Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Bado masaa machache tu kuaga mwaka wa 2025 na kuukaribisha mwaka 2026, wakuu ndipo simu zinapoanza kulia kwa fujo. Ghafla, watu waliokuwa kimya na jeuri kwa siku 364 na zaidi wanakumbuka uwepo wako.
Unakutana na liujumbe refu: “Kama nimekukosea nisamehe,” “tusameheane kabla ya mwaka kuisha,” “maisha ni mafupi ndugu yangu mpendwa, mwaka 2026 ukawe baraka kwako na familia yako, tuendelee kupendana.” Ajabu ni kwamba Krismasi ilipita kimya, Pasaka ilipita kimya, hata kuugua kwako hawakujua wala kujali unaendeleaje—lakini tarehe 31 Desemba wanakuwa watakatifu wa ghafla.
Hii si toba, ni maigizo. Ni unafiki unaovaa koti la unyenyekevu. Ni watu wachache wanaojitengeneza kuwa wahanga wa kutowasiliana, ilhali wao wenyewe walichagua kunyamaza kwa mwaka mzima. Wengine hata namba zao ulikwishazifuta, lakini wanatuma sms ndefu kama thread kana kwamba walikuwa karibu nawe kila siku.
Leo langu wala kukataa msamaha—la hasha, msamahani jambo la msingi. Lakini ninakosoa msamaha wa dakika za mwisho unaotumwa kwa wingi, bila dhamira ya kubadili tabia. Mwaka huu 2025 unapofunga pazia, acha unyonge. Ingia mwaka 2026 kibabe sio kinyonge.
Kataa SMS za kinafiki au kutoka kwa watu ambao wanakuletea unafiki. Usikubali kulazimishwa kusamehe ili watu wajisikie vizuri na kuingia 2026 bila mzigo wa dhamira. Msamaha wa kweli huanza na kuwasiliana, sio sms nyingi tarehe 31 Disemba.
Unakutana na liujumbe refu: “Kama nimekukosea nisamehe,” “tusameheane kabla ya mwaka kuisha,” “maisha ni mafupi ndugu yangu mpendwa, mwaka 2026 ukawe baraka kwako na familia yako, tuendelee kupendana.” Ajabu ni kwamba Krismasi ilipita kimya, Pasaka ilipita kimya, hata kuugua kwako hawakujua wala kujali unaendeleaje—lakini tarehe 31 Desemba wanakuwa watakatifu wa ghafla.
Hii si toba, ni maigizo. Ni unafiki unaovaa koti la unyenyekevu. Ni watu wachache wanaojitengeneza kuwa wahanga wa kutowasiliana, ilhali wao wenyewe walichagua kunyamaza kwa mwaka mzima. Wengine hata namba zao ulikwishazifuta, lakini wanatuma sms ndefu kama thread kana kwamba walikuwa karibu nawe kila siku.
Leo langu wala kukataa msamaha—la hasha, msamahani jambo la msingi. Lakini ninakosoa msamaha wa dakika za mwisho unaotumwa kwa wingi, bila dhamira ya kubadili tabia. Mwaka huu 2025 unapofunga pazia, acha unyonge. Ingia mwaka 2026 kibabe sio kinyonge.
Kataa SMS za kinafiki au kutoka kwa watu ambao wanakuletea unafiki. Usikubali kulazimishwa kusamehe ili watu wajisikie vizuri na kuingia 2026 bila mzigo wa dhamira. Msamaha wa kweli huanza na kuwasiliana, sio sms nyingi tarehe 31 Disemba.