Kama una uwezo huu usikimbilie Majuu!

Kama una uwezo huu usikimbilie Majuu!

Ulaya haina kitu. Msibabaike na Ulaya watanzania. Wenyewe hivi sasa wana matatizo makubwa sana ya kiuchumi. Wananchi wao wako desperate. Europe na Amerika zimekumbwa na wimbi la watu kutaka utajiri wa haraka haraka bila kufanya kazi, matokeo yake ile spirit ya Innovation ambayo ilikuwepo katika nchi kama England karne ya 19 na 20 haipo tena. Waingereza wanapoteza kila kitu kwa Marehemu ya mahesabu pesa kwa kufungua mabanks. Hivi sasa yanawstokea puani.

Ndugu zangu watanzania nawaomba tuipende na kujivunia nchi yetu. Tusipende kuiga maisha ya wazungu. Wao wenyewe hawana mwelekeo hivi sasa. Sisi tufanye ya kwetu na tuchukue tu yale muhimu kutoka kwao.

Wazungu wamejiingiza wenyewe katika mitego ambayo hawawezi tena kujikwamua. Watakwamuliwa na mlipuko kwa sababu hayuko mtu ambaye yuko tayari kuachia anayo yafanya na faida aliyo pata.
Acha kusema uongo! Paragraph ndefuuuu lakini umeongea utumbo mtupuuu.
 
kama ni hivyo sawa ila ungeenda nae slow. maana maswali yako ni mazito kwa mfanya biashara yeyote
Nitajaribu, ila narudia, kwa uzoefu ngumu. Mkenya au Mganda angalau. Ndo maana,biashara nyingi mfano za Kikinga au Kichaga ni mtu na mkewe tuu. Akiweka mfanyakazi tuu, kwa heri, ngoma inarudi kati.
 
Ni masaa 8 mkuu sawa na USD 80 kwa siku, unafanya J3 hadi Ijumaa,unapokea 400usd sawa na 1600usd lakini sio chochote ughaibuni
Nani kasema?
Hivi ndivyo mnavyo ongopeana na waliokwenda bila mipango.
Wamefeli huko wanabaki kulalama nakusema ulaya hakulipi,
 
UK kima cha chini kabisa kumlipa mtu kwa saa ni £7... yaani hata mfagiaji tu analipwa hela hiyo...


ambapo kama mtu unafanya kazi masaa 8 kwa siku jumla ni £56

kwa week let say unafanya kazi siku 5 jumla ni £280

kwa mwezi ni £1120 ambapo kwa hela zetu ni above 3M.... hata kama kodi watamkata nusu ya hiyo 3M bado anabaki na hela nyingi sana....

Tell me mfagiaji bongo hii analipwa sh. ngap??? Bongo nyoso...

Utaspend maisha yako yote kunishawishi kwamba ni bora kubaki Bongo kuliko kuishi nje....
Muwe mnaachaga ujinga wa kudanganyana! Unajua hyo anaelipwa hyo pauni 7 apartment anayoishi analipa shi ngapi? Mwisho wa siku hyo mfagia barabara anaishi km mbangaizaji yoyote wa africa!!

Hyo paundi 1100 kibongobongo ni km kulipwa laki tatu kutokana na gharama za maisha kuwa juu
 
Muwe mnaachaga ujinga wa kudanganyana! Unajua hyo anaelipwa hyo pauni 7 apartment anayoishi analipa shi ngapi? Mwisho wa siku hyo mfagia barabara anaishi km mbangaizaji yoyote wa africa!!

Hyo paundi 1100 kibongobongo ni km kulipwa laki tatu kutokana na gharama za maisha kuwa juu
Hahahaha kweli huo mshahara itabidi wakati mwingine utembee kwa miguu kazini badala ya bus
 
Mi nishajiapiza siendi ulaya hta kwa kubebwa na greda! Now ulimwengu mzima unaliangalia bara la africa kwa matamanio makubwa kutokana na fursa ilizonazo cha kusikitisha vijana wa kiafrica wanataka kuacha fursa zilizopo africa wakatumikishwe kwenye kazi zenye maslahi madogo ..

Jamani vijana wenzangu amkeni hizi story za ulaya ni kudanganyana mwanzo mwisho
 
Hahahaha kweli huo mshahara itabidi wakati mwingine utembee kwa miguu kazini badala ya bus
Yaani wabongo full kudanganyana wanapigia hesabu mishahara ya ulaya kwa matumizi ya kibongobongo waende ulaya wakakutane na apartment ya chumba kimoja euro 2000 huku mshahara wako kwa mwezi ni euro3000 hpo bado hujala na takataka nyinginezo
 
Unakuta mtu anakataa kuosha vyombo tanzania , lakini akienda juu anaosha tena anakwangua na ukoko kabisa , tatizo huko juu pesa unaona kubwa ukibadili kuja pesa za kibongo lakini unashindwa kujua kua matumizi na gharama ya maisha huko iko juu sana pesa unayotumia juu kula , ukilinganisha na bongo ni pesa ya Msosi wa tajiri ,lakini huko unapata chakula kibovu tu , alafu code huko haukwepi na bills nyingi sana , kuna watu waliokwenda juu wakarudi wakijua watakuja kupagawisha hapa , wakakuta wa nyumbani wamefanya vitu kufuru , mpaka wakasema kwel huko wamekwenda kuzurura tu.
 
Yaani wabongo full kudanganyana wanapigia hesabu mishahara ya ulaya kwa matumizi ya kibongobongo waende ulaya wakakutane na apartment ya chumba kimoja euro 2000 huku mshahara wako kwa mwezi ni euro3000 hpo bado hujala na takataka nyinginezo
Maisha yamebadilika sana duniani sio kama zamani
At least upate kuanzia £30000 kwa mwaka ndio utaweza kuweka kidogo kutokana na maisha yalivyo na ukiwa na familia ya watoto hapo ni umaskini tu
 
Maisha yamebadilika sana duniani sio kama zamani
At least upate kuanzia £30000 kwa mwaka ndio utaweza kuweka kidogo kutokana na maisha yalivyo na ukiwa na familia ya watoto hapo ni umaskini tu
Hiyo £ 30000 kwa mwaka bado hela mbuzi tu kwa ulaya yote hyo inaishia kwenye kulipia apartment tu!
 
Hiyo £ 30000 kwa mwaka bado hela mbuzi tu kwa ulaya yote hyo inaishia kwenye kulipia apartment tu!
Hapana mkuu hapo sio kweli itakuwa umeamua kuishi nyumba ya posh
Kwa chumba kikubwa ni £400 average per month inc
Sasa kwa mwezi kama take home ni over 2000 bado una saving yako na sio hela ya mbuzi kama unavyofikiria

Kazi nyingi hata za elimu kuna wanaoanzia 22000 na wanaishi ingawa kwa kujibana
Anyway maisha ni kuchagua wapo wanaotengeneza zaidi nyumbani na wapo waliojiendeleza majuu pia all in all gurudumu linaenda au unaonaje mkuu
 
Sijakuelewa mkuu
Watu wanaoongelea USD 10 kwa saa, unaweza kuwasoma ukajiona kwa kipato chako umayapatia maisha, kumbe hata wewe uliyekizidi sana kiwango hicho una malengo zaidi pia.

Nakataa kukubali kazi wanazofanya wabongonje zina average hiyo.

Lakini, what do I know?

I got cribs in the hood, the 'burb and the city!
I run it like Diddy, with no commitee
Henny in the Hemi, smelling like Dylan Blue
With a lotta Benjis, and all te model type beaus
Every week is a taboo, of de ja vu
 
Watu wanaoongelea USD 10 kwa saa, unaweza kuwasoma ukajiona kwa kipato chako umayapatia maisha, kumbe hata wewe uliyekizidi sana kiwango hicho una malengo zaidi pia.

Nakataa kukubali kazi wanazofanya wabongonje zina average hiyo.

Lakini, what do I know?

I got cribs in the hood, the 'burb and the city!
Usd 10 kwa saa ni kiasi kikubwa sana
Bongo huo ni mshahara wa siku tatu
 
Usd 10 kwa saa ni kiasi kikubwa sana
Bongo huo ni mshahara wa siku tatu
Bora uzima kaka, Nyerere alitufundisha, utu wa mtu ni kazi, pesa ni matokeo.

Kuna watu wanatafuta sana hela, wanazipata, halafu zinawaua.

Bill Gates katafuta sana pesa, kapata mpaka anashindwa kuzihesabu, kila sikuwatu wanakadiria tu,utajiri wake hawawezi kuusema kwa kuupatia katikadakika yoyote maana unabadilikakila dakika kulingana an stock market.

Na kasema augawe, lakini ana tatizo la kuugawa kiufanisi, mpaka kaajiri watu wamsaidie kuugawa kiufanisi.
 
Usd 10 kwa saa ni kiasi kikubwa sana
Bongo huo ni mshahara wa siku tatu
Mwisho wa siku tujiulize! Hyo dola 10 kwa standard za america inaweza kumfanya mtu apige hatua? Au ndyo anakuwa msindikizaji tu!
 
Back
Top Bottom