Mkuu wangu Mwita Maranya, naomba twende hatua kwa hatua ingawaje nafahamu kabisa hatuwezi kufikia muafaka!! Awali ya yote, kutokamatwa kwa Ighondu sio sababu tosha ya kwamba Lwakatare nae asikamatwe (bila kujali kama ni kweli amefanya au hajafanya)! Tunaweza kulalamikia suala la double standard lakini si sahihi hata kidogo kulalamikia suala la kukamatwa Lwakatare! Hilo la Membe sizani kama lina mashiko coz' limekaa kisiasa zaidi na kwa mtu anayemfuatilia Bashe, anafahamu kwamba ni mropokaji anayejitahidi ku-force bifu na Membe! Lakini vile vile, leo ukisema kila kauli ya mwanasiasa uifanyie kazi, basi hakuna lingine litakalofanyika kwa polisi zaidi ya kufuatilia madai ya wanasiasa....!! Wewe mwenyewe shahidi, unaweza usikiri hapa hadharani lakini nafsini mwako unakiri kwamba hata Dr. Slaa nae amekuwa ni bingwa wa kauli tata lakini hajawahi kukamatwa!Mkuu NasDaz kama ungekuwa umewasikia wakuu wa jeshi la polisi wanchokiongea kwenye vyombo vya habari juu ya sakata hili usingeandika huu utumbo uliouandika hapa.
Alichofanya Patriote ni kujaribu kuufahamisha umma juu ya ufirauni uliofanywa na ccm kwa kushirikiana na serikali yao kutaka kuionyesha Chadema mbele ya macho ya watanzania kwamba ni chama cha wauaji wakati ukweli ni kwamba matukio yote ya uhalifu yanayofanyika nchi hii yanaratibiwa na kusimamiwa na vyombo vya dola chini ya ccm.
Dr. Ulimboka alimtaja mtu aliyemteka kuwa ni Ramadhani Ighondu mbona hajawahi kukamatwa ama kuhojiwa? Membe ametajwa na vyombo vya habari kuhusika na tukio la kumteka na kumtesa Kibanda mbona hajakamatwa ama kuhojiwa? Sasa mtu kama wewe unaposhindwa kuona mambo kama haya yaliyo dhahiri kiasi hiki na kufuata mkumbo wa kupiga propaganda inaonyesha dhahiri jinsi waanaojiita wasomi katika nchi hii walivyogeuka kuwa wasaliti.
Badala ya kusimamia ukweli ninyi mmegeuka kuwa makuwadi wa viongozi wa ccm na serikali yake wanaotenda maovu ya kila namn alimuradi tu waendelee kukaa madarakani.
Kama unataka nisimamie ukweli, bado mie ukweli wangu ni ule ule....binafsi sipendi unafiki! Ukweli wangu ni kwamba, video ya Lwakatare ni Genuine na wala sio fabricated...! Watu wamem-set up na akaingia kichwakichwa....anyway, ni ajali kazini coz' haya mambo kwenye siasa yapo! Mkuu wangu utakuwa unafanya kosa sana kutaka kunishawishi niamini vile kama ambavyo wewe na wenzako mnaamini! By the way, as far as upo ndani ya CHADEMA, una wajibu wa kukanusha suala hili coz' usipofanya wewe hakuna mwingine wa kufanya unless kama mtu hutaki ku-practice african politics!
Kama nilivyotangulia kusema, wewe una kila sababu na wajibu wa kukanusha....mimi wajibu huo sina coz' ni mtu huru nisiyefungamana na chochote....video ya Ilunga niliilaani, ya Lusinde vilevile na wacha hii nayo niitafsiri vilevile kama ambavyo nilivyofanya kwa hizo zingine coz' sifungamani na chochote katika hizo...!!
Suala la maovu ya viongozi wa CCM na serikali yake lipo wazi....na hata nikikutuma hapa unitafutie hoja yangu ya kuitetea CCM pale pasipopaswa kutetea, hutaiona!! Lakini uovuo wao huo kamwe hauwezi kuwa ndio tiketi ya wengine nao kufanya uovu! Sie tusio na mlengo wowote, tutapinga na kulaani bila kujali kwamba uovu huo umefanywa na CCM au CHADEMA na wala haitusumbui kuitwa majina ya ajabu ajabu kama mlivyozoea!
Nisisitize tu kwamba sina mashaka hata kidogo na video ile....ni genuine clip na ndio maana hata Dr. Slaa leo wakati anahojiwa amekosa kabisa ujasiri wa ku-defend na matokeo yake akawa anajikanganya kanganya...."mara oh, mmesikia mwenyewe, kwani spray inaua!"
Lakini la mwisho, hebu acha kuwapa ujiko CCM!! Usizani CCM wana uwezo wa kumtumia kila mtu....unawapa sifa adimu ambayo kamwe hawawezi kuwa nayo...! Tukubali kutokubaliana lakini kutokubaliana na CHADEMA not necessary muhusika awe CCM!
Last edited by a moderator: