JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu ameeleza wapi alipo Dereva wake Adam Bakari ambaye alikuwa naye wakati aliposhambuliwa kwa kupigwa Risasi na watu wasijulikana mwaka 2017 Jijini Dodoma.
Akizungumza Leo mei 9,2023 Jijini Dodoma Lissu amesema Dereva wake yupo Ubelgiji alipatiwa hifadhi na Serikali ya Nchi hiyo.
Lissu amesema kipindi alipopata matatizo alienda na Dereva wake Nchini Ubelgiji.
Aidha Lissu amesema Dereva huyo anaendelea vizuri Nchini Ubelgiji na amepatiwa mafunzo ya Lugha na Serikali ya Nchi hiyo na kama kurudi hapa Nchini atarudi muda wowote kwani hapa ni Nyumbani.
Lissu ameongeza kwa kusema kuwa kama Serikali inamuhitaji Dereva huyo kwa ajili ya ushahidi kwa Jeshi la Polisi inabidi mwanasheria Mkuu wa Serikali aandike Barua kwa mwanasheria mkuu wa Ubelgiji ili kumwambia arudi hapa Nchini kwa ajili kutoa ushirikiano wa ushahidi.
Akizungumza Leo mei 9,2023 Jijini Dodoma Lissu amesema Dereva wake yupo Ubelgiji alipatiwa hifadhi na Serikali ya Nchi hiyo.
Lissu amesema kipindi alipopata matatizo alienda na Dereva wake Nchini Ubelgiji.
Aidha Lissu amesema Dereva huyo anaendelea vizuri Nchini Ubelgiji na amepatiwa mafunzo ya Lugha na Serikali ya Nchi hiyo na kama kurudi hapa Nchini atarudi muda wowote kwani hapa ni Nyumbani.
Lissu ameongeza kwa kusema kuwa kama Serikali inamuhitaji Dereva huyo kwa ajili ya ushahidi kwa Jeshi la Polisi inabidi mwanasheria Mkuu wa Serikali aandike Barua kwa mwanasheria mkuu wa Ubelgiji ili kumwambia arudi hapa Nchini kwa ajili kutoa ushirikiano wa ushahidi.