazamo hasi ya wengi, ambao hupenda kusikia yale yaliyo kwenye nafsi zao tu. Mpaka sasa ameweza kuwazindua watendaji wengi goi goi ndani ya CCM kuanzia ngazi za matawi, ambao walikuwa wameanza kujisahau katika utendaji wao wa kila siku. Kitaifa ameendelea vema kusimamia matakwa ya CCM katika awamu ya kuziba mpasuko huko Visiwani.
Hapana shaka ataendeleza vema mazungumzo ya kufikia muafaka ambao utakuwa na manufaa kwa pande zote mbili.
Hoja za Upinzani kuhusu Ufisadi na mafisadi ameweza kuzijibu kwa ufasaha kabisa na kisiasa zaidi, na hakuna mjadala kwa hilo.
Swali ni jee style yake ya kazi atawezana na Mzee Msekwa?
Makamba -secretary general
Amos Makala-FEdha
Kidawa-Oganizainesheni
Membe-Mahusiano ya mambo ya nje
Source:Nchimbi
Makamba -secretary general
Amos Makala-FEdha
Kidawa-Oganizainesheni
Membe-Mahusiano ya mambo ya nje
Source:Nchimbi
Hata kama JK angetaka kubadili watu wamevujisha mno mapema hadi kwenye magazeti, kwa hiyo ameamua kuwaumbua. Nadhani hataki kuonekana anafanya kazi kwa kufuata maoni ya magazetini. Maoni yangu.