Kama sielewi elewi vile!

Kama sielewi elewi vile!

Alikuwa hapatani na wifi yake, sasa kafurahia yaliyomkuta wifi yake.Anasubiri aone wifi yake alivyokuwa na maringo atajivunia nini baada ya hapo.Women bwana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
sikutegemea hili jibu....
yaani sababu sipatani na wifi yangu ndo sina uchungu kakangu kufa? who is wifi anyway...... leo anaweza akawa na kaka kesho asiwe naye, lakini my kaka atabaki kuwa pale
 
Tena unaenda kununua kanga zenye maneno haya "DAIMA TUTAKUKUMBUKA" Kisha unaibuka nazo msibani ukidai ndio sare, unanunua kwa Tsh. 3,000/- then unauza kwa Tsh. 5,000/- Imagine umenunua piece 50 utakuwa na faida ya Tsh. ngapi hapooo????????
ha haaa, hiyo kiboko.... mujini mipango, lol!
 
Kwa Wachaga siwezi kukataa.Nakumbuka siku moja tukiwa tunatoka mochwari ya KCMC jamaa mmoja wa marehemu alituzuia tusiweke jeneza kwenye Toyota Pick up, Tusubiri alete meza kubwa, then tuifunike na kitambaa, then Jeneza ndiyo liwekwe kwa juu.
Nikamuuliza kwanini tufanye hivyo, akanijibu "ili yule anaye record VIDEO aweze kuchukua picha nzuri kabisa".Strange!!!!!!!!!!
Marehemu alikuwa ni mtu mwenye pesa nyingi, hata jeneza lake lilinunuliwa Nairobi badala kuchukua yale ya pale karibu na KCMC.
Na kwenye mazishi every one was happy, except his wife and Children.
ha haaa hiyo kali.....
show kila mahali, lol!
 
sikutegemea hili jibu....
yaani sababu sipatani na wifi yangu ndo sina uchungu kakangu kufa? who is wifi anyway...... leo anaweza akawa na kaka kesho asiwe naye, lakini my kaka atabaki kuwa pale
Ungeongea naye muda mrefu ungepata sababu ya furaha yake.Na sio ajabu angetoa sababu ambayo ingekufanya utamani kumkimbia
 
Misiba siku hizi imegeuka kuwa sherehe wala usishangae tena "tena utasikia hii ndio sherehe ya mwisho ya marehemu" jamani wee kwani alipokuwa hai huyo marehemu hakuwahi kufanyiwa sherehe?? kha! tumrudie mungu jamani.
watu huwa tunalia sababu tunajua huo ndo mwisho wa kuonana naye, yaani kitendo tu cha kuwaza kuwa huyu mtu ndo sitamwona tena hali inakuwa mbaya....
haya kwenda kujipamba hiyo nguvu unatoa wapi?
 
Ungeongea naye muda mrefu ungepata sababu ya furaha yake.Na sio ajabu angetoa sababu ambayo ingekufanya utamani kumkimbia
sikuweza hata kumwuliza swali moja......
maana na ushamba wangu naona angeweza kuniona mimi nimetoka namabengo jana na kuanza kunipasha habari za mujini
 
Sio kanga tu.siku hizi tunapewa T-shirt zenye Picha ya marehemu kwa shs.10,000.Sijui baada ya mazishi zinapelekwa wapi. sijaona anayezivaa mjini.
kuna mdada wangu wa kazi niliamua kumpeleka sekondari, huko kuna rafiki yao alifariki, basi wakajinunulisha hizo tisheti za "tutakukumbuka fulani........". mi naona huwa anaivaa pale home ila sijawahi ona akitokea nayo
 
ha haaa, kuna siku dada mmoja aliyekuwa mke wa tajiri mmoja alikufaga niliona akihojiwa kwenye tv kuhusu mumewe, atamkumbuka kwa yapi.....
Hapo mwili wa mumewe bado haujazikwa, watu wapo nyumbani kwa maombolezo......
Mdada (mjane) kajipodoa balaa, ndo anaongea kwa kweli i will miss him, he was a lovely husband......... Bado kidogo nizimie, lol!
namjua sana hata binti yake alihojiwa..pale walilipia na airtime si mangi yulee alikufa ghafla?
 
Heri sisi kijijini mtu akifa ni gubigubi khanga kichwani hata kuona macho ni shughuli sembuse nywele za saloon thubutu...ni kwetu tu lakini kwikwikwi!!!!!!.
siyo kwenu tu, hata kwetu.....
ila sisi kujifunika gubigubi labda kama ndo mjane, lakini kama ndugu wengine ni ushungi tu
 
yaani kama msiba ni wa ndugu wa mbali lazma utakumbuka kujiremba ila wakwako si ajabu hata kuoga ukasahau.
 
yaani kama msiba ni wa ndugu wa mbali lazma utakumbuka kujiremba ila wakwako si ajabu hata kuoga ukasahau.
umeona eeeh!
nilipopigiwa simu baba amefariki nilikuwa ofisini....... bahati nzuri nilikuwa na mkaka mmoja hivi.......
yeye ndo alikumbuka kuzima laptop yangu na kunibebea handbag kunirudisha home maana naona alihisi drama inaweza tokea...... nilichokuwa nawaza ni ntafikaje huko muda huo huo, angalau kuwa pamoja na mama na wadogo zangu tukilia pamoja kutanipa faraja........ hapo unafikiri kuna kuwaza kama nina mtoto? nilikumbuka baadae dada aliponiletea nimnyonyeshe, lol! nini kukumbuka kujipamba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom