Kama sielewi elewi vile!

Kama sielewi elewi vile!

Juzi nilikuwa namtafuta shosti kwa dharura, akaniambia yupo salon anasuka, akanielekeza nikaona nimfwate....
wakati tunaongea, kulikuwa na mrembo mmoja pembeni anashonea weaving na kutengenezwa kucha, kope, nyusi, n.k.
mara simu ya mrembo ikaita, maongezi yakaanza..... "yaani we acha tu, ndo mambo ya dunia lakini, Tunamshukuru Mungu..... asante sana....
tunaaga kesho mchana na safari ya kwenda Moshi kwa mazishi itaanza baada ya kuaga, kweli tutammiss sana kaka yetu....."
baada ya hapo maongezi yakawa yanaendelea akawa anasimulia kuwa kakake kabisa kafariki, kaumwa siku 2 tu kafa.....
sijui ndo ukijijini au ushamba wangu! kweli nilisikitika sana.....
sipati picha kakangu anafariki, mimi naweza kuwa na nguvu kwenda salon kujipiga msasa ili niende kuzika kakangu au ndugu yangu wa karibu.
Nikajiuliza mambo mengi sana.
1) ni kwamba watu siku hizi wamezoea sana misiba kiasi kwamba wanaona ni kitu cha ajabu tu kufiwa?
2) watu hatuna uchungu tena na ndugu zetu?
3) u-kisasa unatufanya tuwe hivyo?
kweli mahusiano na ndugu/jamaa/marafiki yamepungua kiasi hiki mpaka tunachukulia misiba ya ndugu zetu kirahisi namna hii?
technology is cool.
 
Sasa hata akijigalagaza kwa kulia kaka yake harudi.

Tunajali sana misiba (raia mpaka rais) wakati mtu yupo hai hatujali vya kutosha.

Pengine hana hela ya nauli na kwa kufanya kazi anaongezea nauli na ubani.

Nyie mnafikiri kila mtu ana luxury ya kulia?
 
Sasa hata akijigalagaza kwa kulia kaka yake harudi.

Tunajali sana misiba (raia mpaka rais) wakati mtu yupo hai hatujali vya kutosha.

Pengine hana hela ya nauli na kwa kufanya kazi anaongezea nauli na ubani.

Nyie mnafikiri kila mtu ana luxury ya kulia?
soma mada vizuri rafiki
huyu alienda salon kujipamba siyo kufanya kazi.
hatujaongelea kulia hapa, kulia ni fani za watu..... tunaongelea nduguyo kafa wewe unaenda kujipendezesha ili uende msibani
 
soma mada vizuri rafiki
huyu alienda salon kujipamba siyo kufanya kazi.
hatujaongelea kulia hapa, kulia ni fani za watu..... tunaongelea nduguyo kafa wewe unaenda kujipendezesha ili uende msibani

Wengine kujipamba ni sehemu ya kazi.

Anajipamba kisha anaenda kazini kukusanya nauli akiwa presentable.

Kwa hiyo mtu akifiwa kujipamba mwiko?

Au tushazoea msiba kwa formula, kila mtu awe mnyooonge? Unajuaje kama huyo kaka yake kaacha maagizo msiba wake hataki unyonge anataka watu wafurahie maisha yake?

Mimi msiba wangu -kama kutakuwa na msiba- kulia ni waste of energy, kutojiweka presentable eti kwa sababu ya msiba ni ushamba tu.

Bottom line, do you.

Humjui mtu, hujui historia yake, hujui alikuwa karibu kiasi gani na marehemu, utampangiaje msibani aende vipi?

Wabongo wengine tumezidi kupangiana maisha.
 
Wengine kujipamba ni sehemu ya kazi.

Anajipamba kisha anaenda kazini kukusanya nauli akiwa presentable.

Kwa hiyo mtu akifiwa kujipamba mwiko?

Au tushazoea msiba kwa formula, kila mtu awe mnyooonge? Unajuaje kama huyo kaka yake kaacha maagizo msiba wake hataki unyonge anataka watu wafurahie maisha yake?

Mimi msiba wangu -kama kutakuwa na msiba- kulia ni waste of energy, kutojiweza presentable eti kwa sababu ya msiba ni ushamba tu.

Bottom line, do you.

Humjui mtu, hujui historia yake, hujui alikuwa karibu kiasi gani na marehemu, utampangiaje msibani aende vipi?

Wabongo wengine tumezidi kupangiana maisha.
asante kwa bottom line.....
noted!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom