JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,462
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi, ACP Kaster Ngonyani amesema katika misako mbalimbali inayoendelea katika mkoa huo limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 121 wakiwa na vielelezo mbalimbali vya tuhuma hizo.
Aidha, jeshi hilo limewakamanda Watuhumiwa 14 kwa makosa ya mauaji ambayo yametokea kwa nyakati tofauti katika mkoa huo ambapo amesema watuhumiwa wote wanaendelea na mahojiano mara baada ya kubainika na makosa jeshi hilo litawapeleka mahakamani ili kujibu mashitaka ya tuhuma zao.
Katika hatua hiyo Kamanda Ngonyani amewataka wananchi wote wa mkoa huo kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali kwa amani na utulivu hasa katika kuelekea msimu wa sikukuu ya krismas na mwaka mpya.