Kwa muda wa wiki moja na nusu sasa nimekuwepo hapa Arusha kwa ajili ya shughuli fulani na nimeshukia kwa rafiki yangu mmoja maene ya makao mapya. Katika nyumba hiyo ipo gari ndogo ya kukodi(tax) ambayo ina kibandiko (stika ) ya Dr Batilda Buriani, mgombea wa Ubunge Arusha kwa tiketi ya CCM. Ghafla yule dereve akaanza kukitoa kwa mkono na iliposhindikana alienda nda kuchukia kisu na kuanza kukwangua. Nilimuuliza swali moja, kwa nini unamtoa mama huyu, mbunge wetu mtarajiwa? Akajibu. .' Nimegundua mama huyu ni mzushi na mduwanzi, mama ni mjamzito, atatuongozaje watu wa Arusha?',(anatoa lafudhi ya vijana wa kiarusha)
Sasa mimi nikajiuliza, kumbe mama akiwa mjamzito hafai kuwa mbunge? Lakini baadae nikagundua si suala la ujauzuto tuu, mama huyu wengi wa Arusha hawamtaki kwa sababu zifuatazo
1. Wanasema hawawezi kuongozwa na mtu aliyeolewa zanzibar
2. wengi kutokana na athari za mila hawataki kuongozwa na mwanamke
3. Tatu kuna habari zinazosambazwa kwamba mama huyu hafai kwa sababu si mtu aliye na historia ya kuwasaidia watu kama lowassa, na kuna upepo flani tuu unaolenga kuonesha mama huyu hafai.
Chadema imekubalika sana Arusha kwa sasa, inaonesha kwa mtazamo kama vile watashinda, hata hivyo kelele za watu na wingi wa mashabiki si dalili kamili ya ushindi. Watu wa Arusha, hime, kama kweli mnataka mabadiliko, tar 31 fanyeni jambo, msiridhishwe na wingi wa bendera katika daladala na pikipiki.
NOTE TO CHADEMA
1. Juzi mlimwona shimbo alivyosema, damu haitamwagika maana ameskia kuna watu wanataka kukataa matokeo. Siku hiyohiyo Mh alisema damu haitamwagika,hayo alisema katika kampeni zake. why kauli moja siku moja na wakuu hao? was it coincidence? Na kwanini leo mnadhimu mkuu wa majeshi anazungumzia usalama wa wananchi na si mkuu wa polisi?
2. Yule mkurugenzi wa Arusha, aliyekuwa Arusha amehamishwa in 24 hrs, tena kapelekwa kigoma(if im not mistaken) na kupewa nafasi ndogo kuliko aliyekuwa nayo ARusha, u knw why? Tafakarini, Chukueni hatua