Kama uliwahi tapeliwa njoo hapa

Kama uliwahi tapeliwa njoo hapa

Kutapeliwa kunauma jamani acheni! nawaoneaga huruma wanaotapeliwa papuchi alafu wanaambiwa nitakutumia Tgopessa doh wanaume muwe na huruma!Huu utapeli haujawahi kuwaacha salama wadada wa mujini hahahah
 
Kutapeliwa kunauma jamani acheni! nawaoneaga huruma wanaotapeliwa papuchi alafu wanaambiwa nitakutumia Tgopessa doh wanaume muwe na huruma!Huu utapeli haujawahi kuwaacha salama wadada wa mujini hahahah
Naona unatoa ushuhuda mkuu....enhee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka enzi hizo nimejichanga changa nikanunua cm yenye memory card, nikaenda kuingiziwa nyimbo. Muingiza nyimbo akasema nimpe 5000 aniwekee nyimbo kalii, enzi hizo utaratibu wa usb cable haukuwepo jamaa ikabd atoe memory card. Alivyomaliza akanirudshia cm huyoo nikarud zang home njiani ckutaka kuckliza nikihofia kupokonywa cm yangu na vibaka. Kufika hm cm haina memory card, nililia ck hiyo mpaka b.mkubwa akanionea huruma! Kurudi kwa jamaa nikakutana na sura tofauti na ya mwanzo.
 
Daah mi nilitapeliwa arusha maeneo ya stendi kuu. Nikiwa zangu natembea town jamaa mmoja akaniita, nilivyoenda akanambia eti kuna ujambazi umetokea njiro usiku na wao ni mapolisi kutokea dar wamekuja kufanya upelelezi wa kuwatafuta hao majambazi wakati anaendela kunambia ivyo akapita jamaa mwingine nae akamwita na kumwambia kama alivyoniambia mimi. Akatwambia wanachofanya wao ni kukagua hela na simu za watu wanaowahisi kwenye mashine yao km ndio zilizoibiwa.
Akamwambia yule jamaa aliyemwita baada yangu ampe simu yake na waleti akazicheki kwenye mashine akazunguka kwa nyuma kidogo akaingia kwenye nyumba fulani ivi baada ya kama dakika 5 akarudi akamwambia vitu vyako vipo salama hausiki, nenda zako. Ikaja zamu yangu nikampa kisimu changu cha G Tide na buku mbili akaenda kuzicheki kwenye mashine. Nilimsubir km dakika 15 mtu akurudi ndo akili zikanirudia kuwa hapa nimeshatapeliwa. Aise nilizunguka stendi nzima kumtafuta yule jamaa adi kidogo nigongwe na gari kwa stress za kutapeliwa.
Hahahahahahaha mkuu hao wapumbavu walinitokea Iringa mida ya saa 1 unusu wanadai mauaji yametokea mitaa ya Frellimo wao ni wapelelezi hahahahaha nikawaambia so mnataka nini kwangu wakasema wanatafuta muuaji nikadakia kama na uwezo wa kuua ntaanza na ninyi nikajua hawa ndo walewale nikawaambia mimi nimekaa kwa wahuni chuga nikashika kiuno nikawaangalia weeeee wakasepa wenyewe hahahahahaah nikavuka barabara nikasepa zangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutapeliwa kunauma jamani acheni! nawaoneaga huruma wanaotapeliwa papuchi alafu wanaambiwa nitakutumia Tgopessa doh wanaume muwe na huruma!Huu utapeli haujawahi kuwaacha salama wadada wa mujini hahahah
Mm nakutumia kweli sikutapeli iyo papuchi yako
 
Ndio lilikuwa jaribio langu la kwanza tangu kuzaliwa toka hapo sijawahi kutapeliwa tena labda mtu kunikopa na kushindwa kunilipa!
Mwaka jana nilipita kariakoo mara akaniita mpiga viatu rangi akaniambia brother nina rangi OG ya viatu vyako vilikuwa viko poa havihitaji rangi nikaona poa ngoja nimpe avipake rangi apate naye riziki akaanza kupaka brush ya kwanza akaniambia brother hii rangi ni ya ghali sana hazipatikani hivi hivi!!! Nikamuuliza leo lini akaniambia hujuwi ata leo ni lini ! Nikamwambia sijuwi kweli akaniambia leo juma pili nikasema afadhali nilijua leo j3 nina hitajika mahakamani nina kesi ya kuuwa nimekaa ndani miaka 3 nimetoka juzi tu !!
Nikamuliza itakuwa jumla shilingi ngapi akasema kila brush moja 500 nikamuuliza ushapaka ngapi akaniambia kumi nikamuambi acha hapo hapo usije nifanya nikarudi gerezani kwa kesi nyingine inayo fanana nina buku tu hapa!! Aksema ninakudai 5,000 nikamwambia kama hujuwi kifo katizame kaburi usiongeye neno jingine huyo nikasepa zangu!!!!!
I like tanzanian a lot

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tupe hata kwa ufupi kwani utasaidia wengine watu watajifunza. Please fanya hivo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanza nikiri kuwa ujinga wangu na pupa yangu ndio vimechangia kwa asilimia kubwa kuingizwa mjini kiasi hicho.

Kipindi hicho ndio naanza chuo mwaka wa kwanza, nilipata boom nikiwa nimechaguliwa kusoma koz ya Afya. Boom kwa wanafunzi wa kozi za Afya ni kubwa kuliko la waafunzi wa kozi ambazo sio za afya.

Nilifanya hatua zote za usajili chuoni na kufungua account ya CHAP CHAP (NMB) kwa ajili ya kuwekewa boom. Sasa baada ya hapo nikawa nasubiri boom liingie nianze kuonja mkwanja wa serikali. Boom lilipoingia rafiki yangu akanishtua kwa simu mida ya usiku akaniambia mpunga ndani ya kikapu, moyo ukashtuka paaa!! Nikasema asubuhi nitaenda kudrawal laki 2 kwanza nikafanyie shopping na mazagazaga mengine ya chuo.

Wakati kabla nasubiri boom liingie nilijaribu kufanya practice ya kutumia ATM lakini ilikuwa ni juu sana.
Kesho yake asubuhi na mapema saa 12 kasoro mwanaume nikatinga ATM pale Ubungo Shell, nilipofika tena kwa shauku kwenye hiyo ATM ambayo ilikuwa na sehemu tatu za kutolea hela nilikuta kuna jamaa anatoa hela kwenye tundu moja lilikuwa ndani kidogo halafu mengine mawili yapo kwa mbele, mimi nikaenda kwenye haya matundu ya mbele ambapo moja lililkuwa halifanyi kazi na maelezo yalikuwa yameandikwa pale kwenye kioo kuwa haifanyi kwa muda huo.

Bila kukawiwa nikaingiza card yangu ya Chap Chap kabla sijaanza kuandika neno la siri yule jamaa ambaye alikuwa kwenye tundu la ndani akaja fasta na kubonyeza kitufe chakusitisha process za kutumia ATM halafu kadi ikarudi na akaishika huku akiniambia hii haifanyi kazi njoo huku kwenye tundu ambalo alikuwa anatolea yeye, na nikifikiria jinsi kadi ilivyorudi fasta bila kujua kuwa ndio yeye kairudisha nikaamini na akiwa ameishikilia kadi yangu tukaongozana hadi alipokuwa anatolea pesa na akaingiza card fasta bila mimi kugundua kuwa kanibadilishia kadi na kaingiza fake. Akaniambia(huku amesimama pembeni yangu kwa nyuma kidogo) weka namba ya siri. Nilipoingiza namba zikasomeka live bana tofauti na kawaida ambapo zinaonesha ****, kumbe kazikariri fasta na akabonyeza OK mashine ikaniambia weka namba ya siri ya mtu aliyekutumia pesa(hapo nikapigwa shot kwanza), akaniambia iweke sasa hiyo namba nikamwambia siijui, kumbe kitendo cha kubonyeza fasta fasta ilikuwa mbinu ya kunipoteza alipoona nishapotea halafu tayari namba ya siri kaiona kasepa na kuniacha nikiwa nang'ang'ana na mashine.

Baada ya kuona jambo limenigomea nikaamua nijaribu kuitoa kadi ikagoma, ghafla mashine ikaanza kupiga kelele, daahh! Kumbe ile kadi ambayo ilikuwa fake imeshamezwa. Nikamfuta mlinzi nje nikamueleza tatizo nikmuomba anisaidie kuitoa kadi, alipoenda kuangalia akaniambia ishamezwa hiyo, pia akaniuliza kama kuna mtu alikuwepo na amejaribu kunisaidia nikakiri nikamueleza movie ilivyokuwa. Akanishauri niende Mlimani city ifikapo saa mbili nikasaidiwe kuhusu hilo tatizo, ilipofika saa mbili tayari nilikuwa nishafika hapo Mlimani city nikawaona wahusika pale nikaeleza mkasi ulivyokuwa halafu nikawapa account namba wakacheki tukakuta jamaa kashajizolea mzigo kitambo(yaani baada ya nusu saa aliponiibia kadi) halafu kanibakishia buku 8 tu.

Sikuwa na ujanja zaidi na nguvu za kufuatilia zikawa zimeniishia nikabaki naugulia maumivu ya hatari sana maana boom limesepa lote.

Aisee huo mkasa sitausahau labda utokee mwingine wa kureplace
 
Back
Top Bottom