Agogwe
JF-Expert Member
- Feb 20, 2013
- 2,745
- 2,988
ni kweli kabisa mkuuNi wazi kuwa ofisi ya Dpp inatumika kisiasa na haifanyi kazi zake kwa weledi.
Kama watuhumiwa wa makosa ya kijinai wanaachiwa ili kufurahisha umma ni jambo baya sana kwa muktadha wa taifa letu.
Watuhumiwa wa ugaidi walikabiliwa na makosa mabaya sana. Mbaya zaidi waziri wa mambo ya ndani wakati huo Emmanuel Nchimbi alipointi wazi kuwa walihusika na umwagiaji watu tindikali huko Zanzibar.
Mimi binafsi nina hakika kuwa Emmanuel Nchimbi alikuwa na info za kutosha na za ukweli.
Ok achana na watuhumiwa wa ugaidi, kuna wapigaji na wabadhirifu nao wanaachiwa ili kufurahisha umma.
Hii ni hatua mbaya sana kwa taifa letu. Na haifai maana ni kama kukubaliana na kuunga mkono uhalifu
Zaidi, soma mijadala hii:
1) Uamsho wakana kuhusika na vurugu za Zanzibar
2) CCM yataka Uamsho Zanzibar ifutwe; Yataka Waziri wa Sheria ajiuzulu
3) Mahojiano Ya Mwandishi Jackton Manyerere Na Wana- Uamsho Zanzibar