Molemo umeniliza,Naapa chini ya Mbingu na Ardhi kamwe Shetani hatamshinda Mungu.
Kama Daudi alimuua Goliathi kwa jiwe katu Mashetani hawa wanaotaka kuichafua Chadema hawatafanikiwa na wataangamia.
Naapa kwa Mungu aliye hai yeyote aliyeshiriki kutunga mpango huu mchafu hatabaki salama.
Naapa kwa Mungu Mkuu muumba kila kitu kwamba kila aliyeshiriki kutunga uchafu huu lazima ataumbuka siku si nyingi na ataiomva radhi hadharani.
Naapa kwa Mungu aliyemwangamiza Anania akapasuka matumbo mbele ya madhabahu kwamba wahalifu hawa watafuata njia hiyo hiyo.
Naapa kwa Mungu aliyemwangamiza Herode akadondoka juu ya kiti cha kifalme na mwili wake kuliwa na siafu kwamba waovu waliotunga mbinu hii watafuata njia hiyo hiyo.
Naapa kwa Mungu wa Abraham,Isaka na Yakobo kwamba watu hawa hawataweza kuendelea kuharibu Taifa letu kwa uchochezi wao bali watakipata sawasawa kile kiwapatacho watu wasiomjua Mungu.
Naapa kwa Mungu ambaye jina lake ni NIKO AMBAYE NIKO kwamba Shetani kamwe hatajitwalia utukufu.
Wao wana Baali na Chadema wana Mungu kamwe Baali hawezi kumshinda Mungu.
Mungu aliyehai ataamua kati yetu na wao,
leo nimekuwa na mojawapo kati ya siku ngumu maishani mwangu, ninazo siku mbaya leo na jana nimechanganyikiwa ni moja kati ya hizo nilizosema..
Hatahivyo naomba tutofautiane, mimi naamini Lwakatare amesetiwa na anaowaamini, watu kama Yuda Iskariote waliomuuza Yesu Kristo wamemuuza Lwakatare, wamekuja na story ya kumchunguza mtu wakijua anawaamini, kama mkuu wa ulinzi kwenye chama akawasilikiliza, akawaamini asijue Nchemba Mwigulu amewapa vipande thelathini vya fedha, katikati ya maongezi ya kumchunguza mtu anayeihujumu Chadema wakamrekodi, maongezi ya kawaida yamezua maongezi mazito.,
Mi sielewi, hivi kufa mtu kule Igunga kumeisaidiaje Chadema? Hivi watu wanaweza kuipenda chadema baada ya mtu kufa? Dr Slaa amepata umaarufu kwa kuteka watu au kwa kujenga hoja?
Mungu atajibu kwa moto!!