Kassim Majaliwa: Makontena ya Makinikia yanayosafirishwa nje ya nchi ni halali

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,112


Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa amewatoa hofu Watanzania kuhusiana na kuwepo kwa makontena yenye makinikia ambayo yameonekana yakisafirishwa kwenda nje ya nchi kuwa makontena hayo yanasafirishwa kihalali.

Waziri Mkuu amesema hayo bungeni Mkoani Dodoma wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu kitendo ambacho hufanyika kila siku ya alhamisi iwapo waziri mkuu anakuwepo bungeni.

Amesema makontena hayo yanasafirishwa chini ya utaratibu maalum ambao umewekwa na Serikali kupitia kampuni ya umma ya madini ya Twiga kwa kushirikiana na wachimbaji wakubwa wa madini.

Waziri Mkuu amesema kinachofanywa sasa na serikali kwa kilichopo ndani ya makontena hayo kukaguliwa na kupimwa kisha serikali kulipwa inachotakiwa kupata na baada ya hapo wahusika wa makontena hayo yenye makinikia kupewa nyaraka za kuwadhibitisha ambazo hutakiwa kuzionyesha mara zinapohitajika.

Mwaka 2017 hadi mwaka 2018 Serikali tume maalum ya kuchunguza jinsi ambavyo Tanzania inavyonufaika au la na Sekta ya madini ambapo ilibainika uwa sekta hiyo imegubikwa na udanganyifu.
IMG_20210603_180628_055.jpg

Makinikia.jpg
 
PM anaingizwa chaka baya bila kujua. Ameulizwa general question, na alipaswa kama mtendaji mkuu wa serikali, kupress for more specific details, na wala siyo kuhangaika haraka kuwasilisha maelezo mengi kwa lengo tu la kuwapooza Watanzania.

Hoja ya msingi: ^Kontena zileeeeeee zinaenda tena^

PM angeomba ushahidi specific na kuahidi kufuatilia. Suala la madini ni nyeti sana na limetugharimu mengi huko nyuma na hata wakati wa kurekebisha sheria za madini. Pia linamendewa usiku kucha na wapigaji wa ndani na nje ya nchi. So, halipaswi kujibiwa na kupita kijuujuu tu hivi.

PM zile nguvu zako za weledi na uzalendo halisi ziko wapi!??? Ama ziliishia ileeee tarehe 17 Machi 2021!??? Nawe umekuwa kama Bi Mkubwa na Dkt Plan wake ambao wamewekeza vipaumbele vyao kwenye empty hotuba tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!???
 
PM anaingizwa chaka baya bila kujua. Ameulizwa general question, na alipaswa kama mtendaji mkuu wa serikali, kupress for more specific details, na wala siyo kuhangaika haraka kuwasilisha maelezo mengi kwa lengo tu la kuwapooza Watanzania.

Hoja ya msingi: ^Kontena zileeeeeee zinaenda tena^

PM angeomba ushahidi specific na kuahidi kufuatilia. Suala la madini ni nyeti sana na limetugharimu mengi huko nyuma na hata wakati wa kurekebisha sheria za madini. Pia linamendewa usiku kucha na wapigaji wa ndani na nje ya nchi. So, halipaswi kujibiwa na kupita kijuujuu tu hivi.

PM zile nguvu zako za weledi na uzalendo halisi ziko wapi!??? Ama ziliishia ileeee tarehe 17 Machi 2021!??? Nawe umekuwa kama Bi Mkubwa na Dkt Plan wake ambao wamewekeza vipaumbele vyao kwenye empty hotuba tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!???
Huyu jamaa sijui hata kama anaelewa cheo chake
 
PM anaingizwa chaka baya bila kujua. Ameulizwa general question, na alipaswa kama mtendaji mkuu wa serikali, kupress for more specific details, na wala siyo kuhangaika haraka kuwasilisha maelezo mengi kwa lengo tu la kuwapooza Watanzania.

Hoja ya msingi: ^Kontena zileeeeeee zinaenda tena^

PM angeomba ushahidi specific na kuahidi kufuatilia. Suala la madini ni nyeti sana na limetugharimu mengi huko nyuma na hata wakati wa kurekebisha sheria za madini. Pia linamendewa usiku kucha na wapigaji wa ndani na nje ya nchi. So, halipaswi kujibiwa na kupita kijuujuu tu hivi.

PM zile nguvu zako za weledi na uzalendo halisi ziko wapi!??? Ama ziliishia ileeee tarehe 17 Machi 2021!??? Nawe umekuwa kama Bi Mkubwa na Dkt Plan wake ambao wamewekeza vipaumbele vyao kwenye empty hotuba tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!???
Limekugharimu nn ww mmachinga embu nenda kakate kitambulisho cha machinga cha elf20 ukauze mitumva yako
 
Hii nchi wanakula wachache kwenye hilo la makinikia akiwemo na huyu mjuba..

Hawezi kutoa majibu mepesi hivyo ka si mnufaika..
 
Back
Top Bottom