Kanikataa kwa sababu ya Ufupi...!!

Kanikataa kwa sababu ya Ufupi...!!

Tafuta series ya Game of Throne, ujifunze kwa Tyrion Lannister.....jamaa ni emoro kwer kwer lkn anawapata hao viumbe.

Jipe moyo chief.
 
Habari za majukumu wanajukwaa..!

Rejea kichwa hapo juu, Nimemtongoza kwa zaidi ya miaka miwili kanikataa kwa sababu tu niko mfupi., Ingawaje hata yeye sio Ngongoti.,, Kama kanizidi basi ni cm 3-5...!! Nina 163cm ambazo ni sawa na futi 5.3

Anasema eti itakua kituko siku ya harusi yeye akivaa michuchumio, itabidi nipande juu ya stuli kumchumu ...!! Maneno hayo yote kampa rafiki yake ambaye ni rfk yangu pia hajaniambia mimi direct..!!

Nilipoyaskia yakanitia kichefuchefu kabisa...!! Na kiukweli hii sio mara yangu ya kwanza kukataliwa na wanawake ingawa wengine hawaniambii sababu lkn nahisi kabisa ni hiyo....!! Ingawa wapo wanaonitaka ila mi siwapendi . Na wengine ni wafupi pia wananikataa kisa ufupi nashindwa kuwaelewa...!!

Jamani mnataka mi nikaoe Nyani..?? Umri wenyewe ndo huo, na sina mashaka na sura yangu ingawa mwanaume hasifiwi sura ila wengine wanaogopwa zipo kama Ismigo na ni wafupi...!!!

Naombeni ushauri wadau hivi hawa wanawake nifanyaje...?? Kama ni swaga zipo, sijawahi kua domo zege kabisa, ni mchangamfu sana.,

Pessa zipo ila Siwapi na siwaoneshi kama ninazo.....!! Nna uhakika mtaani kwetu hakuna mtu ananikaribia hata kwa kujikosha kwa mpunga ingawa mauzo sipendi kwa hiyo maisha yangu nayaweka kawaida sana si rahisi mtu mwngine kujua wa nje.....!!

Au wafupi haturuhusiwi Kuchagua...???
Inshu ya ufupi imekua serious kiasi hiki..?? Mbona wazee wa zamani walichukuana mwanaume mfupi na mwanamke mrefu tu...??
Bs tafuta mfupi mwenzio mkuu
 
Inasikitisha sana...

Pole sana.. Utapata wa rika na size yako... Endelea kumuomba Mungu...


Cc: mahondaw
 
Jiamini wewe..unapoteza kwanza sababu kukataliwa mbona kawaida tu na si kila unaemtokea akukatalie sema na wewe jichunguzepo ucje ukawa unakurupuka na kila anaekatiza mbele yako
 
Mkuu kwanza hongera kwa kumkosa mwanamke ambae anafikiria harusi na si ndoa.
Pili kibongobongo wewe sio mfupi sm 163 c'mon. Kutokana na mazingira yetu hapa bongo wewe ni wakawaida ila sio mrefu(average height ya Tanzania according to Wikipedia ni 5'5).
Tatu kama wanajukwaa walivyotangulia kusema wanawake wanapenda mtu ambae atawafaya wafeel secured. Sasa basi tafuta pesa tafuta power ...hivyo vitu vitakufanya uwe reliable
Nne hakuna kitu sexy kama confidence. Jiamini.....hii nayo wanawake wanapenda sana man alie confident.... Huwafanya wafeel secured
Mwisho kabisa wale wanaokupenda jaribu kuwapa chance you never know
NB:kuna Dada mmoja alinizi urefu sana tena sanaaaaaaa ila ashawahi pigana na binti mwingine kisa mie halafu hata hatujadate or whatsoever .....alikua akiniona anapatwa na degedege ....na wapo wengi nliodate nao na ni warefu kuliko mimi na tukaachana kwa sababu za kijamii tofauti na kimo
LOVE YOURSELF AND FEEL CONFIDENT THAT'S HOW TO BE SEXY AND APPEALING
 
Kwa Kweli Hata Mimi .Niliwai kuwatakiwa Na MTU mfupiiiii .Hapana.Yupo vizuri..ana upendo wa dhati..Huruma..yaani vyooote unavyojua.But ufupii.Mpaka Leo Hajui kwa nini nilimkataa Na analaumu sana.
 
Back
Top Bottom