Bhaghosha
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 224
- 163
Kutenda KOSA si KOSA, KOSA ni kurudia KOSAWanabodi,
Nimesoma mahali kuhusu Kamanda Tundu Lissu kuandika barua mbili kwa IGP kuomba kuhakikishiwa usalama wake ndipo arejee nyumbani Tanzania.
Mkuu Joka Kuu, asante kwa taarifa hii ya Lissu kuandika barua kwa HIP, kuhakikishiwa ulinzi na usalama wake kwanza ndipo arejee home, nyumbani Tanzania.
Hatua hii ni nzuri na muhimu sana ili angalau Lissu na dereva wake warejee nyumbani ili sasa ndio vyombo vyetu vya uchunguzi ndipo vianze kazi uchunguzi ya kuwabaini wasiojulikana, waliomshambulia Lissu, maana tangu ameshambuliwa vyombo vya uchunguzi vilishindwa kufanya uchaguzi wowote hadi wamhoji Lissu na dereva wake.
Jeshi letu la polisi ni jeshi lenye utu sana, baada tuu ya shambulio, polisi waliarifiwa within minutes, na kutoka eneo la tukio na kituo cha polisi ni just 10 minutes drive kutoka kituo cha polisi hadi kwenye crime scene, lakini polisi walifika baada ya masaa 2, wakakuta Lissu ameisha kimbizwa Dodoma hospital na hawakukuta mtu mwingine yoyote aliyeshuhudia, wala hakuna hata mlio wa risasi uliosikika.
Licha ya shahidi muhimu wa tukio hilo, dereva wa Lissu kutojeruhiwa na alikuwa available siku nzima, ila polisi wetu walingia utu na ubinaadamu wa kutochukua maelezo ili kumpa nafasi shahidi kupumzika na kupumzisha mawazo, watamchukia maelezo wakati wowote kwani maelezo yana haraka gani kuchukuliwa mapema huku watu wana photographic memory hata baada ya miaka 3, watakumbuka every details hata tiny details.
Lissu na dereva wake walipokuwa Nairobi ambapo ni karibu, jeshi letu la polisi liliingia utu wa kutowahoji ili kusubiria wapone. Walipokwenda Belgium kufuatia kule ni ulaya, na rais Magufuli hapendi safari zisizo za muhimu, kwa vile uchunguzi huo sio muhimu na hauna haraka, jeshi letu la polisi lilingia tena huruma kuwaacha hadi wapone na kurejea nyumbani Tanzania ndipo liwahoji na uchunguzi ndipo uanze.
Hivyo sasa wanasubiriwa kwa hamu Tundu Lissu na dereva wake warejee nyumbani nchini Tanzania ndipo uchunguzi wa tukio lile uanze.
To be honest, baada ya mimi kuangalia ile hard talk ya BBC, nilisema hivi
Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela! - JamiiForums
Hivyo Kamanda Tundu Lissu, Karibu Sana Nyumbani, huna haja ya kusubiri majibu ya Kamanda Sirro kukuhakikishia ulinzi wako. Yule YEYE aliyekulinda na kukuepusha na kifo licha ya kupigwa risasi 16, ni ulinzi mzuri kuliko Vijana wa Siro.
Kuhusu wale wasiojulikana waliokushambulia, according to postulates na theories mbalimbali kuwahusu wasiojulikana hao, japo malengo yao kwako hayakutimia, lakini sasa hata ukirejea, wasiojulikana wale, hawawezi tena kuikamilisha tena kuikamilisha ile kazi kwasababu kazi nyingine ni kama uchawi, mchawi ukiisha mshtukia, hakulogi tena.
Hitimisho
Kwa maoni yangu, namshauri Kamanda Tundu Lissu, kama ni kurejea tuu nyumbani, arejee tu nyumbani Tanzania wala asisubiri jibu la barua zake kwa IGP kuhusu kumhakikishia usalama wake, kwasababu kwanza just his survival is beyond human beings ability and capabilities, its Devine intervention hivyo Aliyemlinda na shambulio lile baya la kutisha na kusikitisha hadi kubakia hai Yupo, Aliyesimamia matibabu akatibiwa hadi akapona Yupo, Aliyeyafanya yote hayo ni YEYE Aweza, na Ataendelea kumlinda, Usikute yote hayo Lissu anayopitia, ni mapito tuu ili YEYE kuonyesha Uweza Wake, hata katika ukombozi wa Ulimwengu huu, ni kwa Kupigwa Kwake, sisi tuliponywa, hivyo at this juncture, Tundu Lissu hatakiwi tena kuendelea kutegemea uwezo wa binaadam katika ulinzi wa uhai na usalama wake, amtegemee YEYE. Tundu Lissu Atamke maneno haya, "NAYAWEZA YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU"
Welcome Back Home, Kamanda Mdogo wangu Lissu (mimi ni kaka yake kule shuleni Ilboru)
Mwacheni Mungu Atwe Mungu
Welcome back home Kaka Mdogo Tundu Lissu.
Mimi Kaka yako Mkubwa
Karibu Nyumbani.
Paskali.