Siyo Kila Mtu Anadukuliwa, Jambo Hilo Hufanyika Maalum Pia Watu Hawajui Nini Maana Ya Kuyaweka Makampuni Sambamba.Kuna umuhimu wa kutoa elimu juu ya somo la udukuzi hapa JF..
Unalazimisha tufuate mawazo yako mkuu. Kuna una hisa huko?Ningekwambia ficha upumbavu wako kwa kukaa kimya lakini nimesita kufanya hivyo kwakuwa pengine hujalewa nilichoandika
KabaangExpress yourself.
halafu mpaka wasomi kabisa na akili zao, eti....wanaacha kutumia VODA!!! wakati ni mitambo ya TCRA na makampuni yote wanafanya hivyoWatanzania tusiwe na akili nyepesi kiasi hichi, Vodacom wamejipambanua jinsi wanavyolazimishwa kutoa siri za wateja wao, kosa lao kubwa sana ni kukubali kutoa mawasiliano kinyume na sheria ya nchi. Lakini je, mnajua mitandao ambayo haijatoa taarifa kama vile TIGO,ZANTEL,HALOTEL na AIRTEL ambao serikali ina hisa nyingi ina matatizo kiasi gani?
Tunapoulaumu mtandao ambao umekua huru kueleza masahibu unayopitia, kumbukeni kua kuna mitandao ambayo haijasema kitu. Kwa ujumla kupitia mazingira haya ya Vodacom ni lazima tuwe na hofu mitandao yote iliyopo nchini.
Kabsa hii itawafanya wengine wawe na akiliFaida ya kuhama VodaCome ni kwamba mitandao mingine itajifunza na itakuwa na woga wa kugawa mawasiliano ya watu! Simple like that man!!
Habari zenu wana wa nchi na poleni kwa majukumu mbali mbali ya ujenzi wa taifa.
Baada ya tafakuli ya kina juu ya tukio la kukamatwa Mwandishi Erick Kabendera jana na Kufungiwa huduma ya mawasiliano ya simu yake na Vodacom nimeoma kuna mambo kadhaa yana tia simanzi sana juu ya Usalama wa raia yeyote kwa sasa hapa nchini.
Mwandishi Erick Kabendera anasema alipoona Mawasiliano yake yamefungwa aliwapigia vodacom na kuwauliza kulikoni? Vodacom wakamjibu kuwa wameagizwa na TCRA wafunge mawasiliano yake. Lakini baadae TCRA ambao ndio wenye jukumu la usimamizi wa Mawasiliano wakakanusha kuwa hawahusiki na tukio hilo na wala sio kazi yao kufungia watu mawasiliano.
Majibu ya TCRA yanatupa maswali magumu juu ya Mtandao wa Vodacom kama ifuatavyo.
1. Kwa nini Vodacom wanawaficha wahusika halisi waliotoa amri ambayo kama waliona ni halali?
2. Lengo halisi la kufunga mawasiliano ya mwandishi ni nini? Ili akitekwa asipatikane hewani na kuwasiliana na ndugu zake?
3. Kama mtuhumiwa anatafutwa na chombo cha usalama SIMU yake ikiwa hewani husaidia chombo cha usalama kujua mahali alipo na kumkamata kirahisi. Sasa Hawa Vodacom kumzimia Simu mtuhumiwa anaye tafutwa wana LENGO gani?
4.Makosa anayotuhumiwa Kabendera hayahusiani na mambo ya Mawasiliano kwa nini Vodacom wamfungie huduma mteja wao ambaye amelipia huduma?
Maswali haya yanatuonesha Vodacom sio Mtandao salama tena kwetu watanzania. Unashirikiana na wahalifu, watekaji, wauaji, na watesaji hapa mchini.
Pili Vodacom wameonesha dharau kubwa sana kwetu watanzania. Kama wanaweza kukufungia Mawasiliano mtu ambaye huna hatia ili udhurike na watekaji watashindwa kuvujisha habari zako?
Je, Pesa zetu tunazo ziweka huko M.PE.SA ni salama tena? Huwezi amka ukaambiwa akaunti yako imefungwa na pesa zako zimechukuliwa kwa maagizo toka juu?
Kitendo hiki hakipaswi kufurahiwa. Vodacom wanapaswa kuchukuliwa hatua na sisi wenyewe wananchi ili kulinda usalama wetu na kuwaonesha kuwa tumefedheheshwa sana na tukio hili.
Hatua za kuchukua ni hizi wana bodi.
1. Kuacha kutumia mtandao wa Vodacom na mitandao mingine kama hiyo inayo shirikiana na waharifu kutesa raia wema.
Vodacom wamejidhihirisha pasi na shaka kuwa ni hatari kwa usalama wetu hima hima tuchukue hatua haraka.
Asanteni.
Natoa mtu mshipa[emoji35][emoji34][emoji35][emoji34]
tunahama kama huwezi hama wewe baki ili kuonyesha nguvu ya uma tunahama vodaNi wazi kampuni ya simu ya VODACOM inapitia kipindi kigumu na hii ni kutokana na tuhuma za kuruhusu mamlaka za nchi kudukua mawasiliano ya wateja wake.... Hili ni jambo baya na itawachukua muda kidogo mpaka kuja kukaa sawa tena.... Si kwamba watatetereka sana la hasha ila watu wengi watahoji umahiri na weledi wao kwenye kuhifadhi taarifa za wateja wao!
Kuna outrage kubwa kutoka kwa watu mbali mbali hasa viongozi wa kisiasa na watu wengine wa kaliba mbali mbali wakihamasisha watu waususie huu mtandao... Baadhi ya watu ni prominent figures ambao wana wafuasi wengi hivyo wanaisulubu VODACOM watakavyo....
Swali la kujiuliza.. Kwanini kadukuliwa Voda na si mitandao mingine....
Jibu ni kwamba si kwamba mitandao mingine ina kikubwa cha ziada na haiwezi kudukuliwa...
Kilichowaponza VODACOM ni uimara wa mtandao wake, huduma bora (mapungufu yapo) na kuweza kuhimili soko muda mrefu bila kuyumba wala kubadilibadili jina la biashara zaidi ya kubadili rangi na logo zake
Uimara wa vodacome na uhakika wa huduma zake.. Umevutia watu wengi prominent wakiwamo viongozi wa kaliba zote, watu maarufu na watu wa kawaida pia
Sinema za udukuzi zinazoendelea wateja wake wengi ni wa vodacome lakini si kwamba mitandao mingine haidukuliwi wala haidukuliki....
Tunaweza kufuata panic ya wanasiasa na kuususia mtandao wa vodacome... Lakini ni vema kumakinika ili usije ukajikuta unaruka mkojo na kukanyaga kinyesi.... Si vema kufuata mkumbo.. Hakuna mtandao ambao haidukuliki Tanzania....! Tusidanganyane kabisa... Maadui wa Voda na wenye chuki binafsi na huu mtandao wasikubebe kwenye mkumbo usiojua.... Ukitaka usidukuliwe tumia satellite mobile phones kama thuraya nk
Nitabaki VODACOM bado sijaona mbadala wake.... Huu ni upepo mchafu tu utapita... Mawasiliano yetu bado yataendelea kulindwa kwa kadiri inavyowezekana... Tunailaumu VODACOM lakini kamwe hatujariribu kujiuliza kama tungekuwa sisi kwenye nafasi yao tungefanyaje...
VODACOM client since 2000
hashtag boycottvodacomMi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
Kwa kuwa vodacom wameamua kutumia tabaka dhalimu la watawala badala ya kufanya biashara...
Na kwa kuwa vodacom wameamua kuwa sehemu ya mhimili huo wa uovu...
Na kwa kuwa sasa ni dhahiri wanashiriki kusaidia raia wema kufuatiliwa mawasiliano yao na kufanyiwa uhalifu na vyombo dhalimu vya dola...
Nimeamua kuungana na watanzania wazalendo walioamua kususia bidhaa za vodacom na hivi natangaza rasmi kuivunja vipande na kuichoma moto line yangu ya Vodacom ambayo nimekuwa nikiitumia tangu mwaka 2002.
Nimewaachia salio la Shilingi 0.56 kwenye akaunti yangu ya m'pesa...wale wafaidi.
May the unscrupulous and evil dogs of Vodacom go to hell and burn among the rocks!
Shubaaamit!