Kama sielewi elewi vile!

Kama sielewi elewi vile!

Yaani misiba ya siku hizi wengine wanaenda kuuza sura,kupata wachumba na mengineyo
Sidhani kama unauchungu na ndugu yako bado unapata nguvu ya kuingia saloon
Ooh my god inachosha sana mambo ya kizazi hiki
 
yaani misiba ya siku hizi wengine wanaenda kuuza sura,kupata wachumba na mengineyo
sidhani kama unauchungu na ndugu yako bado unapata nguvu ya kuingia saloon
ooh my god inachosha sana mambo ya kizazi hiki
ukute ni mume kafa unakuta mama kashonea bonge la weaving hadi kope kabandika jamani..eti mahawara wa mume wa mkome
 
Watu mpaka wanatengeneza matisheti, kanga n.k

ukitokea msiba wa ndugu watu wanawahi tenda.... Chezeiya kifo wewe, wengine ndo muda wao wa kutengeneza pesa!
 
We acha tu! Ila baada ya kuhudhurua misiba mbalimbali nikaja kujua imekuwa kama utamaduni kwa kabila flani kuendesha misiba kizungu zaidi. Pamoja na hayo huo uzungu umenipita mbali.
kuna vitu ni muhimu sana vikupite.....
siyo kila kitu cha kuigwa.....
yaani hapa hata afe babu yangu sidhani kama naweza kwenda kusuka, kama limenikuta na mabutu basi ndo nitazika nayo
 
Yaani misiba ya siku hizi wengine wanaenda kuuza sura,kupata wachumba na mengineyo
Sidhani kama unauchungu na ndugu yako bado unapata nguvu ya kuingia saloon
Ooh my god inachosha sana mambo ya kizazi hiki
bora ambao siyo wahusika utasema wanaenda kutafuta wachumba, lol!
msibani kuna kila mtu, tofauti na kwenye sherehe hadi ualikwe...
sasa kuona mtoto wa marehemu kabandika kope ndo akamzike mamake kwangu naona ni uchuro, lol!
 
ukute ni mume kafa unakuta mama kashonea bonge la weaving hadi kope kabandika jamani..eti mahawara wa mume wa mkome
ha haaa, kuna siku dada mmoja aliyekuwa mke wa tajiri mmoja alikufaga niliona akihojiwa kwenye tv kuhusu mumewe, atamkumbuka kwa yapi.....
hapo mwili wa mumewe bado haujazikwa, watu wapo nyumbani kwa maombolezo......
mdada (mjane) kajipodoa balaa, ndo anaongea kwa kweli I will miss him, he was a lovely husband......... bado kidogo nizimie, lol!
 
Watu mpaka wanatengeneza matisheti, kanga n.k

ukitokea msiba wa ndugu watu wanawahi tenda.... Chezeiya kifo wewe, wengine ndo muda wao wa kutengeneza pesa!
ha haaa, cc. King'asti.....
best itabidi unifunze ujasiriamali huu
 
Last edited by a moderator:
Naona siku hizi hakuna upendo
Kama maandiko matakatifu yanavyosema
"siku za mwisho upendo wa wengi utakoma"
nakubaliana na wewe rafiki
upendo ukipungua hata ku-feel kuwa huyu mtu ndo kaondoka na hatarudi tena kunapungua. unaona kila kitu poa tu
 
Juzi nilikuwa namtafuta shosti kwa dharura, akaniambia yupo salon anasuka, akanielekeza nikaona nimfwate....
wakati tunaongea, kulikuwa na mrembo mmoja pembeni anashonea weaving na kutengenezwa kucha, kope, nyusi, n.k.
mara simu ya mrembo ikaita, maongezi yakaanza..... "yaani we acha tu, ndo mambo ya dunia lakini, Tunamshukuru Mungu..... asante sana....
tunaaga kesho mchana na safari ya kwenda Moshi kwa mazishi itaanza baada ya kuaga, kweli tutammiss sana kaka yetu....."
baada ya hapo maongezi yakawa yanaendelea akawa anasimulia kuwa kakake kabisa kafariki, kaumwa siku 2 tu kafa.....
sijui ndo ukijijini au ushamba wangu! kweli nilisikitika sana.....
sipati picha kakangu anafariki, mimi naweza kuwa na nguvu kwenda salon kujipiga msasa ili niende kuzika kakangu au ndugu yangu wa karibu.
Nikajiuliza mambo mengi sana.
1) ni kwamba watu siku hizi wamezoea sana misiba kiasi kwamba wanaona ni kitu cha ajabu tu kufiwa?
2) watu hatuna uchungu tena na ndugu zetu?
3) u-kisasa unatufanya tuwe hivyo?
kweli mahusiano na ndugu/jamaa/marafiki yamepungua kiasi hiki mpaka tunachukulia misiba ya ndugu zetu kirahisi namna hii?
Alikuwa hapatani na wifi yake, sasa kafurahia yaliyomkuta wifi yake.Anasubiri aone wifi yake alivyokuwa na maringo atajivunia nini baada ya hapo.Women bwana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
ha haaa, cc. King'asti.....
best itabidi unifunze ujasiriamali huu

Tena unaenda kununua kanga zenye maneno haya "DAIMA TUTAKUKUMBUKA" Kisha unaibuka nazo msibani ukidai ndio sare, unanunua kwa Tsh. 3,000/- then unauza kwa Tsh. 5,000/- Imagine umenunua piece 50 utakuwa na faida ya Tsh. ngapi hapooo????????
 
Last edited by a moderator:
si utaje hayo makabila bwanaaa WACHAGA NA WAHAYA
Kwa Wachaga siwezi kukataa.Nakumbuka siku moja tukiwa tunatoka mochwari ya KCMC jamaa mmoja wa marehemu alituzuia tusiweke jeneza kwenye Toyota Pick up, Tusubiri alete meza kubwa, then tuifunike na kitambaa, then Jeneza ndiyo liwekwe kwa juu.
Nikamuuliza kwanini tufanye hivyo, akanijibu "ili yule anaye record VIDEO aweze kuchukua picha nzuri kabisa".Strange!!!!!!!!!!
Marehemu alikuwa ni mtu mwenye pesa nyingi, hata jeneza lake lilinunuliwa Nairobi badala kuchukua yale ya pale karibu na KCMC.
Na kwenye mazishi every one was happy, except his wife and Children.
 
Misiba siku hizi imegeuka kuwa sherehe wala usishangae tena "tena utasikia hii ndio sherehe ya mwisho ya marehemu" jamani wee kwani alipokuwa hai huyo marehemu hakuwahi kufanyiwa sherehe?? kha! tumrudie mungu jamani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom