Kasoro kubwa katika video ya Lwakatare

Kasoro kubwa katika video ya Lwakatare

Namfahamu vizuri lwakatare na sina shaka ni yeye, kuukataa ukweli ni kujiumiza. Ninachopingana na watu wa Ccm ni kuongezea maneno, kwa mfano hakuna mahali lwakatare amekiri kuua mtu au kumuumiza lakini ametolea mfano wa upelelezi walioufanya igunga na morogoro, kama amekiri kwamba waliua basi ipo nyingine.
lakini pili, anaonya kuhusu kuumiza mtu kwamba wasimuumize wala kumjeruhi mtu. Kosa lilipo ni lile la kutaka kumtisha mtu na si kujeruhi
 
hayo maneno ni ya Lwakatare

na alipewa nafasi kwa sifa zinazofanana na hayo maneno

ila hayo maneno si ya kibanda, bali ya kumnasa mtu kwenye kashfa ya uzinzi na ulevi........... GO FIGURE
 
Kwenye hii clip ya Obama, sauti sio yake ila mdomo unaendana sawa na maneno yanayosemwa. Mtu mwingine ameigiza sauti ya Obama na kusema maneno anayotaka yeye.

Kwenye clip ya Lwakatare, sauti ni yake kabisa na wala hilo halina ubishi. Je Lwakatare alishiriki katika kutengeneza hiyo video? kama hiyo clip ni fake je sauti yake waliitoa wapi?

Mkuu wangu hiyo clip ni genuine kabisa wala usiumize kichwa. Wewe subiri tu Mchungaji amwage ukweli wote hadharani maana hapo hachomoki!!
Technologia ni dynamic, watu wanakesha Lab kufanya kazi na kuimprove performance/accurace/precision etc ya hivi vitu. Mwanzo ilisemekana midomo kucheza sambamba na maneno, ni kitu kisichowezwa kuigizwa, nadhan kwa hilo clip hii imefanikiwa kuli prove wrong, mmebaki na point ya aina za sauti. Haya ngoja tuzame tutakuja na yenye sauti halisi kama hiyo wewe unaiona sio sauti inayotoka kwa muongeaji, Stay tuned!!
 
Sioni makosa yoyote kwenye video hiyo.
Kwamba alikua anaongelea wapi,hakuogopa kuonekana au nini nini sio swal la msingi.

Cha msingi ni kwamba:-
1.Huyo ni Lwakatare halisi,sio uongo.
2.Aliongea aliyo ongea,swali ni je,ni nini motive nyumba yake?
a)Kwanini atake kuua waandishi wa habari?
b) Nani ana mtuma kufanya hivyo?
c) Ni kweli kwamba chadema ina ugomvi na vyombo vya habari kiasi hicho?

3. Vipi kama ame nunuliwa kufanya hivyo?
a) Nani anaye m-fund?
b) Ili iweje? Nani targets kwenye hii kesi huko mbeleni?
c) Lwakatare kanyimwa nini huko chadema hadi akubali kulipiza kisasi kiasi hiki?

All in all,ndiye aliye ongea,wapi na katika hali gani sio ya msingi sana.
Cha msingi ni kaongea na maongezi yame onekana either kwa bahati mbaya au kwa kukusudia.

Tujiandae kwa yanayo kuja,ila target sio waandishi wa habari,target sio Lwakatare,
target sio kuwasahaulisha mambo ya msingi,target ni Pesa na uchaguzi wa 2015.

Poleni wapenda siasa,mie natafuta hela tu.
naôna wewe huzungumzii hii clip, kwamba ni Lwakatare nina uhakika ni yeye kabisa, lakini kwamba anapanga kuua au kumjeruhi mtu huu ni uwongo wa karne..maana nimeicheza zaidi ya mara tano lakini hakuna mpango wa mauaji hapo, lengo kuu ni kumtisha mtu anayeihujumu chadema kwa mbinu zozote lakini si kwa kumuumiza, acha unafiki!
 
Wana mapinduzi wanaamini kuwa ukiona mambo kama haya tambua kuwa ukombozi upo karibu. Uhuru na Ruto walifanya kama haya na sasa wameingia ikulu, aibu kwa ICC na mafia wao. Nadhani ni muda wa kushangilia ushindi na mapinduzi ya kweli, watanzania wenye akili, na hasa hawa wanaotumia mitandao ya kijamii na forum makini kama JF watatumia akili zao kuchambua hili. Maana mengi yamesemwa kuhusu CHADEMA yameshindwa....walianza na ukanda ukashindwa, wakaja na dini wakashindwa, wakaja na kadi ya dokta Slaa wakashindwa, sasa wemeibuka na mauaji...hakika MUNGU ni yule yule jana, leo na hata milele, ataendelea kutupigania wana CHADEMA.

Tualianza na MUNGU, tunaendelea na MUNGU, tutamaliza na MUNGU
Ikiwa MUNGU, yupo upande wetu, nani atanyanyuka kinyume chetu?

Mungu hawezi kuwa upande wa wauaji hata siku moja!
 
naôna wewe huzungumzii hii clip, kwamba ni Lwakatare nina uhakika ni yeye kabisa, lakini kwamba anapanga kuua au kumjeruhi mtu huu ni uwongo wa karne..maana nimeicheza zaidi ya mara tano lakini hakuna mpango wa mauaji hapo, lengo kuu ni kumtisha mtu anayeihujumu chadema kwa mbinu zozote lakini si kwa kumuumiza, acha unafiki!

hakuna mpango wa mauaji ila kuna mpango wa kujeruhi kama walivyofanya Morogoro na Igunga. hata hayo hukuyasikia? tatizo lako ni kupenda sana Cdm au nini?
 

Kwa uzuri kabisa kuna video nyingine zinakuja; zitatoka kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.Kati ya video hizo (kutokea CCM) moja inamwonesha"S.6 akiongea ama na Lowasa na Mwakyembe(hawa hawaonekani kwenye movie ila wanatajwa) S.6 anaongelea jinsi ya kuukabiri udini wa JK"; nyingine ni ya B.maembe akimwelekeza kijana mmoja kumfuatilia Lowasa na Bashe kujua wanapanga nini"; kisha ipo nyingine inayomwonesha Kinana" Akimwomba JK (hayupo kwenye picha ila kicheko chake kinasikika) asaidie kumaliza suala la pembe za ndovu kule Hongkong"; Aidha, iko pia video inayomwonesha "JK akimwahidi watu fulani kwamba kina Basir na Mgoja watafungwa kabla ya uchaguzi mkuu ili kuaminisha umma kwamba CCM inapigana kikweli dhidi ya ufisadi".Iko inayomwonesha Wassira akimwita mtu mmoja Sheikh(hayumo katika picha) anasema, hili la kuchinja nitalimaliza tu, anasema ninyi ni lazima muendelee kuchinja, CCM haitaki kuzikosa kura zenu kwa jambo dogo la kuchinja, mtachinja tu"

Mtaona mengi safari hii. Mwl. Nyerere alisema wakishajitenga hawatakuwa salama, hatimaye wataona kuna wanzanzibar na wazanzibara. Sera za CCM dhidi ya CDM zitaanza kutumika pia kulana wenyewe kwa wenyewe.

Acha blah blah wewe jadili hoja ya lwakatare na mauaji ya Watanzania wenzio wasio na hatia!
 
Computer ni kitu cha ajabu kwa mtu anayejua kuitumia. Waweza kuchukua picha ukawekea maneno mengine na background scene na sauti tofauti kabisa kiasi mtu asiyejua IT akadhani ni picha halisi. Ni mchezo mdogo sana wa IT. Najua hii imetengenezwa kuwa confuse wengi lakini mtu anayejua hiyo michezo ya IT anajua kwa hakika kuwa kuwa hiyo sio picha na maneno halisi. Maelezo mengi yametolewa kuhusu hilo na sipendi kuyarudia ila tu- NI PICHA YA KUGUSHI!

na Lwakatare akija kukuri hadharani ni yeye utakimbilia wapi? acha kuwa msemaji wake tumsubiri mwenyewe aje atuambie kisa cha kupanga mikakati ya kujeruhi watanzania wasio na hatia ni nini?
 
Chadema mbona mnahangaika sana na Video ya Lwakatare! Tumeiona tume ielewa!
tusipo kuwa makini ccm itatuingiza kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. they are stupid! haiingii akilini mtu anae panga uhalifu awepo mahali ambapo panaingilika na ewatu kwa namna ile. infact huyu rwakatare aidha amelipwa handsomely au ni mchezo wa computer.ccm amkeni hawa vijana wenu mmewaamini kupita kiwango, wataiingiza nchi hii kwenye machafuko kama ya RWANDA. Kama jahazi lenu linazama jiulizeni kwanini watanzania wamewachoka?
 
Imani kali ya kilokole...

Subirini haya mtayasema mahakamani.

CC.. Ng'wamapalala, chama, Mingoi, Kimbunga,
Mkuu Ritz sikutegemea kama kuna watu ndani ya chama cha siasa wanaweza kujadiri kuumiza watu/kuua ili wapate wanachama, wapenzi na washabiki kwa mategemeo ya kupewa kura. Hizi ni zaidi ya siasa za majitaka. Desparation breed wicked act. It vex me, hawa watu kila siku wanadai Mungu yuko upande wao. Mungu gani huyu?.

It's despairing siasa zetu zimefikia kiwango hiki.
 
Hii video itawatesa sana naona mnajaribu kufanya cover up lakini ukweli huu wa vitendo vya utesaji ambao umekua ukifanywa na kitengo cha ulinzi na usalama ndani ya chadema utaishi muda mrefu sana.
2010 mlitengeneza sms zenye kodi namba za finland!, "made in lumumba"
 
Video ya Rwakatare ni mbinu mpya za Kelelectronic ambazo magaidi wanatumia kutimiza malengo yao. Mafunzo ya kigaidi huko Somalia hayaishii kuua na kuchoma makanisa tu bali pamoja na wizi kwenye mabenki na utapeli wa ki-Electronic. Hebu tazama hii!!! Ukiwa na akili timamu utaamini kwamba Obama aliyasema haya? "Inauguration 2013: A Bad Lip Reading:
 
Ninachopenda CHADEMA ipo makini sana na weng wa wanachama wake/ wanazi wake na ata mashabiki wake ni wasomi wa elimu ya juu na ya kuhoji/utambuzi tu lakini wenzetu ni elimu mgando na weng wao ni darasa la saba kihalali plus kuungaunga na vyuo uchara....

Sasa kwa akili hizo zao wanaamini watu hatujui mambo, nawambie tena msisumbuke na propaganda zenu watu wamechoka na maisha tekelezeni ahadi 72 'mlizo ahidi ata 1/4 itatosha.

@ wasira, makamba jr, nape, ritz.
 
Ukiwa mnafiki uwe na kumbukumbu, na wewe umetumia teknolojia gani kumlisha maneno Riz wan na Nape kuwa wamesema Chadema wanahusika, Wengi wetu tulipitia Wall paper ya Ridh na Nape hakuna neno Chadema walipotaja, Alama za Mtu mnafiki ni 3 na moja wapo ni Uongo.Lwakatare kesha nasa kwenye mtego hateguliwi kwa manati mtazid kumuumiza! Yeye ndo atathibitisha sio kukimbilia kwenye Google Engine kutafuta namna ya kumtoa!

Wall paper ya Riz!!?? ndo makitu gani mkuu..!??
 
Back
Top Bottom