Kanikataa kwa sababu ya Ufupi...!!

Kanikataa kwa sababu ya Ufupi...!!

Habari za majukumu wanajukwaa..!

Rejea kichwa ahapo juu, Nimemtongoza kwa zaidi ya miaka miwili kanikataa kwa sababu tu niko mfupi., Ingawaje hata yeye sio Ngongoti.,,

Anasema eti itakua kituko siku ya harusi yeye akivaa michuchumio, itabidi nipande juu ya stuli kumchumu ...!! Maneno hayo yote kampa rafiki yake ambaye ni rfk yangu pia hajaniambia mimi direct..!!

Nilipoyaskia yakanitia kichefuchefu kabisa...!! Na kiukweli hii sio mara yangu ya kwanza kukataliwa na wanawake ingawa wengine hawaniambii sababu lkn nahisi kabisa ni hiyo....!! Ingawa wapo wanaonitaka ila mi siwapendi.

Jamani mnataka mi nikaoe Nyani..?? Umri wenyewe ndo huo, na sina mashaka na sura yangu ingawa mwanaume hasifiwi sura ila wengine wanaogopwa zipo kama Ismigo na ni wafupi...!!!

Naombeni ushauri wadau hivi hawa wanawake nifanyaje...?? Kama ni swaga zipo, sijawahi kua domo zege kabisa, ni mchangamfu sana.,

Pessa zipo ila Siwapi na siwaoneshi kama ninazo.....!! Nna uhakika mtaani kwetu hakuna mtu ananikaribia hata kwa kujikosha kwa mpunga ingawa mauzo sipendi kwa hiyo maisha yangu nayaweka kawaida sana si rahisi mtu mwngine kujua wa nje.....!!

Au wafupi haturuhusiwi Kuchagua...???


Dah pole mkuu,pambana utapat mwingine wako wengi tu
 
Back
Top Bottom