Ajaye baada ya Rais Samia kumaliza miaka yake kumi ya uongozi atakuwa na kazi nyepesi sana ya kuongoza Taifa letu

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,264
9,715
Ndugu zangu Watanzania,

Rais atakayepokea madaraka kutoka kwa Rais samia baada ya kukamilisha miaka yake kumi madarakani kwa mujibu wa katiba yetu atakuwa na kazi nyepesi sana ya kuliongoza Taifa letu, kwa kuwa atakuta kazi kubwa ya kujenga misingi ya uchumi wa Taifa letu imeshafanywa na kuwekwa na Rais wetu mama Samia.

Atakuta miuondombinu Bora na imara ya Barabara imejengwa kila kona ya Taifa letu ambayo itachochea usafiri na usafirishaji wa mazao mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali nchini kwenda sokoni na sehemu mbalimbali.

Ajaye atakuta Rais samia Amemsafishia njia katika mahusiano ya kimataifa ambapo Taifa letu litaendelea kupokea mafuriko ya wawekezaji, watalii na wafanyabiashara wakubwa kutoka kila pembe ya Dunia. Atakuta mapato yetu ya kila mwezi na mwaka yanaendelea kuongezeka kutokana na kuwa na wigo mpana wa kodi kutokana na kuwa na wawekezaji wa kila aina na biashara mbalimbali nchini pamoja na miradi mbalimbali ya kimkakati itakayoendelea kuleta faida katika Taifa letu.

Ajaye atakuta hali nzuri ya usalama nchini, ujirani mwema, umoja wa kitaifa, mshikamano na uzalendo wa dhati mioyoni mwa watanzania, atakuta Taifa ambalo watu wake wapo imara kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja.

Atakuta huduma bora za kijamii zilizo bora na kuboreshwa kwa kiwango cha juu,atakuta watumishi wa umma wenye morali ya kazi na wenye kujituma makazini na kuleta matokeo chanya kutokana na maslahi mazuri wanayolipwa.

Ajaye atafanya kazi ya kuendeleza tu pale alipoishia Rais samia na kufanya maboresho kiasi ya kisera na kisheria kulingana Na wakati husika wa kuendana na mabadiliko na kasi ya ulimwengu kiuchumi na kiteknolojia. Ajaye atakuta mifumo mizuri ya kisheria katika kuongoza nchi, atakuta Taasisi imara zenye kufanya kazi kwa weledi, uadilifu pasipo kusukumwa au kusimamiwa au kumtegemea mtu mmoja pekee.

Ajaye atakuta Taifa lililo shamiri na kuchanua kwa Demokrasia na uhuru wa kuwawezesha watu kutoa mawazo yao katika ujenzi wa Taifa letu. Atakuta Taifa lenye amani na utulivu na lenye utayari wa kufanya kazi kwa uzalendo na moyo wa uzalendo.

Kwa hakika ajaye baada ya miaka kumi ya Rais samia madarakani atakuwa na kazi ndogo sana na Nyepesi sana katika kuliongoza Taifa letu kwakuwa kazi kubwa Imefanywa na inaendelea kufanywa na Rais samia wakati huu ambao anafanya kazi usiku na mchana pasipo kupumzika na ndio maana tunaona akifanya kazi hata akiwa ndani ya ndege ili kuhakikisha kuwa Taifa linasonga mbele kwa kasi kubwa sana.

Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais atakayepokea madaraka kutoka kwa Rais samia baada ya kukamilisha miaka yake kumi madarakani kwa mujibu wa katiba yetu ,Atakuwa na kazi nyepesi sana ya kuliongoza Taifa letu,Kwa kuwa atakuta kazi kubwa ya kujenga misingi ya uchumi wa Taifa letu imeshafanywa na kuwekwa na Rais wetu mama Samia. Atakuta miuondombinu Bora na imara ya B

0742-676627.
Shetani ,mungu chukua huyu shetani haraka
 
Ajaye atakutana na mzigo mzito wa Madeni ya Nje na Ndani.
Hakuna kitu cha namna hiyo .Rais wetu ameongeza Makusanyo ya ndani ambayo yanatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo.lakini pia inapolazimika kuchukua mikopo serikali yetu inazingatia sana aina ya mkopo,masharti ya mkopo,muda wa kuanza kurejesha au kulipa mkopo,riba yake pamoja na mambo mengine ambayo hayawezi kuathiri maslahi yetu ya Taifa.
 
Hakuna kitu cha namna hiyo .Rais wetu ameongeza Makusanya ya ndani ambayo yanatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo.lakini pia inapolazimika kuchukua mikopo serikali yetu inazingatia sana aina ya mkono,masharti ya mkopo,muda wa kuanza kurejesha au kulipa mkopo,riba yake pamoja na mambo mengine ambayo hayawezi kuathiri maslahi yetu ya Taifa.
Unaweza kutoa mifano miwili ya hizo mikopo unayosema oliyochukuliwa na serikali?
 
Hakuna kitu cha namna hiyo .Rais wetu ameongeza Makusanya ya ndani ambayo yanatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo.lakini pia inapolazimika kuchukua mikopo serikali yetu inazingatia sana aina ya mkono,masharti ya mkopo,muda wa kuanza kurejesha au kulipa mkopo,riba yake pamoja na mambo mengine ambayo hayawezi kuathiri maslahi yetu ya Taifa.
Tanzania's national debt has hit $39,006.1 million (Sh91. 01tr), a monthly increase of $544.8 million, the central bank's monthly economic review reveals. At the end of October 2022, external debt accounted for Sh64 trillion, or 70.5 percent of total debt, while internal debt accounted for Sh26. 6 trillion.10 Dec 2022

Source: The Citizen
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais atakayepokea madaraka kutoka kwa Rais samia baada ya kukamilisha miaka yake kumi madarakani kwa mujibu wa katiba yetu atakuwa na kazi nyepesi sana ya kuliongoza Taifa letu, kwa kuwa atakuta kazi kubwa ya kujenga misingi ya uchumi wa Taifa letu imeshafanywa na kuwekwa na Rais wetu mama Samia.



0742-676627.
uko rada sana komred.
Yaani kila eneo huyu muMama amagusa,
baada yake, ajaye ni kupapasa tu mambo yanaenda sawa sawia
 
uko rada sana komred.
Yaani kila eneo huyu muMama amagusa,
baada yake, ajaye ni kupapasa tu mambo yanaenda sawa sawia
Kwa hakika mh Rais amefanya kazi kubwa sana ndani ya muda mfupi wa uongozi wake,kazi ambazo zitabakia kama alama na kukumbukwa kwa miaka mingi sana ijayo. Ameleta mageuzi makubwa sana ya kiuchumi kisera na kisheria ambayo imekuwa chachu ya kasi ya maendeleo ya Taifa letu.
 
Atakua na kazi kubwa sana kurudisha rasilimali zetu na kuvunja mikataba ya kimangungo.

1. Bandari
2. Misitu
3. Loliondo
4.
6.
7.
Rasilimali zetu zipo salama katika mikono salama ya Rais wetu mzalendo wa kweli Mama Samia Suluhu Hasssan,Na zinaendelea kutumika kwa ustawi wa Taifa letu.
 
Back
Top Bottom