Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,242
lol...niko off-topic kidogo hapa mkuu nisamehe...
Ila mzee wako ni noma!!!...asee!!!
...................OK :fear:
lol...niko off-topic kidogo hapa mkuu nisamehe...
Ila mzee wako ni noma!!!...asee!!!
ha haaa, pole rafiki....
wanasema huko kwao imezoeleka.... wanakodi hadi salon kama harusi
kuna mfiwa (mjane) alivaa mchuchumio na kimini kwenye mazishi ya mumeo eti vimada wa mumewe wakija msibani waone naye yumo.... sasa huo mchuchumio sijui miguu inaweza kurusha hatua! kaazi kweli
shangaa wewe rafiki...Aiseee; tupo tofauti sana hadi michuchumio tena!
mi mwenyewe nilipata ganzi......Duh yaani msiba wa kakake kabisa . Ama kweli kuishi kwingi kuona mengi na mjini kuna mengi . Unajua nilipokua nasoma huu uzi nilidhani mwisho itaishia alikua anatania kumbe ni msiba tena wa ndani. Kweli maendeleo ya sayansi na teknolojia. Sasa hawa wanetu enzi zao sijui zitakuaje manake sipati picha.
yeye ndo mfiwa ujuealafu ukimfuatilia kw karibu dada huyo utagundua kuwa hata mchango msibani hajatoa
Kweli binadamu tunatofautiana! Mi hata kama kuna sale ya khanga, sidhani kama nitanyanyuka kwenda dukani.
wangoni haya bado hayajatukuta.......Kweli binadamu tunatofautiana! Mi hata kama kuna sale ya khanga, sidhani kama nitanyanyuka kwenda dukani.
mmmh . . . ndugu yangu!! Bora hata yasifike yaishie hukohuko mjini, sie wengine mambo ya kutokelezea kibongo movie ilhali ni mkanda wa msiba hatuyawezi mweeeh!wangoni haya bado hayajatukuta....... utafanyia wapi kule mpitimbi? kanga utaletewa mdogo wangu
mi nidhani ni ushamba wangu tu ndo unanisumbua
aisee, nimekuja uzi ukiwa mrefu so nilishindwa kupitia kila kitu; my bad!
so ukisema niwaulize wachaga, maana yake it is a normal thing au? help me there maana uzi ni mrefu sana kupitia each and every post it will take all my time and l had a long day today.
nilienda kwenye msiba wa baba wa rafiki nikakuta mama anaburudika na muziki wa Yesu, hii ilikuwa kidini zaidi..... hakuna kulia ni kuburudika tu kuwa kaenda kwa Baba..... nilijishangalia, lol!
juzi juzi kuna rafki yangu wa kike kafiwa na mumewe,basi ikawa tupo kanisani katika kuaga,lakini nikaona kama ndugu wa mume wanamtenga hv? nikauliza rafki yetu mwingine ndo akanipa mkasa,kumbe yule dada jana yake alikaa chumbani akajishonea hilo sijui weaving akajiremba sasa ndugu wa mume wakakasirika kweli,yaani mwenzio kafa hata kuzikwa hajazikwa we unajiremba....wameenda kuzika mkoani,lazima kutakua na shida sana huko. lakini watu hawana upendo wa kweli nowdays.Juzi nilikuwa namtafuta shosti kwa dharura, akaniambia yupo salon anasuka, akanielekeza nikaona nimfwate....
wakati tunaongea, kulikuwa na mrembo mmoja pembeni anashonea weaving na kutengenezwa kucha, kope, nyusi, n.k.
mara simu ya mrembo ikaita, maongezi yakaanza..... "yaani we acha tu, ndo mambo ya dunia lakini, Tunamshukuru Mungu..... asante sana....
tunaaga kesho mchana na safari ya kwenda Moshi kwa mazishi itaanza baada ya kuaga, kweli tutammiss sana kaka yetu....."
baada ya hapo maongezi yakawa yanaendelea akawa anasimulia kuwa kakake kabisa kafariki, kaumwa siku 2 tu kafa.....
sijui ndo ukijijini au ushamba wangu! kweli nilisikitika sana.....
sipati picha kakangu anafariki, mimi naweza kuwa na nguvu kwenda salon kujipiga msasa ili niende kuzika kakangu au ndugu yangu wa karibu.
Nikajiuliza mambo mengi sana.
1) ni kwamba watu siku hizi wamezoea sana misiba kiasi kwamba wanaona ni kitu cha ajabu tu kufiwa?
2) watu hatuna uchungu tena na ndugu zetu?
3) u-kisasa unatufanya tuwe hivyo?
kweli mahusiano na ndugu/jamaa/marafiki yamepungua kiasi hiki mpaka tunachukulia misiba ya ndugu zetu kirahisi namna hii?