Mjukuu wa kigogo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2023
- 200
- 434
Binafsi nipongeze mabadiliko yaliyofanywa ya kuleta mkuu mpya wa shule ya Sekondari Nyiendo hapa Bunda.Ushauri wangu kwako naomba ujikite kwenye maeneo yafuatayo ill ufanikiwe
1.Epukana na wapambe ambao kwa lugha za siku hizi wanaitwa "machawa".Hawa ndio sumu kwa maeneo mengi ya makazini duniani.Hawa ndio wanaovunja mahusiano mema makazini.Ukiwa neutral hakika utafanikiwa sana!Nasi twakuombea uwe neutral.
2.Rudisha mahusiano na jamii inayozunguka shule ambayo yalikuwa yamekufa zaidi.
3.Fanya mabadiliko ofisi ya taaluma,hii ofisi ilikuwa imegeuzwa kijiwe cha porojo na majungu.Ikikupendeza upande wa Senior Academic master weka sura nyingine tofauti na aliyepo aliyekaa kwa miaka 12.(Hili liangalie kwa jicho la 3)
4.Rudisha utaratibu wa kuzawadia walimu wanaofaulisha kidato cha pili na cha nne kwenye mitihani ya Taifa.Hii itaongeza morali kwa walimu na kujituma zaidi.Kwa kifupi utaratibu huu ulikuwepo wakati wa nyuma ila kuanzia mwaka 2022 kundi la 'machawa' lililokuwa limemteka akili Mkuu wa shule aliyehamishwa lilimshawishi kuuondoa kutokana na kuwa na chuki binafsi dhidi ya walimu waliokuwa wanufaika wa mwaka huo na kuchangia kuvunja morali ya walimu.Kiongozi mkuu wa hao machawa kashaondoka na kujiunga na shule moja changa.Kuondoka kwa huyu mtu ni ahueni kubwa sana kwa shule.Kazi wanayo huko katika kituo chake kipya.
5.Tumia kila mbinu itakayokusaidia kufanikisha malipo ya walimu wa kujitolea maarufu kwa jina la walimu wa "part time.Hawa wanaishi maisha magumu sana fikiria kipindi cha miezi ya nyuma baada ya makusanyo ilifikia hatua wanalipwa tshs(8000/=)kwa kila mmoja.Hapakuwa na hamasa ya kutosha kuhamasisha michango kutoka kwa mkuu wa shule,School Management Team(SMT) na waalimu waajiriwa kwenda kwa wanafunzi.Lakini pia kuna "rumours"pesa za taaluma zilikuwa zinapigwa kiaina.Hili pia lifanyie kazi.
6.Mtangulize Mungu kwa kila jambo!
Karibu sana Shule ya Sekondari Nyiendo.
1.Epukana na wapambe ambao kwa lugha za siku hizi wanaitwa "machawa".Hawa ndio sumu kwa maeneo mengi ya makazini duniani.Hawa ndio wanaovunja mahusiano mema makazini.Ukiwa neutral hakika utafanikiwa sana!Nasi twakuombea uwe neutral.
2.Rudisha mahusiano na jamii inayozunguka shule ambayo yalikuwa yamekufa zaidi.
3.Fanya mabadiliko ofisi ya taaluma,hii ofisi ilikuwa imegeuzwa kijiwe cha porojo na majungu.Ikikupendeza upande wa Senior Academic master weka sura nyingine tofauti na aliyepo aliyekaa kwa miaka 12.(Hili liangalie kwa jicho la 3)
4.Rudisha utaratibu wa kuzawadia walimu wanaofaulisha kidato cha pili na cha nne kwenye mitihani ya Taifa.Hii itaongeza morali kwa walimu na kujituma zaidi.Kwa kifupi utaratibu huu ulikuwepo wakati wa nyuma ila kuanzia mwaka 2022 kundi la 'machawa' lililokuwa limemteka akili Mkuu wa shule aliyehamishwa lilimshawishi kuuondoa kutokana na kuwa na chuki binafsi dhidi ya walimu waliokuwa wanufaika wa mwaka huo na kuchangia kuvunja morali ya walimu.Kiongozi mkuu wa hao machawa kashaondoka na kujiunga na shule moja changa.Kuondoka kwa huyu mtu ni ahueni kubwa sana kwa shule.Kazi wanayo huko katika kituo chake kipya.
5.Tumia kila mbinu itakayokusaidia kufanikisha malipo ya walimu wa kujitolea maarufu kwa jina la walimu wa "part time.Hawa wanaishi maisha magumu sana fikiria kipindi cha miezi ya nyuma baada ya makusanyo ilifikia hatua wanalipwa tshs(8000/=)kwa kila mmoja.Hapakuwa na hamasa ya kutosha kuhamasisha michango kutoka kwa mkuu wa shule,School Management Team(SMT) na waalimu waajiriwa kwenda kwa wanafunzi.Lakini pia kuna "rumours"pesa za taaluma zilikuwa zinapigwa kiaina.Hili pia lifanyie kazi.
6.Mtangulize Mungu kwa kila jambo!
Karibu sana Shule ya Sekondari Nyiendo.